MWONGOZO WA TUMBO LISILOSHIBA

Yaliyomo

Tumbo Lisiloshiba Said A. Mohamed………………………………….1.
Mapenzi ya Kifaurongo KennaWasike……………………………………. 17
/Shogake Dada ana Ndevu Alifa Chokocho ………………………………….31
Shibe Inatumaliza Salma Omar Hamad ……………………………41
Mame Bakari Mohammed Khelef Ghassany……………….45
Masharti ya Kisasa Alifa Chokocho ………………………………….53
Ndoto ya Mashaka Ali Abdulla Ali ……………………………………62
Kidege Robert Oduori ……………………………………70
Nizikeni Papa Hapa Ken Walibora ……………………………………76
Tulipokutana Tena Alifa Chokocho…………………………………. 82
Mwalimu Mstaafu Dumu Kayanda…………………………………. 88
Mtihani wa Maisha Eunice Kimaliro………………………………… 96
Mkubwa Ali Mwalimu Rashid ………………………….104
iii.
1. TUMBO LISILOSHIBA
Historia ya Mwandishi.
Hadithi hii imeandikwa na Prof. Said Mohammed, mwandishi
mtajika ambaye amewahi pia kuandika vitabu vingine vitajika
kama vile Riwaya ya Utengano. Mwandishi huyu bila shaka ni gwiji
katika ulingo huu kwani amewahi kuandika kazi zingine za fasihi
andishi zikiwemo tamthilia, mashairi na hadithi fupi.
Dhamira
Dhamira ni funzo kuu litokanalo na kazi ya sanaa au lengo kuu la
mwandishi. Mwandishi wa hadithi ya Tumbo lisiloshoba alidhamiria
kufunua uozo unaoletwa na ubinafsi na tamaa katika jamii. Aidha
anawajasirisha wanaoathiriwa kuwa wanaweza kukubali madhila
wanayofanyiwa ama kupinga dhulma hizo na kusimama wima na
kutetea haki zao.
Ufupisho wa Hadithi.
Hadithi hii inaangazia maisha ya watu wanaoishi katika mtaa wa
Madongoporomoka, mtaa ambao umepakana na jiji linalokuwa
kwa kasi mno. Jiji hili limeshiba kwa wingi wa mijengo iliyojengwa
k i a s i c h a k u a n z a k u t i s h i a u we p o wa m t a a d u n i wa
Madongoporomoka. Uvumi unawakia wanamadongoporomoka
kwamba mtaa wao utanyakuliwa ili upanuzi wa mji ukie eneo hilo.
Mwanzoni ulianza kama tu uvumi uliokuja na kupita bila ya
wanamadongoporomoka kuwa na uhakika nao. Ingawa uvumi huo
u l i i s h i a k u t ow e k a , M z e e M a g o k a t u h a k u wa r u h u s u
wanamadongoporomoka kutupilia mbali wazo la uvumi huo kutimia
na wao kuishia kufurushwa. Anawaleta pamoja wanakijiji wenzake
ili kutafuta suluhishi kwa tatizo lililokuwa limewakodolea macho.
Kwa pamoja wanakijiji wote wanakubaliana kutoondoka na liwe
liwalo. Hata ikiwa watafurushwa, wanaamua kutetea mtaa wao na
kusalia.
Kisadfa, bwana mmoja mwenye tumbo kubwa anawasili kwenye
mkahawa wa Mzee Mago na kutaka kupewa chakula chote
kilichoandaliwa. Ajabu ni kuwa anapokabidhiwa chakula hicho,
1.
anafyeka chote fyuu! Ni ajabu kwani huyu jamaa ana “Tumbo
lisiloshiba”. Baada ya kula na kutoa bweu kubwa lenye harufu
mbaya, jitu linalipa na kuahidi litarejea siku iliyofuatia.
Siku iliyofuata wanamadongoporomoka wanagutushwa na
maporomoko yanayotokana na vibanda vyao kubomolewa na
mabuldoza. Wanafurushwa wote kwa nguvu. Vibanda vyao
vinabomolewa na wao kuishia kufukuzwa. Ajabu ni kwamba
“Bwana Tumbo” anarejea kama alivyoahidi. Ila wakati huu yuko
ndani ya gari kubwa na dereva anayemwamrisha. Hivyo amerudi
kula kila kitu kama alivyoahidi ila wakati huu amekuja kula
m a s h a m b a y a o . M z e e M a g o a n a w a s h a w i s h i
wanamadongoporomoka kutoondoka, licha ya dhulma hizo.
Umoja wa wanakijiji hawa unawaokoa kwani muda mfupi
baadaye, vibanda vyao vinaanza kuota tena. Wanafaulu kuzuia
tamaa ya tumbo kubwa lisiloshiba la mji kutokula mashamba yao.
MAUDHUI
Baadhi ya maudhui yanajitokeza katika hadithi hii ni kama vile:
a) Ubinafsi na tamaa
b) Unyanyasaji
c) Utetezi wa haki
d) Umaskini
e) Utabaka
f) Migogoro
a) Ubinafsi na tamaa (Tumbo lisiloshiba)
Haya ndiyo maudhui makuu katika hadithi hii. Maudhui haya
yanajengeka kwa kutazama jinsi ambayo wahusika fulani
hawatosheki na mengi waliyokuwa nayo na hivyo basi kutamani
vidongo vya wengine na kutaka kuwahini. Wakubwa wa jiji
wanadai kwamba jiji limejaa tayari hadi Pomoni. Halijaacha hata
nafasi ya mtu kuvuta pumzi.
2.
Jiji lenyewe limekuwa limesheheni usa, ujumi na tamaduni mbali
mbali. Jiji limejaa hoteli, mikahawa, departmental stores, casinos,
viwanja vya gofu, viwanja vya tenisi, voliboli, mpira wa vikapu,
raga, kabumbu, vyuo vikuu, mahakama, hospitali, majumba ya osi
na mengine mengi. Haya yote yamekuwa yamesimama wima jijini.
Hapajasalia hata nafasi kidogo ya kuvuta pumzi. Hivyo basi
wakubwa wa jiji waonelea vyema kwa ardhi ya watu wa
Madongoporomoka kutwaliwa. Hii ni tamaa ya hali ya juu.
Wanataka wajenge majumba ya kifahari huko. Hawataki kuwalipa
wenye ardhi hiyo dhamana inayofaa bali wanataka tu kuwafurusha
wanamadongoporomoka.
Mhusika “Bwana Tumbo” anaingia kwenye mkahawa wa Mzee
Mago. Ukubwa wa tumbo lake unashangaza wengi. Ni dhahiri kuwa
huyu mtu ni mlaji hodari. Jamaa huyu anaishi kuulizia chakula
kilichopo kwenye mkahawa na kukila. Anakula chakula chote
kilichoandaliwa kwa walaji wengine wote. Anamaliza chakula na
kuongezewa kingine. Anakula nyama ya kuchoma, mchuzi wa
nyama, wali wa nazi, samaki wa kukaanga, chapatti kadhaa na
kuishia kuteremshaa na chupa mbili za Coca cola. Anafagia
mkahawa wote. Anaahidi kurejea siku itakayofuata na kutaka
chakula kipikwe mara mbili Zaidi ya kile kilichopikwa siku hiyo. Hii ni
tamaa ya ajabu. Watu waliokuwepo kwenye mkahawa wanabaki
kushangaa ni vipi mtu anakula chakula chote kilichoandaliwa walaji
wote kwenye mkahawa?
Bwana mwenye tumbo ana tamaa ya mashamba. Anajaribu
kuwafurusha wanamadongoporomoka kutoka kwenye makaazi
yao. Anawarausha asubuhi na mapema kwa mabuldoza
yanayobomoa makaazi yao. Inakusudiwa kuwa majengo
yatajengwa katika ardhi hii inayotamaniwa sana na wenye jiji.
Anwambia Mzee Mago kuwa amekuja kula mashamba yao. Hii ni
tamaa ajabu ya mashamba yaliyo na wenyewe.
3.
Jiji lina tumbo ambalo halishibi. Jiji hili limepambwa vyema na
majumba ya kifahari. Jiji limejaa hoteli, mikahawa, departmental
stores, casinos, viwanja vya gofu, viwanja vya tenisi, voliboli, mpira
wa vikapu, raga, kabumbu, vyuo vikuu,mahakama na hata
hospitali. Ajabu ni kuwa jiji hili halijatosheka kwa usa wake. Jiji
linataka kupanua tumbo lake hadi katika mtaa wa
Madongoporomoka.
a) Unyanyasaji
Hii ni hali ya wahusika kuhiniwa haki ambayo wanastahili na
badala yake wengine kupewa haki hiyo kwa haramu.
Wanamadongoporomoma wananyanyaswa na viongozi wa jiji.
Licha ya wao kuwa wamiliki halisi wa mashamba yao,
wanapangiwa hila ya kunyang’anywa vipande vyao vya ardhi.
Ardhi hiyo inapangiwa njama ya kunyakuliwa bila ya wao kulipwa
dia inayostahili. (Uk 4)
WanaMadongoporomoka pia wananyanyaswa kisheria. Ni mujibu
wa sheria kuwatetea watu wote ambao wamehiniwa au kutendewa
isivyo haki. Mzee Mago anafahamu vyema kwamba kuna
uwezekano mkubwa wa wao kupokonywa mali zao ilhali sharia
itumiwe kuwakandamiza yeye na maskini wenzake.Anaomba
waishie kumpata hakimu ambaye ni mpenda haki ili haki isiuliwe na
asiyestahili kuishia kutetewa na sharia mbovu. (Uk 2)
Majengo makubwa yaliyoko jijini yananuia kuwanyanyasa
wanamadongoporomoka na kumeza vipande vyao vya ardhi.
Vipande hivi vya ardhi vinanuiwa kutumika ili kuwahi kujenga
majengo bora Zaidi.
b) Utetezi wa haki
Mzee Mago ametumiwa na mwandishi kama kielelezo cha mtetezi
wa haki ya wakaazi wa kijiji wa madongoporomoka. Mhusika huyu
anawatetea madongoporomoka kutokana na maonevu ya wakuu
wa jiji.alijitahidi kuzuia njama ya watu wakubwa kutaka kuchukua
ardhi za watu wadogo. Mzee Mago aliwafuata wengine ili
kuzungumza kuhusu haki ya unyang’anyaji wa mashamba yao. Yeye
hupiga mbio huku na kule kujaribu kuzuia haki isiangamizwe. (Uk 2)
4.
Kwa kuwa Mzee Mago anafahamu kwamba haki inauzwa na
kupewa watu wasiostahili. Anajua kuwa haki itauzwa. Anafahamu
kwamba haki itapewa wengine wasiostahili. Hivyo basi anamtafuta
wakili mzuri ambaye hatasaidiana na viongozi dhalimu ili kuwahini
mashamba yao.
Mzee Mago anawahamasisha wanamadongoporomoka kutokubali
kufurushwa kutoka maeneo yao. Hawaruhusu watu kusahau uvumi
wa wao kufurushwa. Anawaita katika kikao na kuwakumbusha
uwezekano wa hao kufurushwa. Anawaongoza kutokubali
kufurushwa ikiwa wakubwa wa jiji watakuja kuwaondoa kwenye
makaazi yao. Baadaye wanamadongoporomoka wanapovamiwa,
wanakataa kuondoka hadi wiki tatu baadaye ambapo makaazi
yao yanarudi kuchomoza kama uyoga. (Uk 11)
a) Umaskini
Ni hali ya kukosa mali/hali ya ufukara au ukata. Umma wa
Madongoporomoka unaishi katika hali mbaya ya kimaskini.
Mandhari ya kijiji hiki ni ya kimaskini na kufedhehesha mno. Kuna
mashonde na vinyesi. Kuna vibanda vya uchwara vinavyozungukwa
na uoza na bubujiko la maji machafu. Kuna uvundo unaopasua
mianzi ya pua. (Uk 4). Bila shaka, mandhari haya sio ya mahali
ambapo mtu anaweza kufurahia kuwa. Ni mandhari ya mahali
ambapo ni masikini tu ndio wanaishi.
b) Utabaka
Hii ni hali ya wahusika kugawika katika makundi tofauti tofaauti
kulingana na uwezo wao wa kiuchumi. Kuna tabaka la matajiri na
masikini. Kila tabaka limejikita katika shughuli zao wenyewe za
kutetea matumbo yao. Masikini wanapigania kutetea makaazi yao
ya kimaskini. Wanakataa kata kata kuhiniwa na wachache matajiri
ambao wanamiliki mali nyingi. Kwa upande mwingine, matajiri
wana matumbo yasiyoshiba. Wananyakua mashamba ya masikini
kwa minajili ya kutaka kuendeleza ujenzi wa majumba ya kifahari.
Hivyo basi, matajiri wanaishi kuwafurusha masikini kutoka kwenye
makaazi yao. (Uk 10-11)
5.
a) Migogoro
Katika hadithi hii panazuka migogoro mbali mbali baina ya
wahusika tofauti. Kuna tofauti nyingi ambazo zinazuka kati ya
wahusika mbali mbali katika hadithi. Baadhi ya migogoro hii ni
kama vile:
a) Mgogoro baina ya Wakuu wa Jiji na wanakijiji wa
Madongoporomoka.
Mgogoro huu unatokana na hali ya jiji kupanuka na
kusheheni kila aina ya majumba kiasi cha kukosa nafasi ya
mtu kuvuta pumzi. (Uk 4)Kutokana na hali hii, wakuu wa jiji
wanaonelea kuwa mahali pazuri pa kupanua shughuli za jiji
lile ni huko Madongoporomoka. Huko ndiko kuna vijishamba
ambavyo havina kazi. Vishamba ambavyo vinapaswa
kupambwa na majumba mazuri ya kifahari. Kwa upande
mwingine, maskini hawa wanaenzi vijumba vyao pamoja na
mazingira yao na hawako tayari kuondoka kwa njia yoyote
ile. Hali hii inazua mgogoro kati yao na wakuu wa Jiji.
b) Mgogoro baina ya Bwana mwenye tumbo na wana-
Madongoporomoka.
Bwana Mwenye tumbo ananuia kula mashamba ya wana-
Madongoporomoka. Kwa upande mwingine, wanakijiji hawa
wanakaidi amri ya kuondoka, pamoja na madhila ya
kubomolewa makaazi yao wanamoishi. Licha ya mateso yote
wanayoelekezewa wana-Madongoporomoka, wanakataa
kuondoka katika mashamba yao na kuruhusu ujenzi wa
majumba ya kifahari kutekelezwa. Ni wazi kuwa huu ni
mwanzo tu wa mgogoro kati ya wahusika hawa hawa na
mporaji huyu wa ardhi.
6.
MBINU ZA LUGHA NA UANDISHI.
Hizi ni mbinu ambazo mwandishi hutumia ili kuleta mvuto katika kazi
yake. Mbinu za uandishi ni sawa na mtindo wa mwandishi. Hizi
zinahusu upekee wa mwandishi kwa namna anavyoichora kazi
yake. Mbinu za uandshi ni mbinu ambazo mwandishi hutumia ili
kutupa sisi wasomaji ujumbe wa ziada. Mbinu hizi ni kama vile
matumizi ya ndoto, barua, mbinu rejeshi,n.k. mbinu zilizotumiwa
katika hadithi hii ni pamoja na:
1. Takriri
Takriri ni mbinu ya kifasihi ya kurudiarudia neno au kifungu cha
maneno ili kusisitiza au kulitilia mkazo. Mifano ya takriri ni kama
ifuatayo:
a) Ulianza uvumi. Uvumi ukageuka nong’ono. Nong’ono
zikafumbua kinywa kueneza wasiwasi. Wasiwasi ukawa
hofu… (Uk 1).
b) …gwa sahau hiyo ni tokeo la lile lile la umoja katika uwili.
(Uk 1)
c) Mzee Mago kajifunza kutosahau. Kutosahau hamkumpi hata
kidogo… (Uk 2)
d) Itikadi ya wakubwa ilikuwa bado ni ile ile. (Uk 2)
e) Hawawezi…hawawezi, hawawezi, kabisa hawawezi! (Uk 5)
2. Kinaya
Kinaya ni hali ambayo mhusika anasema au kutenda kinyume
na matarajio. Mifano ya kinaya ni kama ifuatayo:
a) …maana siku hizi wanasheria waaminifu ni adimu kama
haki yenyewe. (Uk 2)
b) Ilishikilia kwamba jiji halina nafasi tena. Yaani limejaa kila
pahala. Limejaa hiki na kile, hili na lile. Limejaa hadi
pomoni. (Uk 3-4)
7.
c) Halikuacha hata nafasi ya kuvuta pumzi. (Uk 4)
d) “sharia gani hiyo iko mikononi mwetu?” Aliuliza Mzee
Mago. “Sheria kila wakati iko mikononi mwao.” (Uk 6)
a) “Nitakula chakula chako chote ulichopika kuwauzia
wateja wako leo.” (Uk 8)
1. Taswira
Taswira ni maelezo ambayo yanaunda picha fulani katika akili za
msomaji. Mifano ya taswira ni kama ifuatayo:
a) Kuna mashonde na vinyesi. Kuna vibanda vya uchwara
vinavyozungukwa na uozo na bubujiko la maji machafu. Kuna
uvundo unaopasua mianzi ya pua. (Uk 4).
b) Wakati huu ndipo pua za wazungumzaji hawa ziliponasa
harufu za vyakula vilivyotoka jikoni. Harufu mchanganyiko
zilizowaingia puani na kukaanza kulambatia na kukaza mate
vinywani mwao. (Uk 6)
c) Jitu lilikuwa limevaa suti nyeusi na shati jeupe. Limekabwa
shingoni na tai ya buluu iliyozama kwenye misuli ya shingo
fupi nene…(Uk 7)
d) Naam. Vyakula vilipakuliwa. Wali na nazi. Mchuzi na nyama.
Nyama ya kuchoma kwa mkaa na bakuli la kachumbari.
Samaki wa kukaanga. Chapatti kadhaa za duara… (Uk 8)
1. Maswali ya Balagha
Balagha ni mbinu ambapo mwandishi huuliza maswali yasiyohitaji
majibu. Maswali haya hulenga kumfanya mhusika au msomaji kukiri
kwa kina. Kwa mfano:
a) Aaa, kuna jabu gani lakini mvua ikinyesha? Si kila siku
huanguka kupunguza joto …? Si huanguka kuburudisha nafsi
zinazohaha na kukata tamaa? (Uk 1)
b) Nani angewashauri wao mburumatari? Sauti zao hazikustahi
kusikika, seuze kusikizwa? (Uk 3)
8.
c) Kwani si kila mtu anafaa kujua kuwa kimya kirefu kina
mshindo mkuu? (Uk 3)
d) Tuondoke twende wapi? (Uk 5)
e) Kuwe na mazungumzo gani hasa yatakayomchangamsha
kila mtu wakati huu kuliko uvumi ulioanza tena kuvuma? (Uk 5)
f) Aaa, nani anayejua hatimaye? Kesho yenyewe haijazaliwa
seuze fumbato ndani ya kesho yenyewe?
g) Chupa mbili za Coca cola zifae nini kwa jitu kuza kama hilo?
(Uk 8)
h) Wakawa wanatazamana kwa wakionyesha hawaamini nini
kinachotokea. Itawezekanaje?
1. Kuchanganya Ndimi
Hii ni mbinu ya uandishi ambapo wahusika huzungumza kwa
kutumia lugha zaidi ya moja ili kuonyesha hali yao na hisia zao
katika mazungumzo. Mbinu hii humwezesha mhusika kujieleza
vyema Zaidi kwa kutumia msamiati ambao hauko katika lugha
fulani. Kwa mfano:
a) Chupa mbili za Coca cola zifae nini kwa jitu kuza kama hilo?
(Uk 8)
b) Jitu hilo lilikuwa limeketi nyuma ya gari kubwa aina ya Audi
Q7…(Uk 10)
c) Simama kidogo Chauffer… (Uk 11)
9.
2. Taharuki
Taharuki ni mbinu inayotumiwa na waandishi ili kuteka hisia na
hamu ya wasomaji kutaka kuendelea kusoma zaidi. Katika
kufanikiwa kujenga taharuki, mwandishi husuka matukio
yalito na mshikamano na mtiririko ambao humvutia msomaji
asiiweke chini kazi hiyo pindi aanzapo kuisoma hadi akie
kikomo chake.
a) Ulianza uvumi. Uvumi ukageuka nong’ono. Nong’ono
zikafumbua kinywa kueneza wasiwasi. Wasiwasi ukawa
hofu… (Uk 1). Msomaji anajiuliza, Ni jambo gani hili ambalo
linatarajiwa kutendeka?
b) Kwa Mzee Mago, iliyobaki sasa ni kutazamia siku ya
kulipuka mambo…(Uk 3)
Ni mambo yepi yatalipuka? Hii inasalia kama taharuki.
c) Kesho nitaka hapa tena. Niwekee chakula mara mbili
kuliko hiki cha leo…(Uk 9)
Tunashangaa ikiwa jitu hilo kweli litarudi.
1. Jazanda/ Istiari.
Jazanda ni mbinu ambayo inaonyesha fumbo lililotumiwa na
mwandishi kurejelea hali fulani kwa njia che. Istiari kwa upande
mwingine inalinganisha moja kwa moja kitu au hali na nyingine
lakini bila ya kutumia maneno ya ulinganisho. Mifano:
a) Angepoaje na ule moto unaomlipukia kila mtu pale mtaani
umeacha mpaka sasa kovu bichi moyoni…? (Uk 2)
10.
b) Wakubwa hawatambui kuwa kwamba jambo hilo la
kuwafanya wao takataka tu ndilo linalowakasirisha… (Uk 3)
c) Sahau imebaki vilevile kutanda giza na kufunga milango ya
wasiwasi vichwani mwa watu… (Uk 5)
d) Bweu likapasuka na kutoa uvundo wa mnyama aliyeoza…
(Uk 9)
Hii ni ishara ya jinsi jitu hili litawahangaisha wanakijiji hawa
baadaye.
2. Tashbihi/Mshabaha
Tashbiha/Tashbihi/Mshabaha ni maneno yanayofananisha kitu,
jambo au kitendo na kingine kwa kutumia vihusishi kama vile ‘kama’,
‘mithili’, ‘ja’, ‘mfano wa’ na kadhalika. kwa mfano:
a) …maana siku hizi, wanasheria waaminifu ni adimu kama
maziwa ya kuku! (Uk 2)
b) Ulikuwa ukitukuta ndani kwa ndani kama moto ya makumbi.
(Uk 3)
c) Umebaki tu ukining’inia hewani kama mvua inayotarajiwa
kunyesha…(Uk 4)
d) Kauli ya jitu hilo ilimwinua Mzee Mago kama mtu
aliyechapwa na bakora. (Uk 7)
e) Lilipokula, lililamba sahani zote kana kwamba lilikuwa na
jukumu la kuziosha.(Uk 9)
f) …vibanda vya Madongoporomoka viliota tena hapo kama
uyoga. (Uk 11)
11.
1. Tashihisi/Uhuishaji
Hii ni mbinu ya lugha ya kuweka hisia na uhai katika vitu
visivyokuwa na uhai. Pia kuna uwezekano wa kuwapa wanyama
uwezo na hulka za binadamu. Mifano:
a) Nong’ono zikafumbua kinywa kueneza wasiwasi. (Uk 1)
b) Maisha ndugu yangu ndiyo- maisha ndiyo yanayotukaba
koo akina sisi! (Uk 1)
c) Yeye hupiga mbio huku na kule kujaribu kuzuia haki
isiangamizwe…(Uk 2)
d) Mzee Mago lakini hairuhusu sahau iketi na kutawala
kichwani mwake. (Uk 2)
e) Aliwakumbusha kuwa maendeleo yanadai mchango wa kila
mtu…(Uk 2)
f) Kesho yenyewe haijazaliwa, seuze fumbato…(Uk 5)
g) Sahau imebaki vilevile kutanda giza na kufunga milango ya
wasiwasi vichwani mwa watu… (Uk 5)
h) Kauli ya jitu hilo ilimwinua Mzee Mago kama mtu
aliyechapwa na bakora. (Uk 7)
i) Haikuchukua muda mrefu akili zilipowaamsha kuwapeleka
maana ya kile…(Uk 10)
2. Chuku
Ni mbinu ya kutilia mazungumzo chumvi ili kuyafanya yavutie
Zaidi. Kwa mfano:
a) K w a m i u j i z a , n d i p o j i t u l a m i r a b a m i n e
lilipoingia…halikujulikana lilipotoka. Liliingia tu ghaa..(Uk
6)
b) Lile tumbo lake limezidi kufura na ndani ya tumbo, ugomvi wa
vyakula ukawa unapwaga kwa mingurumo ya radi iliyosikika
hadi nje. (Uk 9)
12.
c) Mstari huo ulikuwa umefuatana na mpasuko mkali wa radi na
umweso uliomulika mpaka ndani ya mioyo ya watu. (Uk 10)
d) Jitu hilo lilimwaga tabasamu mfululizo iliyoenea eneo lote la
Madongoporomoka. (Uk 10)1. Nidaa
Ni mbinu ya kuonyesha hisia aliyo nayo mhusika. Hujulikana kwa
kutumia alama ya hisi. Kwa mfano:
a) Maisha ndugu yangu ndiyo- maisha ndiyo yanayotukaba koo
akina sisi! (Uk 1)
b) …maana siku hizi, wanasheria waaminifu ni adimu kama
maziwa ya kuku! (Uk 2)
c) Pale lilipoketi, lilionekana kupapa jasho ovyo! (Uk 7)
d) Halikubakisha hata chembe moja ya chakula chochote
alichopewa! (Uk 9)
e) Hazitatuhamisha kabisa hizi fujo zenu! (Uk 11)
2. Tanakuzi.
Ni mbinu ya kutaja vitu viwili ambavyo sifa zao zimepingana.
Kwa mfano:
a) “Hata hivyo, kila mtu, mdogo kwa mkubwa, kike kwa kiume…
(Uk 2)
b) Aliwakumbusha kuwa maendeleo yanadai mchango wa kila
mtu, maskini au tajiri. (Uk 2)
c) Lile jitu lilimkata maneno Mzee Mago, Wakubali,
wasikubali…(Uk 8)
d) Watu wanakimbia huku na huku, huku na kule, mbele na
nyuma…(Uk 10)
e) Kike kwa kiume, vijana kwa wazee, watoto kwa watu
wazima…(uk 10)
13.
WAHUSIKA NA UHUSIKA
a) MZEE MAGO
Huyu ndiye mhusika mkuu ambaye ametumiwa na mwandishi kama
kielelezo cha watetezi wa haki. Ametumika kuwatetea wanyonge
kutokana na madhila ya matajiri wanaotaka kuwapokonya
mashamba yao. Sifa zake ni kama zifuatazo:
i) Ni mtetezi wa haki.
Anakataa kutazama huku wanakijiji wakihiniwa mashamba yao.
Anamtafuta wakili ambaye hajahongwa ili kutetea haki ya
w a n y o n g e . I s i t o s h e , a n a k a t a a k u w a r u h u s u
wanamadongoporomoka kusahau uvumi uliokuwepo hapo awali
kuhusu uwezekano wa vipande vyao vya ardhi kuchukuliwa.
ii) Ni mwenye hekima/busara.
Anafahamu vyema matokeo ya wingu linalotarajiwa kutua. Hivyo
anajiandaa na pia kuwaandaa wanakijiji ili yatapowasili madhila,
wawe tayari wameungana kupigania haki zao.
iii) Ni mwenye bidii.
Ni yeye tu aliye na mkahawa pale madongoporomoka, ishara ya
kwamba ni mtu mwenye bidii ya mchwa.
14.
iv) Ni mwenye ushawishi
Anafaulu kuwahamasisha wanakijiji wote kujiandaa ili kukabiliana
na vita vinavyokuja vya kunyang’anywa vipande vyao vya ardhi.
Isitoshe anawaandaa wanamadongoporomoka kupinga hila
zitakazokuja na kukataa kuondoka kwenye mtaa wao. Hatimaye
wanapovamiwa na kubomolewa makazi yao, wanakaidi na
kukataa kuondoka, jambo linalowapa ushindi baadaye.
v) Amepevuka
Anafahamu ka uzito wa kesi na ubishi unaotokana na ardhi.
Isitoshe ana ufahamu mzuri wa namna ambavyo haki haipatikani
kwa urahisi. Hivyo anaamua kumtafuta wakili aliye mwaminifu
ambaye hatimaye anawaokoa kutokana na makucha ya matajiri
wenye tamaa. Wanarudia kujenga vibanda vyao upya.
a) JITU LENYE TUMBO
Mhusika huyu hatujapewa jina lake halisi ila matendo yake ndiyo
yanashangaza. Sifa zake ni kama zifuatazo:
i) Ni katili
Hana huruma anapobomoa makazi ya maskini. Anawafumania
asubuhi na mapema na kuwafurusha. Anabomoa makazi ya watu
ambao hawana pahala pengine pa kuita kwao, huku akiangua
kicheko akiona namna wanavyohangaika.
15.
ii) Mwenye tamaa
Anatamani ardhi za maskini wa Madongoporomoka na
kuwapangia njama ya kuwafurusha kutoka makwao. Ingawa ana
uwezo wa kutumia buldoza na polisi, anaishia kushindwa katika wizi
wake na maskini hawa kurejelea makaazi yao.
iii) Mwenye dharau/Kiburi
Anawazungumzia Mzee Mago na wenzake pale kwenye mkahawa
kwa dharau na mabezo.
iv) Ni Mla
Anafyeka vyakula vya aina mbali mbali bila kusaza chochote.
Vyakula vyote vilivyokuwa vimeandaliwa wateja pale kwenye
mkahawa vinaliwa na yeye pekee. Mwishowe anatoa bweu kubwa
linalochafua hewa yote pale.
Mhusika huyu ametumiwa kama kielelezo cha watu wenye tamaa
mbaya ya mali, waliojawa na ukatili na wanaoweza kutenda ukatili
wowote ili kupata mali.
Kabwe, Bi.Suruta na Bi. Fambo.
Hawa ni wana-Madongoporomoka ambao wanaoshirikiana na
Mzee Mago ili kujiandaa kwa wingu ambalo lingeanguka hapo
baadaye. Ni wazi kwamba wahusika hawa ni wenye hekima na
waliomakinika kwa mambo yajayo. Wahusika hawa wametumiwa
kama kielelezo cha viongozi wenye mioyo ya ujasiri wa kupigania
jamii zao.
16.
2.MAPENZI YA KIFARAUNGO
Historia ya Mwandishi.
Mwandishi wa hadithi hii anaitwa Kenna Wasike. Ni mwandishi
ambaye yuko katika harakati zake za mwanzo katika ulimwengu
wa uandishi. Yeye ni mwalimu aliyesomea chuo kikuu cha Nairobi.
Dhamira
Mwandishi amekusudia kutahadharish wasomaji wake dhidi ya
kugawanywa kwa misingi ya utabaka. Analenga kukashifu
migawanyiko ya watu kwa kuzingatia uwezo wao wa kiuchumi.
Ufupisho wa Hadithi
Mwandishi anatumia nafsi ya kwanza katika masimulizi yake.
Anatupa hadithi yake mwenyewe akiwa chuo kikuu. Ingawa
amefaulu kuka chuo kikuu, maisha sio mepesi kwa namna yeyote.
Wazazi wake ni maskini hohe hahe wanaopigania mikono kuka
kinywani tu. Bidii yake ndiyo ilimkisha katika chuo kikuu. Msimulizi
anapoka katika chuo kikuu, anashangaa namna ambavyo
wanafunzi wengi wanaandamana kwa mapenzi. Ingawa
anatamani, haimpitii mawazoni mwake ya kwamba naye pia
angeweza kuwa na mpenzi huko chuoni. Masomo chuoni ni magumu
na ambayo hayaeleweki kwa wengi wa wanafunzi hao, ingawa
wanajitahidi. Mwalimu anayewafunza ni Dkt. Maboga ambaye
anatema dhana nzito nzito za fasihi. Wanafunzi wengi wanauliza
maswali ilikuelewa Zaidi anavyomaanisha mwalimu huyu. Bila shaka
hawaelewi mambo anayosema huyu mwalimu, lakini nani
atadhubutu kumuzomea daktari mzima?
17.
Siku moja baada ya msimulizi kupika uji wake na kujiandaa kunywa,
anasikia mtu akibisha mlangoni. Anapofungua, anamkuta binti
mmoja mrembo ambaye baadaye anagundua kwamba ni
mwanafunzi mwenzake nye darasa moja anayeitwa Penina. Penina
anadai kwamba anampenda Dennis bila kujali umaskini wake.
Ajabu ni kuwa Penina ni binti wa Waziri. Ni kinaya kwa msichana wa
haiba yake kumpenda maskini kama Dennis. Baada ya masomo
yao, Dennis na Penina wanaishi pamoja huku wazazi wa Penina
wakilipa kodi ya nyumba na matumizi yao yote. Dennis anajaribu
kutafuta kazi bila mafanikio. Anapata fursa katika shirika la
uchapishaji wa magazeti. Anapopatikana katika chumba cha
udodosi, anashindwa kufungua kinywa chake na kujitetea ni kwa
nini anahitaji kazi ile. Dennis anafurushwa kutoka chumba cha
udodosi kwa haya nyingi usoni na majuto mengi moyoni.
Anaporejea nyumbani, anamkuta Penina ameketi akitazama
televisheni. Anataka kupewa chakula ila anaariwa kuwa hakuna
chakula chochote kile. Penina anamwarifu kuwa chakula hakipo
kwani yeye Dennis hakuwacha chochote cha kuliwa. Kisha Penina
anataka kujua ikiwa Dennis amefaulu kupata kazi. Dennis
anapojibu kwamba hakufaulu, jibu la Penina linamshangaza.
Penina anamwambia kwamba anajutia uamuzi wake kuolewa
kwake. Anajuta kutowasikiliza wazazi wake kwani walimwonya
kutokana na Dennis. Anadai kuwa anataka kuolewa na mtu mwenye
kazi nzuri na pesa. Kisha Penina anishia kumfukuza Dennis kutoka
kwake. Anamwamrisha afunge virago vyake na kuondoka. Dennis
anapomdadisi kuhusu mapenzi yao, anamhakikishia kuwa yeye
hataki kuolewa na maskini kama yeye. Ni ajabu kuwa mapenzi ya
Penina yameyeyuka.
18.
Ni mapenzi ya kifaraungo. Dennis akiwa anaondoka na begi lake,
anasikia sauti ikimwamuru nyumba ile aione paa na asiwahi kurejea.
Hali hii inamletea majuto si haba. Kweli mapenzi ya Penina yalikuwa
na kifaraungo. Yaguzwapo tu na wimbi ndogo yananyauka.
MAUDHUI
Baadhi ya maudhui yanajitokeza katika hadithi hii ni kama vile:
a) Elimu
Hii ni hali ya mhusika kupata maarifa yanayonuiwa kumpevusha
kimawazo. Kuna aina mbili kuu za elimu:
i) Elimu ya Vitabu.
Hii ni elimu ambayo wahusika huipata kwa kuhudhuria madarasa
shuleni na kuelimishwa katika masomo mbalimbali. Baadhi ya
masomo haya ni kama vile kemia, hisabati, bayolojia, Kiswahili,
kingereza, na masomo mengine mengi mno. Elimu hii hutumika
kuwasaidia wanafunzi kuingia katika taaluma mbalimbali kama
vile udaktari, ualimu, uhandisi na kadhalika. Penina na Dennis
wanakutana pale kwenye chuo kikuu wakiwa wanafunzi wa fasihi.
Wanatafuta elimu hii ili kuwahi kupata ajira bora baadaye. Ni
elimu hii ambayo Dennis anaitumia kutafuta kazi katika shirika la
uchapishaji wa magazeti. Watu wote wanaoendelea na
kufanikiwa kwenye elimu hii huishia kufaulu sana maishani katika
kupata taaluma wanazozipenda wao wenyewe. Wanafunzi wote
katika chuo kikuu wanatia bidii masomoni ili waweze kupata kazi
za aina mbali mbali.
19.
ii) Elimu ya Maisha.
Elimu hii haihisiani na elimu ya vitabu. Haya ni maadaili
anayokuzwa nayo mtu. Ni mkusanyiko wa tabia na itikadi njema
ambazo mja hukabidhiwa katika aushi yake ili kuweza
kutangamana vyema na umma. Dennis alikuzwa vyema na
kufundishwa kuwaheshimu watu. Isitoshe, ni mvulana aliye na
tabia nzuri. Anapoenda chuo kikuu, hajihusishi na tabia
zinazoelekeza kupotoka kwake kwa maadili. Anawaheshimu
wote. Kwa upande mwingine, Penina amelelewa kwa kuwabagua
watu kwa misingi ya pesa uchumi wao. Ni wazi kuwa muda wote
huu, alikuwa ameyacha makucha yake tu.
a) Mapenzi
Mapenzi ni hali ya kumkubali mtu wa jinsia tofauti na kumuenzi
pamoja na kujihusisha naye katika mahaba. Mapenzi
yanayoonekana katika muktadha huu ni ya aina mbili:
i) Mapenzi ya kifaraungo.
Penina ndiye anadhihirisha mapenzi haya. Anampenda
Dennis ingawa kwa masharti. Licha ya wao kuishi pamoja,
anamwambia Dennis ya kwamba hawezi kuolewa na mtu
asiye na pesa. Ni wazi kuwa mapenzi yake hayaamuliwi na
uzuri wa penzi bali kiwango cha pesa alichonacho mtu. Punde
tu penzi lao linapoguzwa na upepo mdogo tu (ukosefu wa
ajira) linanyauka na kupotelea mbali.
20.
ii) Mapenzi ya dhati.
Dennis anampenda Penina kwa keweli. Anaishia kumpenda
na hata kumtambulisha kwa wazazi wao. Ingawa alikuwa
anashuku ukweli wa Penina kumpenda maskini kama yeye,
anajitolea na kumpenda Penina kwa dhati. Anatazamia
kumuoa haswaa pindi atakapopata kazi.
b) Utabaka
Hii ni hali ya jamii kugawika katika makundi tofauti kulingana
na uwezo wa kifedha. Mahusiano yote kati ya wahusika
yanaongozwa na fedha walizo nazo mfukoni. Penina
anaonywa na wazazi wake kujihusisha na Dennis kwani yeye ni
maskini. Ingawa anakataa mawaidha ya wazazi wake hapo
awali, anaishia kumfurusha Dennis kwani anamwona kama
maskini asiyefaa kumwoa.
c) Umaskini
Msimulizi wa hadithi hii (Dennis) ndiye kielelezo cha maskini
wanavyoishi. Alisoma kwa shida kwani karo ilikuwa kero
kubwa. Ni wazi kwamba jamii yake inamtazamia yeye
kuikomboa kutokana na umaskini wao. Ingawa amefaulu kuka
chuoni, chumba chake Dennis ni kitupu kisichokuwa na chochote
cha kutamaniwa. Anapohisi njaa, anagutukuka kuwa hana
chochote cha kupika. Anaamua kupika uji. Baadaye
anagundua kwamba hata sukari ya kutia kwene uji wake
mweupe hana. Anaishia kunywa uji hiyo bure kwa kujihurumia.
21.
Ingawa Dennis anafaulu kumpata mpenzi anayempenda,
anajitegemeza kwake kwa kiasi kikubwa. Wanaishi pamoja
lakini ni wazaziwe Penina wanaowakimu mahitaji yao yote sio
Denniskwani yeye ni maskini. Baadaye, Penina anapochoshwa
na Dennis anamfurusha. Ni ajabu kuwa Dennis anabeba kila
kilicho chake kwenye begi moja tu! Anatembea akijutia masomo
yaake ambayo hadi sasa hayajamsaidia kustawisha misuli yake
ya kiuchumi. Anashangaa jinsi ataweza kuwaokoa wazazi wake
na umaskini uliowagubika.
a) Ukosefu wa Ajira
Ajira ni adimu katika nchi anayoishi Dennis. Ametembea katika
makampuni mengi na mashirika mengi akipeleka nyaraka za
kuomba kazi. Amebisha huku na kule akiwacha tawasifu yake
na ya Penina lakini tangu kumaliza masomo ya chuo kikuu,
miaka mitatu baadaye hajafaulu kupata kazi. Dennis anaishia
kufurushwa na mpenziwe kwani hana uwezo wa kukimu mahitaji
yao ya kifedha.
a) Majuto
Dennis anachorwa kama mhusika anayejutia maisha yake.
Anajutia umaskini wake kwani Penina anamfurusha kwa
kisingizio kuwa yeye hawezi kutoa hela zozote za chakula na
matumizi ya pale nyumbani. Anajutia kisomo chake kwani
anatumaini kuwa kitampa ajira lakini ng’o! Anajuta
akiwakumbuka wazazi wake na kukiri jinsi ambavyo anaweza
kuwasaidia ili kuwaondoa katika umaskini. Anajutia bidii yao ya
kumsomesha kwani sasa hivi hawafai wazazi inavyostahili.
22.
Anajutia fumbo ya maisha kuwa kinyume naye katika kila
jambo analofanya. Anajutia kuonewa na maisha.
MBINU ZA LUGHA NA UANDISHI.
a) Tashihisi
i) Ninafuta chozi linalochungulia machoni. (Uk 13)
ii) Njaa inanitafuna kama mbwa anvyoguguna mfupa. (Uk 17)
iii) Mapenzi hukua, huugua yapatapo maradhi na hufa
hatimaye. (Uk 20)
iv) Mapenzi yasiyujua kufa. (Uk 20)
v) …bado bahati yangu haijasimama. (Uk 22)
b) Tashbihi
i) …kumuibia bingwa katika mtihani wa kitaifa ni kama
kutajaria kuyapata maziwa kutoka kwa kuku. (Uk 13)
ii) …sasa anaanza kututamkia maneno machungu kama
shubiri. (Uk 14)
iii) Mapenzi ni matamu kama uki…(Uk 26)
iv) Njaa inanitafuna kama mbwa anvyoguguna mfupa. (Uk 17)
v) Almuradi maskini na matajiri wametengana kama ardhi na
mbingu. (Uk 17)
vi) Mwili mzima unaanza kutetemeka kama ndama
aliyenyeshewa…(Uk 17)
vii) Waamatunaapendana kama ulimi na mate. (Uk 21)
viii) Wanafanana kama riale kwa ya pili. (Uk 23)
ix) Ninahangaika kama kondoo aliyevamiwa… (Uk 25)
23.
a) Kuchanganya ndimi
i) Wanabeba vipakatalishi na Ipad zao mikononi, sa kabisa!
ii) Hatimaye nimeka kwenye ghorofa ya tatu katika jumba
la makazi ya Mastura Hall. (Uk 16)
iii) Mimi na Penina tunaishi katika mtaa wa New Zealand. (Uk
22)
iv) …basi ni wazi kuwa your competence is doubtful. (Uk 25)
v) Unajua tangu nianze tarmacking sijawa nikitazama
runinga. (Uk 26
b) Nidaa
i) Wanabeba vipakatalishi na Ipad zao mikononi, sa
kabisa! (Uk 13)
ii) Laiti mama yangu angeliweza kunisomesha hadi shule ya
kitaifa! (Uk 13)
iii) La hasha! (Uk 14)
iv) Looh! Kwani swali langu vipi? (Uk 15)
v) Lo! Nitakula nini? (uk 17) Lo! Mlangoni yuko msichana
mmoja mrembo. (Uk 18)
vii) Ah! Pengo gani ilhali una mapenzi ya kweli…? (Uk 19)
a) Misemo na nahau.
i) Nikatupa macho huku na kule. (Uk 12)
ii) Analaza damu usiku na mchana. (Uk 14)
iii) Licha ya uchechefu wa pesa, nimejikaza kisabuni. (Uk 21)
iv) Mama na baba wanakula mwata. (Uk 28)
v) Lakini sitakata tamaa. (Uk 28)
24.
a) Uzungumzi nafsia.
Mbinu hii imetawala kote kwenye hadithi kwani haya ni
masimulizi katika nafsi ya kwanza. Mifano michache ya mbinu hii
ni kama:
i) “Kwa nini ninalia sasa?” (Uk 13)
b) Kinaya
i) Unajua watu waliosoma sana kama Daktari Mabonga hawajui
lolote wala chochote. (Uk 14)
ii) Utajifundishaje kula na chakula hukitafuti? (Uk 15)
iii) Masomo ya chuo kikuu si masomo, ni madubwana
yasiyojulikana yalikotoka.(Uk 15)
iv) Ninahangaika kama kondoo aliyevamiwa na jeshi la usubi.
Sina majibu. (Uk 25)
c) Maswali ya Balagha.
i) Itakuwaje wewe ufundishwe kujinadhishia kesho yako? (Uk 15)
ii) Utajifundishaje kula na chakula hukitafuti? (Uk 15)
iii) Lo! Nitakula nini? (uk 17)
iv) Nifunge mlango au nifungue? (Uk 17)
v) Mbona asiketi kitini?…kwani ni lipi alilojia humu? (Uk 18)
vi) Kabwela kama mimi nina faida gani? (Uk 23)
a) Chuku.
i) Darasa zima linangua kicheko. Msichana mmoja amecheka
hadi ameanguka. (Uk 15)
ii) Mtazamo wake unaweza kumwamsha mbwa aliyelala. (Uk 18)
iii) Ukimtazama machoni, machozi ya furaha hayaachi
kukutonatona. (Uk 18)
iv) …kitambo kirefu kilichatawaliwa na kimya- kimya cha
kuanguka pamba uusikie mlio wake. (Uk 18)
v) Wasikilizaji wako watacheka mpaka midomo ianguke. (Uk 22)
vi) Akanyagapo chini ardhi inatetemeka. (Uk 22)
25.
a) Methali.
i) Mzungu wa kula haufunzwi mwana. (Uk 15)
ii) Ujapokosa la mama, hata la mbwa huamwa. (Uk17)
iii) Mzoea vya sahani, vya vigae haviwezi. (Uk 20)
iv) Mume ni mume hata akiwa gume gume. (Uk 21)m
v) Mgomba changaraweni, haupandwi ukamea. (Uk 27)
WAHUSIKA NA UHUSIKA.
1. Dennis (Msimulizi)
Huyu ni mvulana aliyesoma kwa bidii licha ya umaskini wake na
kuka chuo kikuu, ni mpenziwe Penina. Ana sifa zifuatazo:
a) Mwenye bidii.
Licha ya umaskini uliopo pale nyumbani, anatia bidii
masomoni. Anasoma na kufanya vyema kuanzia shule ya
msingi, shule ya upili hadi chuo kikuu. Pia ana bidii ya
kutafuta kazi ili aweze kuwasaidia wazazi wake na pia
kumwoa mpenzi wake Penina.
b) Mwenye mapenzi.
Anampenda Penina kwa dhati. Anamuenzi na kutaraji kuwa
siku moja atamwoa Penina. Anamwonyesha kwa wazazi
wake ambao wanafurahia sana kumwona mwanao akiwa na
mpenzi akama Penina.
26.
a) Mwenye matumaini.
Ana matumaini ya kupata kazi ndiposa anatia bidii
masomoni. Anaahidi kumwoa Penina endapo angepata kazi
ambayo ingemwezesha kukimu mahitaji yao. Ana matumaini
kwamba ingawa hana kazi sasa hivi siku moja bahati
itamfungulia milango na mambo kumwendea vyema
akapata kazi nzuri.
b) Ni mwoga.
Anapopewa fursa ya kuzungumza katika udodosi wa kazi
katika shirika la uchapishaji wa magazeti, anaogopa
kufungua kinywa chake. Kijacho chembamba kinamtiririka
huku akitetema na kukosa maneno. Anafurushwa kutoka
chumba kile bila kutamka chochote.
a) Mwenye majuto.
Licha ya yeye kutia bidii maishani na masomoni, anajuta
kwamba bahati inakataa kumfungulia milango ya heri. Anajuta
kutokuwa na kazi kwani anafurushwa kutoka chumbani na
mpenziwe. Pia anajutia kutowasaidia wazazi wake baada ya
wao kumsomesha kwa shida mno. Anajuta kumwamini Penina na
kukubali mapenzi yake ya kifaraungo.
27.
1. Penina
Huyu ni mpenzi wa msimulizi ambaye walikutana kule chuo kikuu
wakisoma katika darasa moja. Anampenda msimulizi na kuahidi
kuoana naye watakapokuwa matajiri.
a) Ni mzembe.
Anaketi chumbani mchana kutwa bila kufanya kazi yoyote
ile.Kazi ni kutazama televisheni tu. Tawasifu zake zinapelekwa
maosini na Dennis. Hana bidii ya kutafuta kazi. Anaamini
kuwa Dennis ndiye anafaa kutafuta hela.
b) Mwenye unaki.
Licha ya yeye kudai kumpenda msimulizi, ni wazi kuwa penzi
lake ni la kifaraungo. Upendo wake unaongozwa na tamaa ya
pesa na utajiri. Anajifanya kumpenda Dennis lakini ukweli ni
kwamba alitazamia ya kwamba Dennia angepata kazi ili
waweze kuoana.
a) Mwenye tamaa.
Tamaa yake ya pesa inadhihirika wakati ambapo utulivu wake
unakia kikomo. Anamfurusha Dennis kwa umaskini wake.
Anadai kuwa hawezi kuolewa naye kwani Dennis hana pesa.
Anaweza tu kuolewa na mtu mwenye pesa.
28.
b) Mwenye mawazo ganda.
Penina anaamini kuwa ni mwanaume tu ambaye anapaswa
kutafuta hela. In
gawa wote wawili wameelimika, Penina hana bidii ya
kutafuta kazi. Anamwac hia jukum u hilo Dennis
anayezunguka katika maosi mengi bila mafanikio.
1. Daktari Mabonga.
Ni mwalimu wa fasihi katika chuo kikuu cha Mavuko. Ni wazi
kuwa yeye ni mwalimu asiyependa kudadisiwa kwa
vyovyote vile. Ni chanzo cha namna ambavyo mafunzo
yanatendeka katika vyuo vikuu.
a) Mwenye hekima
Anatema maneno yaliyojawa na hekima na maarifa
anapozungumza na wanafunzi wake. Anawapa maarifa
kuhusu maisha ambayo yanawasubiri baada ya masomo
yao. Anawanoa wanafunzi wake vilivyo.
b) Mwenye kiburi/mabezo.
Licha ya yeye kufundisha vizuri wanafunzi wake
hawamwelewi. Anatumia lugha ngumu inayowashangaza
wanafunzi. Wanafunzi wake wanapomtaka atumie lugha
nyepesi ili waweze kuelewa, anawajibu kwa kiburi na
mabezo.
c) Mwenye mapuuza.
Anapuuza maswali anayoulizwa na wanafunzi wake na
kuyaona ya kitoto. Anatupilia mbali maswali yote
yanayoibuliwa na wanafunzi wake wa fasihi.
29.
1. Shakila
Huyu ni msichana ambaye walisoma pamoja na Dennis kwenye
chuo kikuu. Mamake ni mkurugenzi mkuu katika shirika la
uchapishaji wa magazeti. Ametumiwa na mwandishi kuendeleza
maudhui ya ubaguzi.
a) Mwenye dharau.
Anapomkuta Dennis osini akisubiri kufanyiwa udodosi,
anazungumza naye kidogo na kisha kutoa cheko kubwa
lenye dharau linalomkera Dennis. Hii ni ishara tosha kwa
Dennis kwamba hatapata kazi yoyote pale.
b) Mwenye unaki.
Anapomkuta Dennis osini, anamsalimu na kumzungumzia
vyema. Ajabu ni kwamba anapoingia oni kwa mhazili,
anatoa cheko kubwa pamoja na mamake. Anamcheka
Dennis bila shaka.
2. Mamake Shakila.
Mhusika huyu ametumiwa na mwandishi kama kielelezo cha watu
wenye mitazamo hasi kwa wenzao, wenye mabezo na
kujishaua. Ingawa ni mkurugenzi hana utu wa ukurugenzi. Sifa
zake ni panmoja na:
30.
3. SHOGAKE DADA ANA NDEVU
Historia ya Mwandishi.
Mwandishi ni mojawapo ya waandishi chipukizi wenye uwezo wa
kipekee wa kubuni kazi za fasihi. Ni mwalimu aliyewahi kuandika
Makala mbalimbali ya Kiswahili. Isitoshe ana tajriba ya muda
mrefu wa kufundisha Kiswahili katika shule mbali mbali.
Dhamira
Mwandishi wa hadithi hii amedhamiria kuwaonya vijana dhidi ya
kujihusisha na mapenzi ya kiholela. Anawatahadharisha vijana
kuhusu hatari za kushiriki mapenzi ovyo ovyo. Hatari hizi ni mimba
za mapema pamoja na kukumbana na mauti wakati wa kuavya
mimba.
Ufupisho wa Hadithi
Hadithi hii inawasawiri wazazi wawili ambao wamejukumika
kuwalea wanao vyema. Bwana Masudi na Bi. Hamida
wamejukumika vilivyo na kumlea binti na mwana wao kwa
uangalifu mkubwa. Wamemfunza dini na tabia njema.
Wanamlinganisha binti yao na wasichana wengine pale kijijini na
kuwona bora zaidi kuwaliko. Jina la msichana huyo ni Saa.
Saa anawaomba wazazi wake ruhusa ya kumleta shogake
anayeitwa Kimwana ili waweze kusoma kwa pamoja. Wazazi wake
Saa hawana pingamizi kwa ombi hilo kwani wanamtakia binti yao
fanaka katika masomo yake na ikiwa kuna shogake ambaye
wanaweza kufaana katika kudurusu, basi hawaoni tatizo lolote.
Kimwana anakuja siku baada ya nyingine na kudurusu pamoja na
Saa kwenye chumba chake Saa. Kila anapokuja, mama mtu
anawaruhusu kujifungia chumbani ili nduguye Saa asiwasumbue
wakiwa katika shughuli za kudurusu.
Ajabu inayokuwepo ni kuwa wazazi wa Saa hawajawahi kumsikia
huyo shogake Saa akizungumza. Ni “Marahaba” tu ndiyo
inamtoka kila anapokuja kusoma pamoja na Saa na kisha
wanaandamana na kujifungia kwenye chumba cha Saa ili
kuendeleza masomo yao. Hakuna anayewasumbua, iwe ni mama,
baba au ndugu, kwani wanahitaji muda wao wa kutosha ili kusoma
ipasavyo! Wazazi hawamwoni Kimwana kuwa na ila yoyote ile.
31
Baada ya miezi sita hivi, tatizo linaingia. Mama saa anaanza
kuona mabadiliko katika mwili wa bintiye. Habaini ikiwa ni mawazo
yake tu ama ni kweli kwamba mambo yalikuwa yakitendeka.
Anapomdadisi bintiye, Saa anakana kuwepo kwa jambo lolote lile
lenye utofauti katika mwili wake. Ila mamake anatambua ya
kwamba kuna jambo. Lakini ushahidi atautoa wapi vile? Hajui.
Anatulia tuli ila moyoni anasalia na done chungu la tuhuma kwa
bintiye. Anapomuuliza babake Saa, mume anamzomea na
kumhujumu kwa kumtuhumu bintiye.
Siku ya siri kujulikana inapowadia, wanakuwa wameketi baba,
mama na ndugu mdogo wa Saa. Ndugu anamweleza mamake jinsi
ambavyo yeye na rakiye walikuwa wakicheza. Walicheza mchezo
wa kujicha. Ila alipatikana kila mahala alipojaribu kujicha.
Ndipo Lulua akaamua kujaribu kujicha katika chumba cha
dadake. Akafungua mlango na kuona aliyoyaona. Aliwapata Saa
na shogake wamelala kitandani. Walikuwa wamelala lakini huyo
shogake ambaye muda wote huvalia buibui na kudhaniwa ni
mwanamke, alikuwa na ndevu. Mama anagutuka na kudhihirisha
tuhuma zake za siku nyingi.
Kwa sadfa wakati huo, simu inalia. Baba Saa anapojibu, huyo
anayempigia simu anampa habari zinazomkata maini. Saa
amekuwa maiti. Saa anakuwa kaaga baada ya kujaribu kuavya
mimba. Sasa inabainika wazi kwamba yule Kimwana
anayeruhusiwa na wazazi wa Saa kuja kusomea hapo nyumbani
pamoja na Saa hakuwa mwanamke, bali mwanamume
anayejihusisha kimapenzi na Saa, mapenzi ya siri yanayoishia
kumsha saa.
32.
MAUDHUI
Maundhui mengi yameangaziwa katika hadithi yakiwemo:
a) Unaki
Saa ni msichana anayeaminika kwa wazazi wake. Wazazi
wake wanajiamini wakijua kwamba binti yao ameshika
maadili mema ya jamii. Isitoshe, anakuwa kajiweka na
kuwekeka vyema. Anakuwa msichana mwenye tabia na
heshima zake. Saa anapowaomba ruhusa ya kumleta raki
yake pale nyumbani kwa madhumuni ya masomo, hakuna
anayeshuku. Ajabu ni kwamba Saa anawadanganya
wazazi wake. Yule anayedhaniwa kuwa msichana alikuwa
mwanamume mwenye ndevu ambaye wanalala pamoja kule
chumbani muda wote ule wanaodhaniwa wanasoma.
Matokeo ya siri hiyo ni mimba ya mapema inayoishia
kumkatizia saa masomo yake na pia kumletea mauti. Huu ni
unaki wa hali ya juu.
b) Majuto
Wazazi wa Saa wanajuta kumruhusu binti yao kumleta
mgeni nyumbani kwao kwa madhumuni ya kusoma, jambo
ambalo halikutendeka hivyo. Badala ya kusoma, Saa
anajihusisha kimapenzi na Kimwana na kwenda kinyume na
maadili aliyofunzwa na wazazi wake.
Ni wazi kwamba Saa pia anajutia vitendo vyake.
Anapozungumza na mamake, anaonekana kuwa mwingi wa
haya kwa kujutia vitendo vyake. Ni fedheha hiyo
inayomwelekeza kutaka kuavya mimba, jambo ambalo
linamwangamiza.
33.
c) Malezi
Bwana Masudi na Bi. Hamida wamejukumika kumlea binti na
mwana wao kwa uangalifu mkubwa. Wanamkuza Saa na
kumpanda katika maadili. Wanamfundisha akujiwelka vizuri kama
mtto wa kike. Wanampa ushauri mwema utakaomfaa maishani.
Isitoshe elimu ni jambo lenye umuhimu mkubwa kwao.
Wanahakikisha kuwa wamemwelimisha binti yao. Ni furaha na
shauku ya wazazi hawa kushuhudia saa akipaa na kuendelea
masomoni. Wanapomwona akiwa na raki anayeweza kumsaidia
kuimarika masomoni, wanampa nafasi yao kusoma kwa makini bila
kusumbuliwa hata kidogo. Wanamruhusu Saa kujifungia
chumbani na rakiye ili waweze kusoma kwa pamoja. Haya ni
malezi mema kwa watoto hawa.
a) Mapuuza
Wazazi wake Saa wana mapuuza. Wanapoambiwa ya
kwamba Saa na Kimwana wanasoma huko chumbani
walikojifungia, wanaamini tu. Hakuna yeyote anayeshuku
ikiwa ni uwongo. Hata hawashangai ni kwa nini shoga huyu
Kimwana hapendi kuketi sebuleni au hata kuzungumza nao.
Wazazi hawa wanafungia macho uwezekano wa Kimwana
kuwa samba anayevamia zizi la kondoo.
Kando na hapo, hakuna aliyewahi kujaribu kudhibitisha
ukweli wa vijana hawa wawili kusomea chumbani. Wazazi
h a wa wa n a p o a m b i wa n i m a s o m o ya n ayo k u wa
yakiendelea, hawatilii shaka ukweli huo bali wanaamini
moja kwa moja. Haya ni mapuuza ya hali ya juu. Mapuuza
ya wazazi hawa yanaishia kumuangamiza Saa kwani
anaaga baada ya kujaribu kuavya mimba.
34.
b) Mapenzi
Kuna aina mbili za mapenzi yaliyoangaziwa karika hadithi hii:
i) Mapenzi ya dhati.
ii) Mapenzi ya uwongo.i)
Mapenzi ya dhati.
Haya ni mapenzi ya kweli kati ya wahusika. Mapenzi haya
yanaweza kuwa kati ya ndugu wawili au kati ya mzazi na
mwanawe au kati ya wahusika wawili wenye jinsia tofauti. Bwana
Masudi na Bi. Hamida wanampenda binti yao. Upendo huu
unadhihirika kwa namna ambavyo wanamlea kwa makini.
Wanahakikisha kwamba binti huyu amekuzwa kwa maadili mema,
amefundishwa kujiweka sawasawa. Akilinganishwa na wasichana
wengine pale mataani, hakuna msichana wa kifuu chake. Huu ni
upendo wa kweli. Isitoshe, wazazi hawa wanadhamini masomo ya
binti huyu na kumpa msaada wotote kadri ya uwezo wao.
Wanamtakia Saa mema maishani.
Bwana Masudi na Bi. Hamida wanapendana kwa dhati. Hawa ni
wazazi wawili wenye mapenzi ya dhati kati yao. Wanazungumza
mambo mazito na ya ndani kila jioni wakisubiri usingizi uwachukue.
Wao huzungumza mambo yote yaliyopo ndani ya nafsi zao. Haya
ni mapenzi ya dhati.
35.
ii) Mapenzi ya uwongo.
Mapenzi haya ni yale ambayo huibuka tu kwa mshawasho wa
ujana na tamaa za mwili. Mapenzi haya yamejitokeza katika
uhusiano uliopo kati ya Saa na Kimwana. Matokeo yake ni
mimba haram u ambayo inamtia Saa mashakani.
Wanapojaribu kuitoa wanamletea Saa mauti. Waama,
mapenzi haya huwaletea wahusika majuto.
a) Elimu.
Elimu ya vitabu ni muhimu kwa maisha ya baadaye. Saa
anahimizwa kutia bidii masomoni ili aweze kupata nafasi katika
shule ya upili. Wazazi wake Saa, Bwana Masudi na Bi.Hamida
wanamsaidia binti yao kwa lolote atakalo mradi tu apite
mtihani huo wa shule ya upili. Katika kumsaidia Saa kupita
mtihani, wanamruhusu kumwalika rakiye ambaye anamsaidia
katika masomo yake. Wanasaidiana ili wote wawahi kupita
mitihani yao na kuelekea katika shule za upili.
MBINU ZA LUGHA NA UANDISHI.
a) Majazi
i) Bwana Masudiii)
Kimwana- Hili ni jina ambalo linapendekeza jinsia ya mtu
huyu anayedhaniwa kuwa mwanamke. Yeye ni Mwana
(MVULANA) bali sio msichana.
iii) Saa- jina hili linapendekeza kuwa mhusika huyu ni sa wa
tabia. Ni kweli kwamba yeye ni sa lakini mwisho tu ndio anatia
doa hulka yake.
iv) Lulua- hiki ni kitu cha thamani mno. Mwana huyu anapendwa
mno na wazazi wake.
36.
b) Tashihisi
i) …wanapokuwa kitandani wakingojea usingizi mtamu
uwachukue.. (Uk 29)
c) Maswali ya balagha
i) Wangapi wanaozaa watoto wazuri kama au kuliko Saa
wetu. Na watoto hao hutokezea kuwa na balaa tupu? (Uk 29)
ii) Ya nini ushungi huo? (Uk 31)
iii) Si hubaki humo mpaka wamalize kusoma na kujadiliana? (Uk
32)
iv) Itakuwaje waamini kila kitu anachesema Saa? (Uk 32)
v) Kweli? Uongo? Kweli au uongo yale maneno ya binti yake?
a) Nidaa
i) …lakini matendo yake afadhali ya mbwa, tena mbwa koko!
(Uk 29)
ii) Saa mama, umo ndani mwenu ‘vyo! (Uk 31)
b) Methali
i) Lisemwali lipo, kama halipo linakuja. (Uk 30)
ii) Siri ya kata iulize mtungi. (Uk 30)
iii) Kidole kimoja hakivunji chawa. (Uk 31)
c) Tanakuzi
i) Saa halindwi, hujilinda yeye mwenyewe. (Uk 31)
d) Taharuki
i) Ni kwa nini Kimwana alijifunika buibui?
ii) Ni kwa nini Kimwana hakuzungumza mambo yoyote?
iii) Mbona Kimwana na Saa walijifungia mle ndani kwenye
chumba? (Uk 32)
37.
e) Mdokezo
i) Tena haishi kutapikatapika… (Uk 33)
ii) Pamoja na kujilinda kwangu… (Uk 33)
iii) Kumbe mlango haukufungwa… (Uk 34)
iv) Ameshakufa…ameshakufa… (Uk 35)
f) Kinaya
g) Mfano mzuri mpaka leo ni kwamba wao wazazi hawajapata
hata neno lake, ila “Shikamoo” inayotoka midomoni nyuma ya
buibui kama kata ya maji mtungini. Ni ajabu kuwa wazazi wa
Saa hawajui ni nani anahusiana na binti yao.
a) Misemo na nahau
i) Kwa hivyo watakuwa wanaongozana na kuzibana nyufa…(Uk
31)
b) Tashibihi.
i) …ila “Shikamoo” inayotoka midomoni nyuma ya buibui kama
kata ya maji mtungini.
c) Takriri.
i) Juzi…juzi… (Uk 34)
ii) shogake…shogake…(Uk 35)
iii) Ameshakufa…ameshakufa…(Uk 35)
WAHUSIKA NA UHUSIKA.
1. Saa
Huyu ni msichana mdogo aliye katika shule ya msingi. Ni bintiye
Bwana Masudi na Bi.Hamida. Anatarajia kujiunga na shule ya upili
hivi karibuni ikiwa atapita mtihani wake wa shule ya msingi. Sifa
zake ni pamoja na:
38.
a) Ni msiri
Anafaulu kumcha raki yake wa kiume na kumvisha buibui
ili kuwapumbaza wazazi wake kumdhania kimwana kuwa
mwanamke. Wanaendelea na mchezo wao kwa siku nyingi
hadi Saa anaishia kupata mimba. Isitoshe, anacha mimba
yenye na kuikana mamake anapomdadisi ikiwa kuna jambo
lolote mbaya limemtendekea. Anacha mimba yake na
kujaribu kuiavya. Hapo tu ndipo wanazi wanabaini
yaliyokuwa yakiendelea kwa muda wote huu.
b) Mwenye Unaki
Anawadanganya wazazi wake kwamba anasoma pamoja
na rakiye wa kike ilhali Kimwana ni mvulana.
Wanadanganya kwamba wanasoma ilhali ni mapenzi
yanaendelea kule chumbani mwa Saa. Huu ni unaki wa
hali ya juu.
a) Msaliti
Saa anasaliti uaminifu ambao wazazi wake walikuwa nao
kwake. Wanamwamini wakijua yeye anasoma ilhali wakati
huo, yuko kwenye mahaba ya Kimwana.
b) Ni mwenye bidii.
Anapokuwa nyumbani yeye hufagia, hupika, huosha
vyombo, hufua, hupiga pasi na kutandika kila siku.
c) Mwerevu.
Katika kila mtihani, Saa aliibuka wa kwanza kabisa katika
darasa. (Uk 30)
39.
1. Kimwana
a) Mwongo
Anajifunika buibui na kujifanya kama mtu wa jinsia ya kike.
Kwa uwongo huu, anafaulu kuingia nyumbani kwa Saa na
kuandamana naye hadi chumbani mwake wanakodhaniwa
wanaendelea masomo.
b) Mwenye unaki
Katika mawazo ya wazazi wa Saa, Kimwana ni msichana
ambaye ni raki ya Saa. Wanadhaniwa kusaidiana katika
kudurusu kazi ya shuleni. Ajabu ni kwamba Kimwana ni simba
anyemnyemelea kondoo na kumla mzima mzima akiwa zizini.
2. Bwana Masudi
a) Mwenye mapenzi.
Anampenda mkewe na watoto wake. Ni baba mwenye
upendo.
b) Mwenye Bidii.
Anajibidiisha kuhakikisha kuwa jamii yake inaishi vyema.
Isitoshe anajibidiisha kumuelimisha Saa.
a) Mwenye mapuuza.
Anapoelezewa kuhusu mabadiliko yanayotokea kwa
bintiye, anakana na kuyatupilia mbali.
40.
1. Bi. Hamida
a) Mwenye mapenzi.
Anampenda mumewe kiasi cha kumfungulia moyo wake
wote. Isitoshe anawaenzi watoto wake na kuwapenda
mno. Anamtakia Saa mema na hivyo kumfunza maadili
mema.
b) Mdadisi.
Umakini wake unamfanya kugundua kuwa kuna jambo
baya na bintiye. Anagundua kuwa bintiye ana tatizo na
umbo lake limeanza kubadilika kwa kiwango fulani.
Udadisi wake ndio unamuelekeza kugutukia hali mpya
ya bintiye.
1. Lulua
a) Ni mkweli.
Anapoulizwa maswali kuhusu dadake, anasema ukweli wote
bila kucha chochote, jambo linalowapa mwangaza wazazi
wake kuhusu tabia za dadake saa.
4. SHIBE ITATUMALIZA
Historia ya Mwandishi.
Mwandishi ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Tanzania. Ni msomi na
mwalimu wa Kiswahili. Amechangia pakubwa katika Isimu na
lugha.
Dhamira
Mwandishi amedhamiria kuwaonya hasaa mataifa ya Afrika
kuhusu tabia za ula na uroho.
41.
Ufupisho wa Hadithi
Sasa na Mbura ni watoto wa mwanasiasa, Mzee Mambo. Mzee
Mambo anawaandaa wanawe kuingia katika harakati za
unyonyaji wa mali ya umma katika nchi husika. Anawataka wanawe
pia waingie katika siasa na wizi wa mali ya umma.
Baada ya uteuzi, sherehe zinaandaliwa za kufana ili kusherehekea
ufanisi wa wanasiasa. Sherehe zinaandaliwa na matangazo yake
kupeperushwa kwenye runinga. Watu wote nchini wanashuhudia
jinsi ambapo wanasiasa wanasherehekea. Magari ya kifahari
yanatumiwa na wanasiasa ili kujishaua na kuonyesha fahari ya
wanasiasa.
Kisadfa, wakati huo huo wa sherehe, wanasiasa wakiwa kwenye
sherehe wakila, wananchi hawana chakula. Wananchi hawana
dawa hospitalini. Pia kuna uhaba wa chakula. Wanasiasa
wanafurahia shibe, ilhali wananchi wanateseka na kuumia kwa
kukosa mahitaji ya kimsingi. Wanasiasa wanapeana makandarasi
kwa kujuana
.
Katika sherehe, inadhihirika kuwa Dj alipewa kandarasi kuuza
dawa ambazo zilistahili kuwasaidia wananchi. Dawa ambazo
zilistahili kupewa wananchi zinafujwa na kupewa Dj ili aziuze.
MAUDHUI
a) Uongozi mbaya
Uongozi mbaya unapelekea wananc hi kukosa huduma
wanazostahili. Umma hauna dawa kwani viongozi wamejinyakulia
madawa ambayo yanapaswa kuwa kwenye hospitali za umma na
kisha kuwapa watu binafsi wanaojifaidi kama vile Dj (Uk 43).
42.
a) Ubinafsi na tamaa.
Dj ananyakua dawa za wagonjwa na kuziweka kwenye duka lake
mwenyewe, kuuza na kujifaidi huku mamia ya watu wengine
wakiumia kwa kukosa dawa hizo.
b) Usadi
Sasa na Mbura ni watoto wa mwanasiasa, Mzee Mambo, na
hawakustahili kupewa kazi yoyote kwenye serikali. Ajabu ni
kwamba wanapewa nyadhifa ili kusimamia Mipango na
Mipangilio. Nyadhifa hizi haziwafai hata kidogo kwani hakuna
kazi yoyote wanayotekeleza. Isitoshe, Dj na wenzake wanavuna
mabilioni ya pesa kwenye sherehe kwa njia za udanganyifu.
MBINU ZA LUGHA NA UANDISHI.
a) Mdokezo
i)…hata yeye mwenyewe hujikuta kimya kimya huku akisema
nafsini mwake…(Uk 36)
ii) Kwenye kioo cha taifa, fesibuku, gazeti la… (Uk 45)
b) Methali
i) Wajinga Ndio waliwao. (Uk 37)
c) Utohozi – haya ni maneno yaliyoswahilishwa.
i) Fesibuku (Uk 38)
ii) Wasapu (Uk 38)
iii) TV (Uk 38)
iv) Monokotilidoni (Uk 43)
v) Kwenye kioo cha taifa, fesibuku, gazeti la… (Uk
45)
vi) …mabomu, presha, obesity, sukari, …(Uk 44)
d) Tashibihi
i) …matumbo yao matupu yalishindana kunguruma kama
radi. (Uk 39)
43.
e) Misemo na nahau
I) Magari yanapina vikumbo kuingia na kutoka kwa Mzee
mambo. (Uk 38)
a) Tashihisi
i) Jingine linamimina jamaa na mzee Mambo shereheni. (Uk
39)
ii) Njaa inawatafuna. (Uk 39)
iii) Upepo unawapuliza na kuwabembeleza… (Uk 41)
iv) Swali nalo linagoma kupuuzwa namna hii. (Uk 41)
b) Tanakuzi
i) Vyakula vyeupe. Vya rangi. Vitamu. Vikali. Vichachu.
Baridi. Haya tu. (Uk 39)
c) Matumizi ya mashairi
i) Shairi 1- Uk 43- Shairi hili ni la kuwagutusha wanasiasa
wanaolala. Ni shairi linalokusudia kuwazindua wanasiasa na
kuwagutua wawe watu wa kujukumika.
d) Matumizi ya nyimbo
i) wimbo wa kwanza-Uk 37. Wimbo huu unatumika
kuwaponza wahusika Sasa na Mbura ili kuwagutusha na
kwamba Mola aliyewapa wao mali anaweza pia akawapa
wengine.
Wimbo wa pili- Uk 43. Wimbo huu ni jibu kwa ule wimbo wa
kwanza. Viongozi dhalimu wanawajibu wananc hi
wakiwaambia wananchi kwamba hawajali wala kubali
lawama zozote zile wanazopewa.
a) Takriri
I) Kunywa na kunywa na kunywa tena.
ii) Huiga kwa jamii. Huiga…huiga. (Uk 40)
44.
WAHUSIKA NA UHUSIKA.
Wahusika wakuu katika hadithi hii ni wawili: Sasa na Mbura. Sifa
zao zinafanana. Sifa hizi ni pamoja na:
a) Ni wala.
Wanapohudhuria sherehe, kazi yao ni kula na kula tu bila
kujalli. Wanatunga foleni mara tatu tatu na kujaza vyakula
kwenye masahani yao hadi pomoni. Wanakula na kumaliza
vyakula vyote vilivyojaa kwenye masahani yao hadi pomoni
.
b) Ni sadi.
Wamepokea kazi katika asi za serikali. Wanapewa
nyadhifa za mipango na mipangilio kama wakuu lakini
wanaishia kutofanya lolote. Kazi zenyewe hawakuzipata
kwa njia halali. Ulikuwa ni usadi uliowaingiza katika osi
hizo.
c) Ni wazembe.
Baada ya kula sahani tatu tatu za vyakula kwenye sherehe,
wanalala usingizi mzito badala ya kwenda kazini.
5. MAME BAKARI
Mohammed Khelaf Ghassany ni mzaliwa wa Zanzibar ambaye ni
mshauri na mwandishi wa hadithi fupi. Kwa sasa ni mwanahabari
katika idhaa ya Kiswahili ya Redio Welle Ujerumani.Sena ni
mwanafunzi,alibakwa akitoka masomo ya ziada.Kitendo hiki
kinamsababishia uchungu moyoni,ukiwa na unyonge.Mara
anaamua kubadilisha mtazamo wake kuhusu maisha .Anaamua
kukabiliana na dunia,anaamua kutolia tena wala kujilaumu
tena.Lazima maisha yaendelee .Anaamua kutoavya mimba
,kutojiua na hata kutokimbia pao.Ujasiri huu unamwelekeza
kumfunulia moyo wake rakiye Sarina.Sarina anaahidi kumsaidia
kubeba mzigo ule.Waliamua kuucha ujauzito chini ya
Jilbabu(vazi pana linalifunika mwili ili kuweka heshima).Waliamua
pia kuwa sehemu ya kujifungulia kuwa shamba kwa wazazi wake
Sarina.
45.
Beluwa dadake Sarina alimhudumia Sara nyumbani ili kucha
siri.Hatimaye anawaeleza wazazi wa Sara yaliyompata
Sara.Wanapokutana pale hospitalini Sara anashtuka kwani
hakutarajia kuwapata wazazi wake pale na zaidi ya
hayo,alishtushwa na utu wa mapenzi waliyodhihirisha wazazi
wake.Mimba ya Sara inaishia kuwa jambo la kawaida kwenye
nyumba yao na mipango yote ya awali ikawa haina maana tena.
Sara anajifungua mtoto wa kike ambaye alikuwa Mke wa babake
mpya.Sara bado ana nia ya kulipiza kisasi kwa huyu mbakaji.Akiwa
kwao anasikia ghasia na fujo huko nje.Ina sadfu kuwa fujo hiyo
ilihusiana na Yule mbakaji.Alikuwa amelala huku anataka kutapia
roho yake iliyokaribia kumtoka kutokana na kichapo alichokuwa
amepata.Anapigwa kwa mvua ya matufali hadi anafariki.
DHAMIRA
a) Mwandishi anakusudia kukashifu tabia ya wazazi ya
kuwadidimiza wanao na kutowaelewa.Inafanya watoto
waogope sana wazazi wao na wanashindwa kuwaambia
wanayopitia.
b) Mwandishi alidhamiria kuonyesha umuhimu wa kuwajibika
kazini.fano: Alivyowajibika Sakina na hatimaye anasaidia
kupatanisha Sara na wazazi wake.
c) Mwandishi alikusudia kukashifu tabia ya ubakaji kwa
kuonyesha athari zinazotokana na tabia hii.
d) Mwandishi pia alikusudia kukashifu taasubi ya kiume
katika jamii
WAHUSIKA:
Baba Sara
Katili
Kulingana na Sara,babake angemchinja na kumlaumu kwa kubakwa.
Hangemwamini Sara.Badala angemdidimiza zaidi pia
angemfukuza toka nyumbani.
a) Mkali
Ni kutokana na kuwa mkali ndio sababu Sara anashindwa
kumweleza kilichompata.
46.
Mama Sara
Dhaifu/mnyonge
Hawezi kujitetea mbele ya mumewe. Hawezi kutetea bintiye.Ni
dhaifu kwa sababu ni mwanamke.
Sara
Mnyonge/dhaifu
Baada ya kubakwa na kupata ujauzito aliishi kulia.Hakuwa na
njia ya kujitetea .Aliamua kulia tu.
Mwenye kisasi
Hakuweza kumsamehe yule mbakaji,alitaka kulipiza kisasi.Hata
baada ya kupata mtoto wake Sara bado alitamani kulipiza.
Msiri
Anaamua kutomwambia yeyote kuhusu kubakwa na hata kuhusu
ujauzito wake.
Mwenye Imani
Alikuwa na imani na raki yake Sarina.Aliamini kuwa Sarina
angemsaidia katika hali hii ngumu. Mtani
Anamtania Sarina kuwa ni zamu yake kubakwa.
Mcha mungu
Tokea hapo awali alijulikana kama mcha mungu.Hata kuvalia
jilbabu halikuwa jambo la kushangaza.
BELUWA.
Amewajibika ;
Yeye ni mlezi wa Sakina .Pia anaahidi kumpa kila msaada
uliohitajika kuhusu ujauzito.
Mshauri mwema
Alimshauri Sara aende hospitalini ujauzito ulipotimia miezi sita
kwani vipimo vya sasa vingelishirikisha mambo mengine ambayo
hayangeweza kufanyika nyumbani.
Ni Mpatanishi
Anawapatanisha Sara na wazazi wake.Baadaye wanakuwa na
uhusiano mzuri .Ujauzito uliokuwa mzito Sara unakuwa mwepesi.
Jasiri
Anawaelezea wazazi wa Sara kuhusu ujauzito wa Sara na
anapanga kuwakutanisha Sara na wazazi wake pale hospitalini.
47.
.MAJIRANI.
i.Ni wadaku.
Walikuwa wameanza kumsema Sara walipojua kuhusu ujauzito
wake.
MBINU ZA UANDISHI
1. Mbinu Rejeshi(kisengere nyuma).
Mwandishi hurudi nyuma na kuanza kusimulia kisa kilichokuwa
kimetendeka kabla ya alichokuwa(ashback).
a)UK 47..Aliendelea kuliona lile janadume asilolijua likimvamia na
kumbaka ghaa.Kisha likambamiza ardhini na ardhi ikashuhudia
ukatili na udhalimu ule.
b)UK 47…Anakumbuka vyema siku ile….ilikuwa ni jumatano moja
ya bahali mbaya kwake majira ya saa tatu unusu usiku,akirudi
darasani.
2)Takriri
Ni mbinu ya kurudiarudia neno moja au kifungu cha maneno ili
kusisitiza ujumbe fulani(Repetition). UK 47
a).Anaona alivyokuwa akigeuzwa kushoto na kulia,kulia na
kushoto.
b).UK 46 Ndiyo mbo yake,mbo yamnyonge na mnyonge ni
yeye sasa.
c).UK 49-50 Nimekosa
nini? Nini? Nini hasa?
d).UK 49 Dunia we dunia,Dunia na mwenye nguvu.
3Tashihisi/Uhuishaji(pensonication)
Ni mbinu ya kupatia kitu kisicho hai sifa za kiumbe mwenye
uhai(sifa za kibinadamu). (UK 47)
48.
a).UK 47….Kisha likambamiza ardhini na ardhi
ikashuhudia ukatili na udhalimu ule
b).UK 48….Bwana Yule mwenye masikio makaidi
c)UK 50……Kioo hakikumpa makini kamwe.
d)UK 50…. Akili imehama chumbani mwake.
Inaranda huku na huko kutafuta la kufanya.
e)UK 50…. Kila wazo likatangaza suluhisho mwafaka.
f)UK 53…. Kilio kikachukua nafasi.
4.Taswira
Ni matumizi ya lugha/maneno yanayojenga picha ya hali/jambo
fulani kwa msomaji.
a). UK 47…Kisha likambamiza ardhi na ardhi ikashuhudia ukatili
na udhalimu ule.
b) UK 47…..Anaona alivyokuwa akigeuzwa kushoto na kulia,kulia
na kushoto kama mdungo wa mshikaki juu ya tanuri la makaa.
5. TASHBIHI
a). UK 47…Anaona alivyokuwa akigeuzwa kushoto na kulia, Julia
na kushoto kama mdungo wa mshikaki juu ya tanuri la
makaa.
b). UK 52…Waliubeba kishujaa hata wakauhisi mwepesi kama
vunge la pamba.
c). UK 49…Kutengwa kama mgonjwa wa ukoma.Waliubeba
kishujaa hata wakauhisi mwepesi kama vunge la pamba.
d). Sara anabadilika kutoka msichana na kuwa mama.
e). Jina lake Sara linabadilika na kuwa mama Sara.
f). Baba aliyekuwa mkali anabadilika.
g). Uhusiano kati ya baba na mamake anabadilika na kuwa mzuri.
49.
6 MASWALI BALAGHA.
Maswali yasiyotarajia kujibiwa.
a).UK 49-50
Udhaifu na unyonge si ndio maana ya uanauke? Si ndio
unaotumiwa kutimiza unyama wao?Nimekosa nini? Nini?
Nini
hasa? Kipi kipya kilichotokea?
7. Ritifaa.
Mbinu ya kuzungumza na mtu aliyekufa (au asiyekuwepo)kana
kwamba yuko pamoja nawe.
UK 51…Sitakuua mwanangu kamwe,alikiahidi kijanacho.
8. Jazanda.
Matumizi ya maneno yenye maana che.
a).UK 47….Muhuzi mpya(ule ujauzito)
b)UK 47…Ukanda wa picha
c)UK 48…Ukurasa(maisha mpya)
9. UZUNGUMZI NAFSI.
Mhusika hujizungumzia,ama kwa kuongea au kuwaza,bila
kukusudia kusikika na yeyote.
a). UK 47….Aaa,maskini Sara miye,maisha yangu ndiyo
yameshakunjwa hivi! Alijiambia kimoyomoyo.
b).UK 49…Lakini kwa nini?na kwa nini hasa? Sena
aliendelea
kujiuliza ilivyopasa.Je!Nimetendewa hayo kwa sababu
ya
udhalifu wangu.
10.SADFA.
Ni kugongana kwa vitendo viwili vinavyohusiana kana kwamba
vilikuwa vimepangwa,japo havikuwa vimepangwa. (coincidence)
50.
UK 51…Shauri la usiniuwe la Abdulaif Abdalla ambalo Sena
alikuwa amelisoma siku mbili kabla ya mkasa huo kusudia
kilichompata Sena;ule ubakaji na kushika ujauzito.
UK 54….Wakati Sena alipokuwa akikiri atakavyo mwadhibu
baba wa mtoto wake? Ilisadifu kuwa wakati huo kukawa na ghasia
pale nje kwao.Ikawa aliyekuwa akipigwa na watu alikuwa ni Yule
mbakaji.Hatimaye akafa.
UK 52…Wakati Sena alipata ujauzito,kisadfa,babake akaanza
kumwita mama Sena.
Chuku:Kutilia chumvi.
UK 47…Hadi sasa pua yake imejaa ile harufu kali ya kutuzi
iliyompa kipalizi na kumkolizo.
MAUDHUI.
Mabadiliko.
1. UK 46…kuna mabadiliko katika mwili wa Sara… Sara
alishtuka wakati mkono wake uligusa tumbo lake, alihisi
mabadiliko ya kitumbo chake kilichokwishaanza kufura.
2. UK 50…Baada ya Sara kulia kwa muda mrefu, alitambua
kuwa kilio chake hakikumsaidia .Anaamua kutulia tena ,
kutojijutia na kutojilaumu tena.Anaamua kutafuta suluhisho la
tatizo lake kwa kuikabili dunia moja kwa moja.
3. Ujauzito uliokuwa mzigo mzito kwa Sara unabadilika na
kuwa mwepesi baada ya Sara kumweleza Sarina.
Ukatili
Ukatili ni kule kukosa utu /ubinadamu.
Lile janadume lililombaka Sara halina utu .Halikuwa na
huruma lilimkabamiza ardhini kwa ukatili na udhalimu (uk
47). Pia ni ukatili kwa jamii kumlaumu na kumtenda
aliyebakwa badala ya kumhurumia.
51.
ELIMU
Elimu imetiliwa maanani katika jamii hii na ndio sababu kuna
mpango wa masomo ya ziada ..twisheni.
NAFASI YA MWANAMKE.
a) Mwanamke anaishi katika ndoa ambapo hajui kujitetea nafsi
yake mbele ya mumewe kutokana na udhaifu wake.
b) Kama aliyewakulaumiwa kila kulipokuwa na visa vya
ubakaji.Yeye alionekana kuwa ndiye shetani.Kama chombo
cha kutimiza uchu wa mwanaume,kama aliyetumiwa kutimiza
unyama wa wanaume.Mwanamke ametengwa kutokana na
kosa la mwanamume.Baada ya kubakwa na kupata
ujauzito,mwanamke anatengwa shuleni,nyumbani na kila
mtu.
MAJUTO.
Sara alipobakwa hakumweleza yeyote kilichomfanyikia.Alienda
nyumbani na kukoga.Baadaye akawa anajuta kwa nini hakutoa
taarifa kuhusu kubakwa na kwa nini akakoga.
UNYONGE/UDHAIFU.
Sara alipobakwa alijawa na unyonge na ukiwa.Ni mnyonge kwa
sababu hata baada ya kubakwa hangepata haki,hangeweza
kujijitea,hangeweza kuaminiwa.Kilichobaki ni kulia na kulipiza
tu.Mamake pia ni dhalifu kwa kuwa hawezi kujitetea nafsi yake
mbele ya mumewe.
Sara anabakwa kwa sababu nimnyonge,unyonge unaotokana na
yeye kuwa mwanamke.Anasema Udhalifu na unyonge ndio
unaotumiwa na wenye nguvu zao.
TAASUBI YA KIUME.
Jamii hii inamuona kama mwanamume ni bora kuliko mwanamke.
Katika jamii hii,mwanamke alilaumiwa ndiye shetani kila
kulipotokea visa vya ubakaji.
52.
MASWALI.
Nimekosa nini ?nini ? Nini hasa ?
a) Eleza muktadha wa maneno haya.(AL4)
b) Ni mbinu gani za uandishi zinazojitokeza katika dondoo hili ?
(Al 2)
a) Jadili maudhui ya udhalifu na unyonge kama
yalivyojitokeza katika hadithi hii(AL 14)
“Thibitisha ukweli wa methali.Hakuna siri ya watu wawili.
Siri si siri inapotolewa kwa mtu mwingine”.
Sara alipomwelezea Sarina kuhusu kubakwa na ujauzito
wake.Waliamua kuwa wangeiweka kama siri.
Wakapanga kuwa Sara avalie vazi ambalo litaweza
kuucha ule ujauzito.
Wakapanga pia kuwa sehemu ya kujifungulia itakuwa
shamba kwa wazazi wake Sarina.
Walimhadithia dadake Sarina,Beluwa ambaye alikuwa
daktari wa uzazi.
Beluwa naye alipaswa kuweka siri hii.Mwezi baada ya
mwezi alichukua vifaa vya kupima mimba na kuvipeleka
nyumbani kumhudumia Sara,maana walitaka iwe siri kubwa.
Ujauzito ulipotimia miezi,Beluwa akamtaka Sena aende
hospitalini kwani vipimo vya wakati huo vingelishirikisha
mambo mengi ambayo hayangeweza kufanyika
nyumbani.Sara alipoka katika chumba cha daktari,kumbe
baba na mama yake Sara walikuwemo wanamsubiri ,kumbe
Beluwa alikwisha waeleza wazazi wake kuhusu ujauzito
wake. Siri ikawa si siri tena.
6. MASHARTI YA KISASA.
Na Alifa Chokocho
Msuko
Hadithi masharti ya kisasa ni hadithi fupi iliyoandikwa na Alifa
Chokocho. kwa mapana na marefu amezungumzia suala la
mapenzi. Anayalinganisha mapenzi na ugonjwa usiokua na dawa.
Mwandishi anaelezea mapenzi kupitia kwa mhusika Dadi njia hasi,
kuwa mapenzi ni mateso, utumwa, ukandamizaji, udunishaji na
ushabiki usio na maana.
53.
Dadi ni mchuuza samaki, licha ya hayo amezaliwa na kukulia mjini.
Dadi alikuwa amelemazwa na tamaa yake kwa Kidawa na alikuwa
akimwinda mara kwa mara. Kidawa alimwekea ukuta ili kuyakata
mawasiliano, mara kwa mara akajifanya kuwa hataki kuzungumza.
Siku moja, Kidawa alimkujia Dadi na kwa wakati huu akawa
mwingi wa maneno. Dadi alishangaa nakutoamini aliyokuwa
akiyasikia. Mkururo wa maswali uliompikita Dadi kwa mshangao na
wasiwasi mwingi kwa maana hakuamini.
Jambo moja ambalo Kidawa alikariri mara si moja ni usasa. Hili
halikumwia wazi dadi alilokuwa akimaanisha likawa ni fumbo
ambalo hata Dadi mwenyewe hakuweza kulifumbua. Katika
ukurasa 58, “nimekupimanisha Na kukuona mtu wa maana. Ila tu,
Zaidi ya hayo, nataka ujue kwamba mimi ni mwanamke wa kisasa
na mwanamke wa kisasa hutafuta mwanamme wa kisasa, mwenye
mapenzi ya kisasa. Huba ya Dadi kwa Kidawa ilimziba macho
asipigikamae msasa maneno yenyewe. Alisikia neno kisasa kama
mapigo yenye mahadhi mazuri.
Mwandishi anasema kuwa hii ingekua ndoa ya ajabu kama Dadi
angefahamu masharti ya ndoa. Lakushangaza ni kuwa alikubali
basi kuelewa mzigo ulioambatana na masharti hayo.
Bi Zuhura anamfanyia Dadi stihizai na kumtania sana.Baada ya
kufanyiwa mzaha, anaamua kutomuuzia Bi Zuhura samaki.
Tatizo la Dadi lilikua kumshuku mkewe kuwa ana uhusiano na
mwalimu mkuu.Hali hii inampeleka kumpeleleza. Anafululiza hadi
shulleni mahali ambapo mkewe alifanya kazi ya umatroni. Huko
anagundua kuwa wasiwasi wake ulikua wa bure katika shuguli
yake anatambua kuwa mkewe alikuwa radhi kuiacha kazi kwa hofu
yakuwa mmewe hakuwa anamwamini. Dadi anapofumanishwa
akichungulia anaanguka chini na kupoteza fahamu.
MAUDHUI.
1. MAPENZI
Mwandishi anayaona mapenzi kama kitendawili,
anayalinganisha na ugonjwa usiokua na dawa. Kupitia kwa
mhusika Dadi anayaelezea kwa njia hasi anayafasili kuwa
mateso, utumwa, ukandamizaji, udunishwaji na ushabiki.
Hata hivyo, Dadi anajitumbukiza katika mapenzi haya bila
kuyatalii. Kidawa anapendekeza mapenzi ya kisasa na
kusema kuwa atakuwa mke wa kisasa. Dadi hakuwa na
mtazamo huo. Mtazamo wake ulikuwa kupenda na
kupendwa bila masharti yoyote. Jambo hili linamfanya
kumshuku mke wake.
54.
1. USASA.
Mwandishi kupitia kwa mhusika dadi anaonyesha jinsi usasa
unavyoathiri maisha ya mwanadamu. Usasa ulikuwa na
maana ya kuchukua majukumu kwa zamu. Kidawa
alipendekeza wasaidiane katika majukumu ya kinyumba
kwa mfano; iwapo ameenda kazini. Dadi apike na kupiga
deki.Kidawa anasema kuwa yeye ni mwanamke wa kisasa.
Dadi alikiri kuwa mizani kwa kuwa amezaliwa na kulelewa
mjini anaelewa barabara. Hivyo basi, anayakubali yote
aliyoambiwa na Kidawa bila kuyatia kwenye mizani.
2. UTABAKA.
Kuna matabaka mawili. Tabaka la juu ambalo linawakilisha
mwalimu pamoja na Kidawa. Dadi ndiye anayejiweka katika
tabaka la chini na kujidunisha. Utabaka huwa ni zao la watu
wenyewe mfano utabaka unajitokeza pale ambapo tuna
m a k u n d i m a w i l i k a t i ya wa l e wa l i o n a v yo n a
wasiokuwanavyo. Dadi anaingiwa na kiwewe kutokana na
hali hii ambayo inamlemaza na kuulemaza uhusiano wao.
3. ELIMU.
Dadi ndiye anatufahamisha kiwango cha elimu ya Kidawa.
Yeye mwenyewe hatuambii alipokia anataja tu kazi yake.
Hata hivyo tunaskia kuwa kiwango chake cha elimu kilikua
chini kikilinganishwa na kile cha Kidawa.
4. NDOA/KUTOAMINIANA.
Ndoa inastahili kujengwa katika msingi unatokana na
kuaminiana. Hata hivyo, ndoa baina ya Dadi na kidawa ina
mushki kwa sababu Dadi ana wasiwasi . Wasiwasi huu
unatokana na kujidunisha kwake. Kwa upande wa Kidawa,
hana tatizo lolote. Kabla ya kuoana alikuwa ameyatoa
mashrti ambayo yangekuwa mwongozo wa ndoa yao. Kila
wakati ilipotokea hali ya swintofaham u Kidawa
alimkumbusha masharti.Ndoa hii inapata msukosuko pindi
Dadi anapoamu kumfuata mkewe akimshuku kuwa ana
uhusiano na mwalimu mkuu.
55.
6.MASHARTI.
Masharti yanayoambatana na tatizo linalotokana na
makubaliyano mara nyingi huweza kusuluhisha migogoro fulani.
Hata hivyo mojawapowa yale mawili anapokosa kuyatimiza, basi
huwa kunatokea mvutano na mgongano. Dadi aliingia katika
makubalioano kwa pupa bila kuyawazia hali hii inasababisha
matatizo makubwa, pindi anapofanya kosa, anakumbushwa
masharti.
Dadi aliingia katika makubalioano kwa pupa bila kuyawazia hali
hii inasababisha matatizo makubwa, pindi anapofanya kosa,
anakumbushwa masharti.
WAHUSIKA
1. DADI
Dadi ni mchuuza samaki kama tunavyofahamishwa katika
utangulizi wa hadithi. Licha ya hayo Dadi mwenyewe anadhibitisha
hayo anaposema kuwa mimi ni muuza samaki tu. UK. 58.
Ingawa kidawa ameelimika dadi hataki kubaki nyuma, anasema
kuwa amezaliwa mjini. Kulingana na Dadi kuwa usasa unaweza
kulinganishwa na maisha ya mji.
SIFA.
a) Mwenye bidii.
Dadi ni mtu mwenye bidii kazini. Kuzaliwa na kukulia mjini
kumemfunza namna ya kuyakabili maisha. Dadi hakutegemea
kazi ya kuajiriwa bali aliweza kujiajiri mwenyewe. Kazi ya
kuuza samaki inahitaji mtu mwenye jitihada, kuwatafuta samaki,
kuwatafutia soko kama tunavyoelezwa na mwandishi anapita
akitembeza samaki wa mwishomwisho. Uk 59.
b) Mwenye hamaki.
Msanii amewasiri Dadi mwenye hamaki pindi anapolazimishwa
kufanya hivyo. Hapendi kuingiliwa masuala yake ya ndani
sana.Bi. Zuhura anapomwingilia kwa hamasa, Dadi alitamka “
ukiwanunua utafanya heri” ukr 62. Bwana Dadi anachujia
baiskeli yake anamweleza peupe “ wewe hutaki samaki,
unataka umbeya na kujua mambo ya watu” Uk 63.
56.
c) Mwenye kujidunisha.
Dadi anajiona duni mbele ya Kidawa. Ana mawazo nyu
kuhusu hali yake na kazi yake. Anasema kuwa” mimi ni muuza
samaki tu” uk 58.
d) Mwenye kushuku
Kutokana na hali yake ya kujidunisha, Dadi anakosa kujiamini
kiasi kuwa hamwamini ata mkewe. Hali hii inafanya amfuate
mkewe hadi mahali pa kazi akimshuku kuwa na uhusiano na
mwalimu mkuu. Nusura hali hii inasababisha maafa makubwa.
Wasiwasi wake haukuwa na mashiko.
e) Mwenye pupa
Kiini cha matatizo yake ni kutokana na pupa yake katika
maamuzi. Kama angekua amemakinika asingeingilia ndoa
bila kutafakari masharti aliyowekewa na kidawa. Kilichokuwa
kimemzuga Dadi ni neno “kisasa”. Kiasi kuwa hangeweza
kuona chochote wala kusikia lolote lile.
UMUHIMU WAKE.
Ni kiwakilishi cha watu ambao hufanya maamuzi bila kujali
matokeo yake. Dadi ni mfano wa watu ambao hufanya
maamuzi yanayoadhiri maisha yao kwa kiasi kikubwa.
KIDAWA
Hili ni jina la kimajazi amabalo linawakilisha dawa katika
moyo wa kisasa ambaye anataka mambo yafanywe kwa
usasa. Anafanya kazi katika shule kama matroni.
SIFA
a) Mwenye dharau
Mwandishi anasema kuwa hawangeweza kupataan
anatumia fumbo kwa kusema” wakati wa zile siku ngumu
yeye alipotembea ardhini, kidawa aliruka hewani” ukr 56.
kidawa anadhihirisha dharau kutokana na viwitabia vyake
mfano
a) Uk 56 a) kuiburia midomo kumbeza
b) kidawa kumwambaa dadi
c) kumpa dadi mgongo
57.
(ii) uk 57 a) nimefuatwa na wanaume wengi walionitaka
uchumba.
b) “wenye uwezo na wasio nao”
(b) mwenye masharti
Ndoa yao ilijengwa kwenye masharti magumu ambayo hatimaye
yanaiadhiri kidawa alikuwa na mpango wake wa awali kuhusu
maisha ambayo angetaka waishi lakini dadi hakuyaelewa
masharti yale.
Masharti yale yalikuwa mpango wa awali wa ndoa yao na kama
dadi angeyaelewa ndoa yao ingekua ya kupigiwa mfano.
a) Mwenye mapenzi ya dhati
Kidawa alikua mwenye mapenzi ya dhati ni kutokana na
hali hii ambayo anayaweka mashrti ili asivunjwe moyo.
Alipomuuliza dadi kama mapenzi ni dhahiri kuwa
hakutaka kuvunjwa moyo. Alipokua akitafutwa
alionyesha kana kwamba hakutakauhusiano lakini ilikua
njia ya kukadiria kiwango cha mapenzi ya dadi kwake.
Kuandaa chakula ni ithibati kuwa alimpenda dadi. Hata
hivyo alikua tayari kuacha kazi yake ili kuonyesha penzi
yake kwa mmewe.
(d) mwenye mapato
Kidawa anasema kuwa alitafutwa na wanaume
waliosoma nna wasiosoma wenye uwezo na wasio nao.
Hii ilikua ni njia mojawapo ya kujigamba kuwa sio dadi
pekee aliyemtaka.
MWALIMU MKUU
a) Mwenye bidii
Mwandishi kupitia kwa mkewe mwalimu mkuu anaonyesha
jitihada za mwalimu kazini hasa tukizingatia kuwa ilikua ni
wakati wa jioni. Anazidi kusema kuwa huwa anfanya hivyo
kila siku kazi inapozidi. Wakati kidawa alipoenda
kwenye osi ya mwalimu mkuu alimpata akiwa kazini. Na
hata sauti yake ilishauri uchovu. Hii inaonyesha kuwa
mwalimu ni mchapa kazi.
58.
a) Mwenye hekima
Kidawa alipoenda osini akiwa na wazo la kutaka kuacha
kazi, mwalimu mkuu alimuuliza kama amekiria, anaonyesha
kuwa mbali na kuwa na hekima ni mshauri bora kwa sababu
anamwambia kuwa ni magumu. Anajali maisha yake na jamii
yake kwani hangependa ataabike na maamuzi ya haraka.
ZUHURA
(a) Mwenye dharau
Jinsi anavyomzungumzia dadi ni ithibati kuwa ana dharau.
Anaingilia masuala yasiyomhusu hasa yanayoingilia jamii.
Kumuuliza dadi kama wameshaoza ni kiwango cha juu cha
madharau.
(b) Mdaku
Bi zuhura anajiingiza kwenye mambo ya watu wengine. Alitaka
kujajua masual ya ndani ya kidawa na dadi
© Mjeuri
Anaposimamisha dadi anamuliza kama ana samaki wa kuuza au
anao wa kumkaangia bi kidawa, lake lingekua la kununua
samaki wala si mengine
MBINU ZA KUGHA
1. Maswali ya balagha.
Maswali ya balagha au tashtiti ni maswali yanayoulizwa na
msimulizi au mhusika ambayo yanahitaji jibu.
(i) Uk 56……kwa nini misumari ya nyuki inamuuma sasa ila si
wakati ule wa tamaa ya ushindi. Ilipokuwa mabli mbingu na
ardhi.
(ii) Uk 57……(a) bwana wewe unataka mapenzi utayaweza
a) Tuseme kisasanini
b) Ameshatuliza moyo wake
c) Nani angeangamini?
(iii) Uk 60…..(a) kwani dadi engewezaje kupuuza yale masharti
ya ndoa ya kisasa?
(b) yale masharti yanaendelea kumtamiriria
(c) dhana au ukweli?
(d) hata wepesi wa kufahamu kibinadamu hanao?
59.
(e) huyu mwanamke asiyechoka kujipodoa akiingiliana ndani?
(iv) uk 62…….a- kwa nini limkere mtu
b- watu inawahusu nini
c- mbona nawaona laini namna hii?
d- au wameshaoza?
a) Unaona mashavu ya samaki yalivyo mekundu hivi?
1. NIDAA
Ni usemi unaoonyesha kushangazwa na jambo Fulani na
huambatanishwa na alama hisi
(i) Uk 56…ni ugonjwa usio na dawa
(ii) Uk 57…..dawa ya ugonjwa wangu’
(b)………sikiliza dadi
(iii) Uk 58….ladha ya ajabu
(iv) Uk 60……eti dhana
(v) Uk 61…..masharti ya ndoa ya kisasa
(vi) Uk 62……Jamani
(vii) Uk63…….biashara haigombi hivyo
2. KUCHANGANYA NDIMI
Msanii anapoyaweka maneno yasiyo ya Kiswahili katika
sentensi ya Kiswahili, msanii anweza kufanya hivi kwa kusudia
au bila kusudia. Anafanya hivyo kuonyesha ana ya mhusika
anayehusishwa na uneni ule.
Uk 65 (i) ‘stop your gaze’

a) my dress, my choice’
b) Celeb ama socialite
1. UTOHOZI
Hii ni mbiu ya kuswahilisha maneno ya kiingereza na kufanya
yawe na mapigo ya silabi ya Kiswahili.
a) Uk 60… fasheni
b) Uk 61… umetroni
c) Uk 66…friji
d) Uk 67….paipu
e) Uk 69…. Ambulensi
60.
1. TASHBIHI
Huu ni mlinganisho wa kitu na kingine kwa kutumia kiunganishi
kama :mfano wa, mithili ya , kama na ja
1. uk 56….(i)akimwinda kama kunguru
(ii)kuambaa kama ugonjwa wa tauni
2. uk 57…..maskio kuwa wazi kama anga
2. TAKRIRI
Hii ni mbinu ya kurudiarudia neon moja au kifungu cha maneno
ili kusisitiza ujumbe Fulani;
(i) Uk 57…. Nani angeamini? Baada ya visa vyote vile dadi
alivyofanyiwa nani angeamini?
(ii) Uk 58…..(a) na mapenzi ya kisasa yana shuruti za kisasa
(b) lazima ufanye wajibu wa kisasa kwa mimi
nitakayekuwa mkeo wa kisasa
(iv) ) uk 59…..kwa hatua, kipembe baada ya kipembe
…….pom pom pom poom poom pom poom
3. MDOKEZO
Msanii hukatiza maneno au anaamua kuachia maneno bila
kutaja kitu. Mdokezo huwa ni mbinu ya kumfanyia msomaji
awze kujijazia kwa njia ya ubunifu
(i) Uk 59… pom poom pom poom pom poom
(ii) Uk 66,,,,,na tazama
(iii) Uk 67……lakini leo ni leo
(iv) Uk 68….labda anachungulia wasichana
MIFANO MINGINE
4. SADFA
5. UZUNGUMZI NAFSIA
6. MAJAZI
7. MSEMO
8. NAHAU
61.
7. NDOTO YA MASHAKA
Ali Abdulla ndiye mwandishi wa hadithi Ndoto Ya Mashaka. Yeye ni
mzawa wa Pemba. Ameondokea kuwa mwandishi stadi wa hadithi
fupi. Amechangia pia mkusanyo wa Damu Nyeusi na hadithi
Nyingine.
Mashaka alikua kijana aliyeishi maisha yaliyojaa mashaka.
Alizaliwa na baada ya muda akaitwa yatime. Mamake alifariki
alipomzaa kishaa babake akafuata,akashindwa kuvumilia
upweke. Biti Kidete akamchukua Mashaka na kumlea. Biti Kidete
daima alilalamika kuhusu miguu yake ambayo haikusikia dawa.
Ilimbidi Mashaka atafute vijibarua ili wapate riziki.
Baada ya Mashaka kumuoa Waridi,maisha yao yalijawa na shida
na umaskini. Jambo ambalo halikuwafurahisha wazazi wa Waridi
hawakulipenda.
Waliishi katika chumba kidogo ambacho hakikuwatosha. Walipata
watoto saba, sita kati yao walizaliwa kwa pacha tatu na mmoja
pekee. Waliishi katika mazingira yaliyokuwa duni na machafu. Siku
moja Waridi alishindwa kuvulia na akarudi kwao na watoto wote.
Mashaka aliyempenda Waridi sana alijawa na upweke na ukiiwe.
Alijitahidi kuwasaka lakini hakuwapata.
Kuna utabaka ambao unadhihirika wazi. Matajiri walio wachache
wanazidi kuwa matajiri zaidi. Nao maskini walio wengi walizidi
kuwa maskini zaidi . Ndotoni Mashaka anawaona maskini
(wasakatenge) wakiandawana na hatimaye maisha ya
wanabadilika na kuwa bora
Anwani
Anwani ‘Ndoto ya Maisha’ ni faafu kwa sababu hadithi nzima ni
ndoto. Kuwapo kwa Waridi na maisha yao, ni ndoto. Mashaka
anasema “Aaaa, kumbe ii yote ilikua ndoto, ndoto yangu Mashaka,
ndoto ya mashaka yangu , ndoto ya Mashaka isiyo Waridi wala
tamaa ya maisha kuboreka. Heri nisingeota.”
Dhamira
1.Mwandishi alikusudiwa kukashifu mfumo wa utabaka katika jamii.
2.Mwandishi alidhamiria kuonyesha athari za umaskini katika jamii.
3. Alitaka kuthihirisha ukweli wa methali, “Mapenzi ni majani,
popote penye mbolea hujiotea.”
62.
MAUDHUI
Umaskini
Watu wengi katika jamii hii wameathirika na umaskini. Kutokana na
umaskini wa Biti Kidete , Mashaka alilazimikakutafuta vijikazi ili
apate riziki. Aliweza kwangulia watu nazi au kwenda pwani
kurambaza au kuokota kombe na chanje.
Mashaka alipomuoa Waridi maisha yao yalizidi kuwa na shida
nyingi. Waliishi katika chumba kimoja kwa miaka mingi katika
mazingira duni. Kuliponyesha, michinzi ya maji lilionekana kwani
paa lilikua likifuja.
Chumba chao kilik]ua hakiwatoshi. Usiku binti zao walibanana na
mama yao kwenye kijichumba chao na wavulana wakalala jikoni
kwa chakupewa, jirani yao. Chumbani mlikua na vitu vichache tu.
Hawakua na sababu ya kuvinunua na pia hawakua na pesa za
kuvinunua. Mkewe alilalia mayowe na watoto wa kike wakalala
chini kwenye mbacha.
Wasakatenge waliathirika mno na umaskini hadi wakatamani
wafe.
Uchafu
Mazingira walimoishi wasakatenge yalikua machafu kupindukia.
Kwa mfano, chuma cha Mashaka kilikumbatiana na choo cha jirani.
Harufu yote kutoka chooni uliingia hadi chumbani mwa Mashaka.
Upande mmoja wa kile chumba kukawa na mfereji wa maji
machafu. Mvua uliponyesha , mfereji ule ulifurika na kwote kukawa
na uvundo. Wakati mwingine hawa wasakatenge walitumia
karatasi za plastiki kufanyia haja ndogo na kubwa kasha kutupa
huko nje.
Utabaka
Kupitia kwa Mashaka , tunaelewa pengo ulilopo kati ya watu wa
tabaka la juu na watu wa tabaka la chini ni pana sana (uk. 78)
Mashaka anauliza , “Na je , hizo fedha hupatikana wapi ?Nini
kinaleta tofauti hizi?kwa nini pengo hili kuzidi kukua na kupanuka
kila uchao?…”Matajiri wanazidi kuwa matajiri na fukara wakizidi
kufukarika na kudidimia
63.
Mapenzi ya dhati
Waridi anampenda Mashaka kwa kweli bila ya kuangalia uduni
na utupu wa Mashaka,alimpenda katika umaskini wake.
Mashaka pia alimpenda Waridi ‘kufa’. Alimpenda kwa hamu na
ghamu.Alipoachwa na Waridi hakua na dhamani ya maisha tena.
Alijitahidi kuwasaka bila ya mafanikio.
Ajira kwa watoto
M a s h a k a a l i t a f u t a v i j i k a z i a l i v yo v i we z a . A l i c h u m a
karafuu,akaangulia watu nazi. Alienda pwani kurambaza au
kuokota kembe na change. Pia alisaidia mtu kijikazi chake mkono:
kufyeka majani usoni pa nyumba yake ,kuyachanja kuni magogo
yake na hata kufua na kupiga pasi nguo zake… yote kwa lengo la
kutafuta riziki.
Kifo/Mauti
Kuna vifo vya watu tofauti. Mamake Mashaka alifariki alipomzaa.
Babake naye aliposhindwa kuvumilia upweke baada ya kifo cha
mkewe naye akafa. Hatimaye Biti Kidebe naye akaeafuata.
Urembo
Mashaka anaeleza kuhusu urembo wa Waridi. Anamlinganisha na
ua lenye hauba iliyotukuka na aliye na harufu nzuri.
WAHUSIKA
Mashaka
Ndiye muhusika mkuu
Mwenye mapenzi
1.Uk 74: Mashaka anasema alimpenda Waridi Kufa .
Anapowakosa Waridi na wanawe pale nyumbani alijitahidi
kuwasaka bila ya mafanikio.
2.uk 77: Mashaka alipoachwa na Waridi hakuona thamani ya
maisha tena.
3.uk 79: Mashaka anasema “Nilimpenda mno bila shaka,
nilimpenda kwa hamu na ghamu.”
4.uk 80: Waridi aliporejea, Mashaka alifurahi sana na hata
akasahau yote yaliyokuwa yamepita.
64.
Upweke na Ukuwe
1.Uk 87:Alikua mwenye upweke na ukuwe Waridi alipomtoka
katika maisha yake.
2.Babake Mashaka aliposhindwa kuvumilia upweke baada ya kifo
cha mkewe . Huo upweke ndio ulisababisha kifo chake.
Mwenye Mashaka
Maisha ya Mashaka ni mashaka matupu. Alipozaliwa, mamake
akafa na baadae babake akamfuata kwa kushindwa kuvumilia
upweke.Biti Kidebe aliyemchukua baada ya vifo vya wazazi wake
akawa naye hajiwezi kiafya na kimali. Mashaka yakamzidia
Mashaka. Huyo akawa anafanya vibarua ili apate riziki.
Hatimaye naye Biti Kidebe akafa.Baada ya kumuoa Waridi
matatizo yakawa chungu nzima. Yalipozidi Waridi akashindwa
kuvumilia na akamuacha Mashaka pekee. Akabaki akiwa na
umaskini.
Kufa moyo
Uk 79: Nikaona kira za nafsi yangu zinaendana na zile za moyo
wanguuliokwisha tamauka.
Uk 79: Mashaka anasema “Nimelioka hata naradua kufa kuliko
kuishi.”
Uk 80:Wanyonge wa tabaka la chini waliandamana huku
wakipiga kelele , “Tunataka Tufe!Bora Tufe!”
Waridi anashindwa kuvumilia maisha ya Mashaka na anaamua
kurudi kwao.
Maskini
Uk 74:Waliishi katika chumba kile kile kibovu kwa miaka mingi na
shida zikawa zinawatamirira kila upande. Kazi yao kubwa ikawa
ya kijungu-meko,kazi ya kupigania tumbo.Walilala chini na hata
kuomba nafasi kwa jirani. Hawakuwa na vitu chumbani kwani
hawangeweza kununua.
65.
Waridi
Mwenye mapenzi ya dhati
Uk 74: Waridi alimpenda Mashaka kwa dhati. Hakuangalia hali
duni ya Mashaka .Alimpenda katika umaskini wake.
Mapenzi hayachagui fukara wala tajiri kwani mapenzi huota
popote.
Mvumilivu
Aliweza kuvumilia maisha hayo ya umaskini kwa miaka mingi.
Mrembo
Uk 70: Mashaka anafananisha urembo wa Waridi na ua ambalo
hupendeza macho na kumfurahisha mtima.
Wasakatange
Ni watu maskini wa tabaka la chini. Walitamani kutokana na hali
yao duni.
Mzee Rubeya
Alikua babake Waridi.
Alikua na asili ya Yemeni.
Alikua tajiri ambaye alihuzunishwa na ndoa ya Mashaka na bintiye
Waridi kwa sababu Mashaka alikua maskini.
MBINU ZA UANDISHI
Jazanda
1.Ua la Waridi limetumika kijazanda kulinganisha Waridi mke wa
Mashaka.(uk 70)
2.Mashaka analinganisha mshahara wake na mkia wa mbuzi.( uk
76)
3.Nitaramba na kulmbatua asali yake tamu kama nyuki (uzuri
wako).
Maswali Balagha
Ni maswali yanayoulizwa na msimulizi au mhusika ambayo
hayahitaji jibu (rhetorical question).
66.
Uk 70: Na harufu yake je?
Leo harufu tu ina sifa hiyo, waridi lenyewe je?
Ni Biti Kidebe mamangu, au waja tu na dharau zao?
Uk 76:Wamekwenda wapi watu hawa?
Uk 78: Na je ,hizo fedha hupatikana vipi? Mbona kuna pengo
kubwa kati ya walionazo na wasiokuwa nazo? Nini kinaleta tofauti
hizi?
Nyimbo
Uk 77: Wimbo uliopigwa na redio Tanzania Dar ulipendwa sana na
Waridi. Wimbo huu unaonesha hisia za kutamauka. Mtu aliyekufa
moyo
Methali
Uk 70: Baada ya dhiki faraja
Jungu kuu halikosi ukoko
Uk 75: siri ya mtungi iulize kata au kitanda usichokilalia hujui
kunguniwe
Uk 78: Subira ni ufunguo wa heri.
Uk 79: Ngoja ngoja huumiza matumbo
Chuku
Ni kutumia maneno yaliyotiliwa chumvi ili kusisitiza ujumbe Fulani
au kusia kitu.
Uk 71: Nikalienzi ua langu kuliko hata mboni za macho yangu
Uk 74: Nampenda kufa
Uk 76: Dhiki ndio ilikua nguo na harufu yetu.
Uk 80: karne nzima imepita sasa pasi na kuliona ua langu. Ndio
kwanza leo nilitie jichini baada ya miaka mia. (muda mrefu
sana)
Tabaini
Matumizi ya kikanushi ‘si’
Uk 72: Si maisha si wazimu
Uk 71:Si ya sasa si ya baadae
67.
Tashihisi
Hii ni mbinu ya kupatia kitu kisicho hai sifa za kiumbe mwenye
uhai(binadamu)
Uk 74: Harufu yote itapikwayo na domo la choohicho
Uk 74:Nao hutema uchafu wao katika mto Msimbazi.
Uk 76:Katika maisha hayo siku zilijisotora zikapita kama hazitaki.
Uk 82:Rangi ya urujuani ulichungulia katika nyufa
Uk 88: Mwili wangu niliuhisi mtamu. Ulinitafuna kama kidonda
Uk 79: Haukutoka (msemo) na wala haukutaka kamwe kutoka
Utohozi/Kuswahilisha
Uk 74: Plastiki
Takriri
Ni mbinu ya kurudia rudia neon moja au kifungu cha maneno ili
kusisitiza ujumbe fulani. (repetition}
Uk 81: Ilikua radi iliyopiga kila mahali. Ilika kila mahali. Kila
mahali uliingia.
Uk 79: “Hadi lini lakini…hadi lini…”
Tashbihi
Hii ni mbinu ya lugha inayo linganisha vitu au hali mbili tofauti kwa
kutumia maneno ya kulinganisha:kama, mithili ya,sawa na,je.
Uk 72:Akaiga dunia bado mbichi kama jani la mgomba
Uk 73:Rubaa ya watu wane ikajitema chumbani kama askari wa
fanya fujo uone
Uk 74:Choo chenyewe kimeinuka juu kama ghorofa
Uk 75: Wavulana walilala jikoni kama nyau…
Uk 76: Katika maisha hayo siku zilijisotora zikapita kama hazitaki
Uk 77:Ilikua tamu kama ya ndege wa peponi.
U k 7 7 : N i l i k u a k a m a n d e g e k a t i k a t u n d u
uk 88: Ni maadamano yale walikua wamefwua na kufwuana kama
unga
68.
Majazi
Ni pale tabia za wahusika zinaambana na majina yao halisi
Uk 73:Waridi: Mashaka anasema jina lake lilipige ndipo bila
shaka. Linaelezea urembo wa Waridi
Uk 74:Wasakatenge (maskini)
Uk 75:Chakupewo ?(anawapa mahali pa kulala)
Misemo
Uk 72:Kusalimu amri
Uk 72:Maji yalipozidi unga
Uk 72:kupiga kite
Uk 76:Ziligonga mwamba
Uzungumzi nafsia
Mhusika hujizungumzia, ama kuwa au kuongea bila kukusudia
kusiko na yeyote.
Uk 76:Nilijiuliza lakini jibu sikupata
Uk 77:Niliwaza mengi zaidi. Nikawaza ya laity ningekua na
maisha mazuri.
Uk 78:Nafsi yangu uliniambia “subira ni ufunguo wa heri.”
Uk 79:”Hadi lini lakini…hadi lini. Subira hiyo?” Moyo uliuliza
Maswali
1.Mashaka, Waridi na wasakatenge ni majina ya majazi. Thibitisha
kutoka kwa hadithi
2.Onesha jinsi mwandishi wa hadithi ya Ndoto ya Mashaka
amefaulu katika matumizi haya
a)Chuku
b)Tashisi
c)Tashbihi
d)Nahau
Chuku
ni kutia chumvi katika jambo ili ufafanuke zaidi au lieleweke
waziwazi.
Uk 71:Nikalienzi ua langu kupita hata mboni za macho yangu.
Uk 74:Nilimpenda kufa
Uk 76: Sura zetu zilitosha kuwa sura za kusemea
Uk 76: Dhiki ulikua ndio nguo na harufu zetu
Uk 80:Karne nzima imepita sasa pasi na kuliona ua langu.Ndio
kwanza leo nilitie jichoni baada ya miaka mia.
69.
8. KIDEGE
ROBERT W EDUOR
Msuko
Hadithi hii imejikita katika mazingira ya bustani.Bustani ya ilala ni
mahali ambapo wapenzi walikuwa wakikutana.
Taswira inayojitokeza ni ya watu wanaopendana.Ili kusisitiza
jambo hili,mwandishi anazungumzia rangi.Rangi inapotumika
kisanaa huweza kuwasilisha wazo Fulani.Msanii anasema kuwa
,’Nyasi zilikuwa zimepiga umanjano na kukaribisha binadamukwa
hali za kila aina’uk83.
Msimulizi anasema kuwa mahali hapa ni mandhari ya
wapendanao.Ni mahali ambapo waja huzungumzia mambo mengi
na wengine wakiwa na mambo mengi.Tunaelezewa kuwa mahali
pale ni mahal I pa kuanzisha uhusiano.
Msimulizi anasema kuwa,kati ya waliokuwa wakizuru Bustani ile ni
Joy na Achesa,Siku hiyo walikuwa na mchezo wa kitoto.Wakiwa
katika mchezo,mawazo ya Achesa yanatekwa na ndenge
mmoja.Ndenge Yule alimfanyia mambo ya ajabu,akawa ni
mhusika muhimu katika masimuluzi haya.Pamoja na ndenge Yule
inasadifa kuwa Mose alikuwa amejibanza………
Jina halisi la mose ni Musa.Mose alikuwa mapenzi makuu kwa
samaki waliokuwa kwenye kidimbwi.Kutokana na mapenzi yale
akawa na mazoea ya kuwasilisha na kuwatunza.Mose alikuwa na
raki yake kwa jina Shirandula.Shirandula alikuwa mtani mkubwa
wa mose,alimtegea mose kitendawili ambacho kilimlemea.
Mose aliota ndoto usiku wa kuamkia jumamosi,ndoto ilikuwa juu
yan midege ya ajabu.Katika uhalisia anaamua kuelekea kwenye
bustani.
MAUDHUI
a) Uhusiano mwema.
Uhusiano mwema hudhihirika kutokana na mahusiano na
mwingiliano barua ya watu.Katika hadithi kidege
unadhihirika kati ya Joy na Achesa.Wanaonyesha hali hii
kwsa kucheza pamoja mchezo wa kitoto.
Mose anataniana na maraki hawa bila kuwaudhi UK85
wakabaki wanachekeana,ama wanachekacheka ovyo.
70.
a) Mapenzi
Mapenzi yanadhihirishwa na wanadamu wanapojituliza
chini kwenye vipimbe vilivyowacha wakiendeleza
mining’ono ya mapenzi.Mapenzi yanayolengwa ni ya
mwanamke.Mwandishi anasema kuwa mahaba
yamewafura.Anamaanisha kuwa mapenzi yamekita mizizi
katika jamii hii,mwandishi anatutilea taswira ya ndege
wanaotazama wanadamuwakiwa katika haba.
b) Utunzaji wa mazingira na viumbe.
Mose alijipatia wajibu wa kuwatunza samaki na
ndege.Aliwatupia samaki kipande cha sima bila kuwasahau
ndege.
B u s t a n i ya i l a l a i l i k u wa i m e h i f a d h i wa v i z u r i .
Mwandishianasema kuwa uzuri………………???????????
h a wa k u wa wa n aya h a r i b u m a z i n g i ra ya l e. H a t a
samakiwaliokuwa kwenye kidimbwi hawakudhuriwa na
wanadamu.
c) Uraki
Uraki unajitokeza kwenye hadithi Joy na Achesa ni
miongoni mwa maraki waliokuwa wakijituliza kwenye
bustani.Ni maraki tu ambao wanaweza kuwa na mchezo
uliokuwa ukichezwa.Licha ya hao wawili,kulikuwa na Jozi
nyingine ya maraki nao ni Mose na Shirandula.
d) Starehe
Katika hadithi hii,mwandishi anatupeleka kwenye mazingira
ya bustani.Bustani ya ilala ilikuwa na uzuri wake ndio maana
watu walikuywa wakienda mahali pale ili kustarehe.
WAHUSIKA
Hawa ni watu,vitu au viumbe wanaoishi katika kazi ya
kisanaa kwa lengo nla kubeba dhamira mbalimbali na
kuiwasilisha kwa wanajamii.Mwandishi wa hadithi kidege
amewatuma wahusika wa aina mbalimbali.Amewatuma
wahusika wanadamu,ndege na samaki wote kwa lengo la
kuwasilisha madhumuni yake.Kuna wale aliowadokeza na
hawa kuendelea zaidi wakawapokeza wengine majukumu
ya kuendeleza maudhui.
71.
1) MUSA
Jina la utani ni Mose,jina hili linaendelezwa hadi mwisho wa
hadithi.
SIFA
a) Mwenye bidii
Licha ya kuwa na shughuli zake aligeuza uhusiano wake
na samaki kuwa wajibu.Vipande vya sima alivyokuwa
akivibeba havikuwa vyake bali vilikuwa vya kuwalisha
samaki na ndege.Hata katika ndoto yake anapovamiwa
na midege,kra zake zinampeleka mfukoni kwani
yalikuwa ni mazoea yake kuwalisha.
b) Mwenye mapenzi makubwa kwa samaki.
Mose aliwapenda samaki na kuwafanya uraki
nao.Aliwatunza samaki hata kama haikuwa kazi
yake,alichukua wajibu wa kutenda hayo (uk86).Samaki
walimjua na kumzoea, hii inatokana na hali ya kuwatupia
vipande vya sima.
c) Mtani
Mose alitaniana na shirandula ndio shirandula alimtegea
mose kitendawili.Kitendawili ambacho aliomba siku mbili
ili akitegue.
d) Mkarimu
Aliweza kuwatunza na kuwalisha wale viumbe.Iwapo
angekosa siku mbili au tatu,siku ya nne angefanya juhudi
kuwatembelea.Hali hii inaonyesha ukarimu wa muda
wake na kidogo alichokuwa nacho…..ni yeye tu ambaye
angeweza kuwatembelea kwa madhumuni ya namna
hii.(UK 89)
e) Mtabiri
Ndoto yake inakuwa ni utabiri wa mambo ambayo
yangetokea.Ndoto ni kioo cha yaliyojiri baadaye.
f) Anamlahaka mwema
Mhusika huyu anaonyesha jinsi wanavyoingiliana na
maraki zake.Hii ndiyo sababu iliyomfanya ajibanze
mahali akiwatazama Joy n AchesA.Yeye na shirandula
hawakuwa na utofauti.
72.
1) Shirandula:
a) Mtani
Mwandishi anatuelezea kuwa Shirandula alizoea
kumtania mose kila wakati kutokana na utani wake
hakosi la kusema anavyoeleza kuwa c hoo
kinachimbwa kasha kinajengwa..(UK87)
b) Mbunifu
Mtu mbunifu hakosi la kusema pindi tu anapojipata
katika hali ya kujitolea.Shirandula hakukosa la
kusema katika kitendawili.Mfano wanapozungumzia
kuhusu choo na kuelezwa kuwa choo hakijengwi
kinachimbwa…(UK86)
Anatoa jibu mara moja…(UK87)
c) Mcheshi
A n a p o p a t a j i b u l a m o j a k wa m o j a . Awa l i
anazungumzia kuhusu vijisamaki ambavyo anasema
huwezi kuvila na anauliza ni vya faida gani.
d) Mshamba
Watuwa mji wanamwita mshamba kwa kuwa yeye
alizaliwa kijijini.Mbali na kuzaliwa kijijini,tabia zake
zinadhihirisha hali hii kutokana na mawazo yake
kuhusu samaki.
2) JOY NA ACHESA.
Hawa ni baadhi ya wale waliokuwa wakizuru bustani ili
kujituliza.
SIFA
a ) Wenye mapenzi ya dhati.
Hawa wawili wanaonekana kuwa na mapenzi ya muda
,kama tunavyoelezwa na mwandishi kuwa walikuwa na
mazoea ya kuzuru mahali pale.
73.
b) Watani
Kutokana na mchezo wanaocheza wa kitoto ni bayana
kuwa lazima wawe wametaniana.Joy kumrukia Achesa
na wote kujikuta wakiwa chini.
c). Wacheshi
Kila mmoja anaangua kicheko kutokana nay ale
wanayoyashuhudia.
MBINU ZA LUGHA.
1. Uhuishi/Tashihisi.
Hii ni tamathali ya usemi ambayo msanii huvipatia
vitu sifa walizonazo binadamu kutenda na kufanya
kama wanadamu..
a)Ndege walijibizana,mmoja huku na mwengine kule
wakizungumza(UK83).Ingawa ndege wana uhai
huwa hawazungumzi,msanii amewapatia sifa ya
kuzungumza.
b) Ndege naye pale mtini akaona na kushangilia..(UK
85)
C) Ndege akaamua kuwafunganisha ndoa…(UK85)
d) Fikra zikamtuma mfukoni (UK89)
2. Tabaini
Ni tamathali ya usemi ambayo msanii hutuma usemi
unaosisitiza jambo kwa kutumia maneno ya ukinzani
a) Jua si jua,baridi si baridi(UK 83)
b) Si wakubwa ,wala si wadogo(UK89)
c) Mwewe si mwewe,tai si tai(UK89
3) Takriri
Ni mbinu inayotumiwa na msanii ya kurudiarudia neno moja au
kifungu cha maneno kwa lengo la kusisitiza : Mfano ;
i. Wakabingiria,Wakabingiria ….UK 84
ii. Samaki kumvutia mose,mose kumvutia ndege,Ndege
n a y e k u m v u t  a n a n i ? M o s e n a
Ndege,………………UK88
iii. Vuta,Vuta ………….….UK92
Shika, shika……………….UK86
74.
1) Nidaa
Huu ni msemo unaotumiwa na msanii kuonyesha kushangazwa na
jambo Fulani na huambatana na alama ya hisi au mshangao.
a) Poa! UK 83
b) Usivue! UK 86
c) Lakini wapi! UK 89
d) Lo! UK 94
e) Hawa watu na matamshi yao! UK 87
1) Tashbihi
Tamathali ya usemi ambayo msanii anavilinganisha vitu viwili
au zaidi, kwa kutumia maneno kama vile
Mfano wa mithili ya,kama na ja.
i. Alifuata desturi kama ibada…UK 89
ii. Midomo kama panga….UK 91
2) Tanakali za sauti
Hii ni mbinu ambayo msanii hutumia kuiga sauti za milio
mbalimbali. Milio inaweza kuwa ya vitu,wanyama n.k
i. Ndege alitoa sauti chwi!UK 84
ii. ………alikuwa keshamrukia pu !UK 84
iii. Kikalenga kwenye pua, chwa !UK 85
iv. ………Sauti yake ya kawaida chwi!UK 90
Chwi!……Chwi!……Chwi! UK 92
MTINDO WA UANDISHI
Msanii ametumia mtindo wa fasihi simulizi.Ameweza
kuingiza tanzu za fasihi simulizi katika masimulizi
yake.Lengo la kufanya hivi ni kuendeleza dhamira yake
na kuyakuza maudhui:
a) Utanzu wa maigizo
Mwandishi ametumia kipera cha kitendawili UK
90Kitendawili!Tega! Anayejenga choo na
anayejenga?
75.
8. NIZIKENI PAPA HAPA
Ken walibora ni mkaazi wa Kenya, na mwandishi maarufu wa
Kiswahili. Ni mwandishi mtajika wa kazi ya fasihi ya Kiswahili.
MUHTASARI
Nizikeni papa hapa .Haya yalikuwa maneno ya otii mwenyewe.
Otii alikuwa akisakatia kandanda timu ya Bandari FC Kwenye
uwanja wa manispaa na kote inchini.Wakati huo alikuwa na siha
yake na aliishi Mombasa.
Anakutana na Rehema Wanjiru msichana aliyekuwa mrembo Zaidi.
Rehema alimwambukiza Otii ugonjwa.Akawa anaendesha
akakonda sana na akawa na kikohozi kisichokoma .Ugonjwa huu
unampeleka hadi kaburini .
Kabla ya kifo chake ,wanachama wa chama cha nyumbani
wananza kukutana kwake kupanga mipango ya mazishi .Walihitaji
kuchangisha fedha za kukondisha magari yakuchukua maiti na
waombolezi kutoka Mombasa hadi sidindi karibu na Kisumu.Otii
hakuona umuhimu wa safari hii ya kutoka Mombasa hadi sidindi
.Anapendekeza azikwe hapo Mombasa.
Hakuna anayesikiza ombi la Otii .Wanasisitiza lazima
{azikwe]maiti ya Otii angepelekwa Kisumu kulingana na mila na
desturi zao. Jamaa na maraki na watu wa nyumbani lazima
waandamane kupeleka maiti Kisumu. Walipoka mtito Andei
wanakabiliana na Lori refu ambalo lilikuwa likija kasi huku
linayumbayumba barabarani. Dereva wa matatu iliyokuwa
imebeba maiti alijaribu kukikwepa kichwa cha lori lakini
hakufanikiwa. Watu arubaini walifariki hapo papo . Wengine kumi
na watatu walijeruhiwa ,baadhi yao vibaya sana.
Yote haya yalisababishwa na kupuuza . wangemsikiliza otii mambo
hayangeishia vile;
ANWANI
Anwani ya hadithi hii nizikeni papa hapa inaoana na yale
yaliyomo. Hili lilikuwa ni pendekezo la Otii kuwa akifa maiti
yake isisarishwe hadi Kisumu lakini azikwe papo hapo
Mombasa.
76.
DHAMIRA (LENGO)
1. Mwandishi anakusudia kuonyesha umuhimu wa uhusiano
katika kufanya mambo
2. Anadhamiria kukashifu mapenzi ya kiholela na kutuonyesha
athari zake. Mf uhusiano kati ya Otii na Rehema Wanjiru.
3. Mwandishi alidhamiria kuonyesha ukweli wa methali
asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
MAUDHUI MILA NA DESTURI
Wananchama cha watu cha nyumbani wanasisitiza kuwa lazima
otii(maiti) ipelekwe Kisumu kulingana na mila na desturi.
Wanasema katika mila na desturi zetu kauli ya marehemu si
chochote, si lolote, muhimu ni kwmba sharti mtu wa kwetu azikwe
nyumbani.
USHIRIKIANO/ UMOJA
Wanachama wa chama cha watu wa nyumbani wanatangamana
na kupinga mipango ya mazishi ya oti. Baada ya kifo cha otii,
jamaa na maraki wa watu wa nyumbani ya mazishi walikjumuika
kwa wingi, katika kitongoji duni cha Kisumu ndogo kupanga
mazishi. Kwa pamoja wanachangisha fedha za kununua jeneza,
mavazi ya kumvalisha maiti pamoja na fedha za kukodisha magari
ya kuchukua maiti nyumbani, siku ya kupeleka maiti nyumbani
wanajitokeza kwa wingi.
UJEURI NA ATHARI ZAKE
Wanachama wa chama cha watu wa nyumabani walipoanza
mipango ya mazishi na hata kufanya michango ili kugharamia
mipango ya kupeleka maiti nyumbani.Otii aliwaambia mara
kadhaa wamzike papo hapo Mombasa laikini hawakumsikiza.
Walipokuwa safarini kuelekea Kisumu, kunatokea ajali mbaya
ambayo inawaangamiza wengi na wengine wanapata majeraha
mbaya.
(uk100) rakiye Otii anamtahadhirisha Otii dhidi ya kuwa na
uhusiano na wasichana wazuri Zaidi kama Rehema Wanjiru. Otii
hakutilia makini hayo. Alisema “pana hasara gani nzi kua
kidondandani?”Aliendelea na uhusiano huu. Akapata ugonjwa
uliompleka kaburini.
77.
SIFA ZA WAHUSIKA
OTII
Otii ndiye mhusika mkuu
Mchezaji hodari.
Aliyechezea timu ya Bandari FC kwenye uwanja wa manispaa na
kote nchini. Alichezea timu ya taifa Harambee stars wakati
alipotambaa jijini Mombasa .UK98 anakumbuka mataifa mengi ya
kigeni alikosari kwenda kusakata Kabamba kwa niaba ya taifa
lake na jukumu la kupeperusha bendera ya nchi yake.Alipokuja
tamko la michezo lililonukuliwa gazeti lilikisi kira za wengi. Pengo
la Otii haliwezi kuzibwa.
MBADHIIFU
Wanachama wa chama cha watu wa nyumbani walipokutana
kupanga mipango ya mazishi, walikusudia kuchangisha fedha za
kununua jeneza, mavazi ya kumvalisha maiti pamoja na fedha za
kukodisha magari ya kuchukua maiti na waombolezaji hadi sindindi
yeye hakutaka hayo alisema, ‘ gharama zote hizo za kunipelka
sidindi za nini? Lakini wenzake wakasisitiza kuwa gharama hizo ni
zao si zake{UK97]
UJEURI/MWENYE MAPUUZA
Alipotahadharisashwa dhidi yakuwa na uhusiano na huyo msichana
mrembo Rehema Wanjiru alipuuza.Hatimaye akaambukizwa
ugonjwa uliompeleka kaburini.
CHAMA CHA WATU WA NYUMBANI
1.Umoja/ushirikiano
Wanashirikiana kuanzia mwanzo hadi mwisho katika kupanga
mazishi ya Otii wanachanga pesa, wanakutana kwa Otii na
wanafuatana kuelekea sidindi kuhudhuria mazishi ya Otii.
2.Wanamapuuza
Otii alisisitiza kuwa yeye angetaka azikwe palepale Mombasa
lakini wakapuuza. Hatimaye wakapata ajali mbaya sana wakiwa
safarini kwenda sidindi kuhudhuria mazishi.
78.
3.WATAMADUNI
Wanasisitiza lazima wamzike otii nyumbani kulingana na mila zao.
Ni kinyume cha mila na ada zao kumwadia mwenzao kutupiliwa
mbali kana kwamba hana kwao.
WAKARIMU
Wanahakikisha wamechanga pesa za kutosha kugharamia mazishi
ya otii.
REHEMA WANJIRU
Ni msichana wa aina yake, mwenye urembo wa kutikisa jiji zima,
urembo wa kulikausha bahari, urembo uliompa wasichana wenziwe
husuda na wanaume mshawasha Fulani.
MZINIFU
Kuna uwezekano kuwa ugonjwa huu aliupata kupitia tabia ya
uzinifu.
MBINU ZA UANDISHI
Chuku(hyperbole)
Ni kutumia maneno yaliyotiliwa chumvi ili kusisitiza ujumbefulani au
kusifu.
Uk 96…. kituamepotelea kwenye kitanda chake( mdogo Zaidi)
Uk 97…..Alipokua anakanyaga ardi mpaka inatetemeka( kwa
nguvu kutokana na afya nzuri)
Uk 100.. urembo wa kulitikisa jiji zima( mrembo sana)
Uk 101.. pengo aliloacha otii haliwezi kuzibwa( mchezaji stadi)
Uk 102.. wanahabari waliotiwa mbinu ya kupiga picha
hawakuweza kula nyama tena mazishini mwao.
Istiara
Ni kulinganisha vitu viwili moja kwa moja.
Uk 96….. kabakia sindano (ameendelea sana)
Uk 96 wanamwita mbu ( mdogo Zaidi)
79.
Tashbihi (simile)
Ni mbinu ya lugha unayolinganisha vitu au hali mbili tofauti kwa
kutumia maneno ya kulinganisha, kama mithili ya, sawa na ja;
Uk 98. Hakuweza kunyanyuka pale chini alikoabwagikie kama
gunia la chumvi.
Uk 99…. Alikuwa ametupwa kama masimbi yabuzaa
Uk 102…. Akajaribu kukwepa kichw acha hari kilichokua
kimemkodolea macho kama simba wa Hifadhi ya Wanyama ya
Tsavo.
Jazanda:
Kutumia maneno yaliyo na maana che.
Uk 96…jamaa zake si watu wa kusubiri mvua kunyesha ndipo
waanze kutafuta pahali pa kununua mwavuli..(jeneza)
Uk 98…. Alikua mwibe.
Uk 97,,, mbwa( kitu kisicho na thamani)
Uk 100… pana hasara gani nzi kua kidondani.
Utohozi
Ni mbinu ya kuwahilisha maneno ya lugha yatamkike kama ya
Kiswahili.
Uk 98…. Manispaa(Municipal)
Uk 98…..mechi(march)
Uk 99 eksirei(xray)
Uk 99… klabu (club)
Uk 96 fremu
MSEMO
UK 97… Anapiga chafya.
Uk 99…. Akichungulia kaburi.
Uk 99…..Hawakujali hawakubali.
Uk 99….kufumba na kufumbua.
Uk 100..akapigwa na butwaa.
80.
Tashhisi/ Uhuishaji.
Hii ni mbinu ya kupatia kitu kisicho hai sifa za kiumbe mwenye
UK100 urembo wa kulikaulisha bahari.
Uk.101.sifa za kibroda waombolezaji na kutapika wengine.
102 akajaribu kukikwepa kic hwa c ha lori kilic hokuwa
kimemkondolea macho.
METHALI
Uk.99. Mwacha kile hanacho na chema kimpotele.
Uk.99.aliyeumwa na nyoka akiona ungongo hushtuka.
Tabaini
Ni tamathali ya semi ambayo kwayo maneno/mawazo
yanayokinzana hutumiwa katika sentensi ili kuleta msisitizo wa
wazo.
UK99.si barabara ya mlango wa papa ,si barabara ya Nkrumah, si
barabara ya jomo Kenyatta, si ya Digo
UK100..Si kuendesha, si kukonda, si vipele si si kukichwa
kukikokome….
Mbinu rejeshi
UK96….Ukutani kumetundikiwa fremu yenye picha yake alipokuwa
bado na siha yake alipokuwa akisakatia kandanda timu ya
bandari FC.
Uk95…anakumbuka jinsi alivyokuwa akiwala chenga wachezaji
wa timu pinzani.
MASWALI
1. Anwani Nizikeni papa hapa ni mwafaka kwa hii
hadithi.Fafanua.[al 20]
2. Anzeni mapema kuchangisha fedha za kusarisha
maiti.
a] Eleza muktadha wa dondoo hili. [al 4]
Haya ni maneno ya mwenyekiti wa chama watu wa nyumbani
walikuwa kwa Otii kando ya kitanda cha Otii ili kupanga mikakati
ya mazishi. Hii ilitokea baada ya daktari kuwaeleza wamrejeshe
Otii nyumbani kwa kuwa hakukuwa na matumaini ya kupata afueni.
81.
b] Walihitaji pesa za nini? [al 4]Walipaswa kununua jeneza,mavazi
ya kumvisha maiti pamoja na fedha za kukodisha magari ya
kuchukua maiti na waombolezaji kutoka hapa
Mombasa hadi Kisumuasilia.
c)Kwa kurejelea hadithi ya nizikeni papa hapa , eleza maafa
yanayotokana na ujeuri na mapuuza.
Wanachama wa chama cha watu wa nyumbani walipoaanza
mipango ya mazishi na kufanya michango ili kugharamia mipango
ya kupeleka maiti ya Otii nyumbani.Otii alipendekeza azikwe pale
Mombasa lakini hawakumsikiza kabla ya Otii kukata roho. Pia
aliwakumbusha pendekezo lake la kuzikwa pale Mombasa,lakini
bado hawakutilia pendekezo lake maanani. Walipokuwa safarini
kuelekea Kisumu walipata ajali mbaya ambayo iliangamiza wengi
na wengine wakapata majeraha mabaya.Wangemsikiliza Otii
hawangepanga safari ya kwenda Kisumu na basi hakungekuwa na
ajali hii ambayo ilileta maafa Zaidi.
UK100….Rakiye Otii anamtahadharisha Otii dhidi ya kuwa na
uhusiano na wasichana warembo kama Rehema Wanjiru lakini Otii
alipuuza .
Aliendelea na ule uhusiano akaambukizwa ugonjwa uliompeleka
kaburini.
MASWALI
Methali ni nini? taja na ufafanue
Methali zilizotumwa katika hadithi ya mama bakari.
10.TULIPOKUTANA TENA
ALIFA CHOKOCHO
Hadithi hii inasimuliwa na Sebu,Msimulizi akiwa mkewe pamoja na
rakiye Kazu aliyekuwa na mkewe pia,walikuwa kwenye Hoteli
Rombeko. Maraki hawa walikuwa na mazoea ya kukutana kila
mara walipopata wakati,kwa lengo la kubadilisha mazingira
Kutokana na mazungumzo yao,ni bayana kuwa maraki hawa ni
watani.Utani wao unawajumuisha wote wanne bila kuudhika huku
wakijihusisha jamii zao.
82.
Siku hiyo walizungumzia kuhusu uchawi.Vicheko vyao vilidhihirisha
uhusiano mwema,hali hii inaonyesha mlahaka uliokuwepo baina
wane hao.
Mazungumzo yalibadilika pale msimulizi alirejelea maisha yake ya
awali ambapo alikuwa na kumbukizi ya raki yake wa utotoni kwa
jina Bogoa.Msimulizi anasema kuwa yeye Bogoa waliyafanya
mengi ya utotoni lakini walitengana baada ya kuhitimu miaka 19
mwaka wa1966.
Kazu anazungumzia kuhusu Bogoa aliyetoka sehemu za
mate.Anaelezea kuwa Bogoa alijifuza usonari na alikuwa
akikifahamu kitinya kama lugha Yake mwenyewe.Inasadifu kuwa
Bogoa wanaye mzungumzia ni yuyo huyo mmoja.
Hofu ya Sebu ilikuwa uwezekano wa Bogoa kukubali mwaliko kwa
sababu anavyotueleza msimulizi ni kuwa aliipuuza nchi yake na
hata kuwasahau wazazi wake.
Miradi yao ilikuwa wakutane club Pogopogo,kwa watu wa kupata
cha chini.Bogoa alimtambulisha mkewe Sakina kwa raki yake
Sebu naye akamtambulisha Bogoa kwa mkewe Tunu.
Bogoa anaturejesha katika maisha yake kwa uc hungu
mwingi.Ilikuwa ni hadithi ambayo hakuwa amemsimulia yeyote
hata mkewe.Anayakumbuka maisha aliyoyapitia kwa mlezi
wake.Alinyimwa hata uhuru wa kucheza na badala yake akafanya
ngumu.
Wazazi wa Bogoa wanaonyesha hali ya kutoajibika majukumu yao
kama wazazi.Hawakuwa na wakati na mtoto wao hata baada ya
kumuachia mle hawakufaidia maisha yake .Bogoa anabaki kuwa
na kisasi kuwa na kisasi na wakazi wake.
DHAMIRA
Mwandishi anawakashifu wazazi ambao hawayatekelezi
majukumu yao ya uzazi.Wengi wa wazazi wanawaachia walezi
majukumu yote bila kujali hisia za watoto wao.
83.
Bogoa utotoni anayapitia maisha magumu na hakuwa na
wakumwelezea madhila aliyoyapitiaila ila tu aliangalia ndani kwa
ndani.Hali hii inapalilia kisasi dhidi ya wazazi wake.
MAUDHUI.
1. Ulezi
Jukumu la kila mzazi ni kumlea mtoto kwa njia ifaayo na
kuyatekeleza mahitaji ya huyo mtoto.Jambo la msingi ni
kumwelimisha na kumpatia mashauri.
Wazazi wa Bogoa waliyakwepa majukumu yao na kumtwika
mlezi ambaye alimdhulumu mwanao.Malezi hayo yanamfanya
Bogoa kulipiza kisasi dhidi ya wazazi wake hata wanapoaga
dunia hakuhudhuria mazishi yao..
2. Ukatili
Sinai alimtendea ukatili Bogoa kwa kumnyima fursa ya kucheza na
wenzake.Fauka ya hayo alimpiga pindi tu alipochelewa
kurudi.Babake Bogoa aliutenda unyama kwa kumpeleka
mwanawe kwa mlezi bila kufuatilia maisha yake yalivyokuwa
kwa mfadhili wake.
3. Elimu
Elimu ni mwanga kwa kila mja.Njia moja ya kuelimika ni kwa
kupelekwa shule.Hata hivyo kuna elimu inayopitishwa na
wanamrika(peer);mfano:Sebu alimfunza Bogoa kusoma mpaka
akaweza kusoma hadithi nzima.Kulikuwa na mtazamo hasi
kuhusu watoto wa kimaskini ambao ilisemekana kuwa hawastahili
kusoma shuleni.Mtoto ambaye hakwenda shule alidhaniwa kuwa
mtoro.
4. Umaskini
Sababu kuu ya umaskini kulingana na mwandishi ni idadi kubwa ya
watoto.Wazazi wa Bogoa walikuwa na watoto takribani kumi na
sababu ya kumpeleka Bogoa kwa mlezi ilikuwa ni kutowamudu.
Ishara ya umaskini inadhihirishwa na vazi alilovalia msimulizi
a n a s e m a . ” K i l i k u wa n i k i v a z i p e k e e c h a m t u n g i n i
kwangu”.Hawakuwa na fedha hata za kununulia viatu.Vile vile
hakuwa na pesa za kulipia nauli ndiyo maana walitembea kutwa
hadi jijini.
84.
1. Uraki
Uraki wa maraki haya ni wa dhati.Maraki hawa walikuwa
wanakutana si mara moja kwani anasema kuwa …….`tulipenda
kuja seka kubadilisha mazingira na kuonana na maraki
z e t u . ” … ( U K 1 0 4 ) . K w a k u w a w a l i k u w a m a r a  k i
wakubwa,waliwahusisha wake zao.Ni kutokana na mojawapo wa
mikutano yao. Kazu anapomtaja Bogoa. Kutajiwa Bogoa kunaleta
kumbukumbu katika mawazo ya Sebu.Anamkumbuka raki yake
wa utotoni.Kutokana na mjadala ule ndipo wanapokutana tena.
Maudhui mengine:
1. Ukandamizaji wa watoto
2. Uchawi
3. Bidii
4. Uwajibikaji
5. Uhuru wa watoto
6. Nafasi ya wazazi katika malezi.
WAHUSIKA.
a) SEBU
Huyu ndiye msimulizi, jina lake halisi tunalitambua kutoka kwa
wahusika wengi kama Kazu na Mkewe.
a) Mtani
Sebu pamoja na rakiye wanataniana kwa kiwango kikubwa bila
kuudhika .Ni watani wa muda mrefu kwa sababu wanataniana
kuhusu jamii zao.
b) Ana mlahaka mzuri
Kutokana na mazungumzo yao tunaelewa kuwa uhusiano wao ni
mzuri.Anatueleza kuwa huwa wanakutana pindi wanapopata
upenyo .Hali hii ndiyo iliyomfanya kuwa na uhusiano mwema.
c) Mwaminifu
Bogoa alimwaamini tangu wakiwa watoto.
85.
a) BOGOA.
Raki wa utotoni wa msimulizi.
Sifa:
Msiri;
Hakumwelezea Sebu shida alizokuwa akizipitia kwa mlezi
wake.Hakuwaelezea wazazi wake madhila aliyokuwa
akiyapitia.Wanafunzi wenzake hawakujua asili yake kwa maana
hakuwaelezea walibaki tu kukisia.(UK 116)
Mvumilivu;
Aliyavumilia mateso kutoka kwa mlezi wake.Katika umri wake
mdogo alifanyishwa kazi nyingi zilizopita umri huo.Kama
anavyoeleza ni kuwa angechelewa,alitafutwa na kupigwa vibaya
sana..(UK 116).
Mwenye Bidii;
Licha ya kupitia madhila hayo,Bogoa alikuwa mwenye
bidii.Alijifunza kazi ya usonara na kuajiriwa.
Ameajibika;
Aliwajibikia jamii yake na ndoa yake ilikuwa imesimama imara,
zaidi ya hayo ni kuwa watoto wake walikuwa wamekomaa.
Mwenye Kisasi;
Alikasirika kiasi cha kutorudi kwao tena,Hata mazishi ya wazazi
wake hakuhudhuria.Alikuwa na kisasi na wazazi wake.
MATUMIZI YA LUGHA
a) Tashbihi
Tamathali ya usemi ambayo msanii huvilinganisha vitu viwili au
zaidi kwa kutumia maneno ya kulinganisha kama vile:Mithili
ya,sawa na,ja,na mfano wa:
· Kubadilika mara moja kama uso wa mtoto mchanga(UK
109)
· Kumtoka kama maji yanavyotiririka bombani.
86.
a) Uhuishi
Uhuishi/Tashihisi/Uhaishaji ni tamathali ya usemi ambayo msanii
huvipatia vitu visivyokuwa na uhai sifa walizonazo binadamu na
kutenda kana kwamba vina uhai.
a) Vicheko vilivyovuma na kuparamia kuta.(UK 107).Vicheko
vinapatiwa sifa ya binadamu ya kuparamia kuta.
b) Kuikimbiza furaha na kuileta huzuni(UK 109)
c) Ukweli wenye makali yanayochinja bila huruma (UK 117)
b) Nidaa
Ni msemo unaoonyesha kushangazwa na jambo Fulani na
huambatana na alama ya mshangao.
a) …….na kuwatema watu hao huko magharibi!(UK 105)
b) ……mimi ni binadamu mwenzako!(UK 105)
c) …..hatukupata hata fununu ya kuwepo kwake(UK 110)
c) Maswali ya balagha
Haya ni maswali yanayoulizwa na msimulizi au mhusika na
hayahitaji majibu ya moja kwa moja.
a) …..huoni kwamba unaniumiza?(UK 105)
b) …..uchawi si sayansi?(UK 106)
c) ……kabadilika vipi? (UK 111)
d) Semi
Haya ni mafungu ya maneno ambayo yanapotumika,hutoa maana
nyingine badala ya ile ya maneno yaliyotumika.Hutumika ili
kuipamba lugha .Kuna:
NAHAU
Huu ni usemi unaotumia maneno ya kawaida kwa lengo la
k u l e t a m a a n a i l i y o t o f a u t i n a m a n e n o h a y o
yaliyotumiwa.Tofauti na msemo huwa na vitenzi.
a) Napiga funda (UK 106)
b) Kupiga funda (UK 114)
87.
MISEMO
Hizi ni semi fupi fupi zinazotumiwa mara kwa mara kwa
lengo la kuleta maana maalum.Mfano;
Pua na mdomo(UK 108)
11.MWALIMU MSTAAFU
Dumu Kayanda ni mwandishi chipukizi mwenye uwezo wa kubuni
hadithi ilio na upeo usiokadirika. Amekuwa mwalimu wa somo la
Fasihi kwa muda katika shule mbalimbali.
Mwalimu Mesi ndiye mhusika mkuu katika hadithi hili. Anwani hii
inafaa kwa sababu hadithi inaelezea kuhusu maisha ya Mwalimu
Mesi Kabla na baada ya kustaafu.
Kutokana na kuwajibika kama mwalimu,Mwalimu Mesi alipewa sifa
chungu nzima. Aliweza ‘kuwanyanga’ wanafunzi wake mpaka
hatimaye wakawa watu wa kutajika. Wengine wakawa
mawaziri,wabunge,marubani,wahandisi,madaktari na wengine
wahasibu.
Siku ya sherehe ya kumuaga shuleni,wazazi wa wanafunzi wa
zamani na wampya walihudhuria na kumletea zawadi za aina
tofauti tofauti. Hotuba zilizotolewa zilisheheni sifa isipokuwa
hotuba ya Jairo iliyokuwa ya kumlaumu tu Mwalimu Mesi.Jairo
alikuwa zuzu hata darasani , anamlaumu mwalimua eti
alimpotezea muda wake na ndio kwa sababu yeye ni maskini.
Mwalimu anampa Jairo zawadi zote lakini Jairo hana shukrani.
Anakiona hicho kitendo cha kupewa zawadi kama kuaibishwa na
Mwalimu. Jairo anawaleta mke na watoto wake kwa mwalimu
kama zawadi. Mke wa Jairo alipewa nyumba kwenye kichumba
cha mwalimu na akakaa na watoto wake.
Jairo hakuwapitia kwa Mwalimu Mesi kuwaona jamaa yake hadi
siku alipokiwa na tetesi kuwa mwalimu amemwoa bintiye. Kumbe
ilisadifu kuwa mwalimu na kile kisichana walipoandamana kwenda
kununua kitabu mjini, mwalimu akawa mgonjwa na Yule msichana
akapelekwa shule ya bweni. Ilikua ni sababu tosha ya wenye
umbeya kueneza uvumi kwa mwalimu na bintiye Jairo.
Hawakuonekana na ni kwa sababu wameanza kuandika kurasa
mpya za maisha yao pamoja.
88.
Anwani.
Anwani hii MWALIMU MKUU inafaa kwa sababu hadithi mzima
inazungumza kuhusu maisha ya Mwalimu mstaafu Mesi .
Dhamira
1.Mwandishi alikusudia kuonyesha umuhimu wa kuwajibika kazini
kama alivyowajibika Mwalimu na mazao ya kazi yake
yanaonekana.
2.Mwandishi pia anadhamiria kuonyesha tofauti ya watu wa elimu
maishani. Kuna tofauti ya watu waliosoma na wale ambao ni zuzu
kama Jairo.
WAHUSIKA
Mwalimu Mesi
1.Amewajibika
Kutokana na kule kuwajibika, anapewa sifa chungu nzima .
Wanafunzi wanaishia kuwa madaktari,, mawaziri, marubani n.k.
Wengi wanahudhuria sherehe yake ya kumuaga na kumletea
zawadi nyingi kama ishara ya shukrani.
2.Karimu
Anampa Jairo zawadi Zote alizoletewa katika sherehe ya
kumuaga.
Anakubali mke na watoto wa Jairo waishi kwake.
Kisichana cha Jairo kilipofukuzwa shuleni kwa kukosa kitabu,
waliandamana hadi mjini kukinunulia kitabu.
3. Mwenye utu/ubinadamu
Anaamini watu wote ni sawa, hakuna mtu nusu mtu. Anasisitiza watu
ambao hawakuja kwa magari mazito pia wapewe nafasi ya kutoa
hotuba walivyopewa wengine wa tabaka la juu. Jairo anapotoa
hotuba yake, alimlaumu tu Mwalimu lakini hilo halikumkera
Mwalimu.Anampa Jairo zawadi zote , anaamini jairo alizihitaji
zaidi.
89.
4.Mwenye sifa tele
Uk 120…Wanafunzi wake wote hao hawamsahau kwa nasaha
zake, kwa insafu yake, kwa huruma yake, kwa hekima yake,kwa
ustaarabu wake,kwa uadilifu wake ,kwa uwajibikaji wake, kwa
nemsi yake,kwa ucheshi wake.
Hotuba zao zilijaa sifa tele.
JAIRO
Alikua mwanafunzi wa Mwalimu msaafu ambaye mambo
hayakumwendea vizuri.
1.Mwenye Kulaumu
Jairo alikuwa mmoja wa wanafunzi wa Mwalimu Mstaafu. Yeye ni
tofauti na wengine wengi, aliishia kuwa mtu ovyo . Hali yake ya
umaskini inamfanya amlaumu Mwalimu eti alipotezea wakati kwa
kumueka darasani na kumpa tumaini za uongo.
2.Zuzu
Hata baada ya kuwa shuleni kwa miaka yote ile hakuweza kuunga
moja na moja. Pia alipata sufuri masomoni.
3.Mcheshi
i)Haelewi kwa nini Mwalimu alimshauri asilewe ilhali anaamini
tembo inampa raha ya kuishii. Alisema kuwa alipolewa hata
akitembea bila viatu na kujikwaa au kudungwa na miiba, hakuhisi
kitu.
ii)Hakuelewa pia kwa nini kuepukana na ulevi, kusubiri hadi ndoa
ndipo ‘kuchana ngazi.’
iii)Anapeleka mkewe na wanawe kwa Mwalimu na kumpa kama
zawadi.
MKE WA MWALIMU
1.Mwenye utu
Anakubali mke wa Jairo na wanawe waishi kwao. Anamtunza kama
bintiye. Anamwambia , “Hapa paite nyumbani. Upaone hapa
kwenu kama si nyumbani pako. Ukae upumzike. Ukae uone raha ya
kuishi.”
90.
2.Mwenye bidii/Anauhusiano mzuri na watu
Wanaandamana na mke Wa Jairo kwenda kondeni kupanda
mbegu, kupalilia, kumwagia mazao kondeni mbolea. Pia walienda
k u t e k a m a j i n a k u t a f t a k u n i . Wa l i c h u m a k u n d e n a
mchacha,mabenda kondeni wakiziambua na kuzikata mboga hizo
pamoja pale uani.
MKE WA JAIRO
1.Mvumilivu
Mwandishi anaeleza maisha ambayo mkewe Jairo ameyapitia.
“Katika maisha yake na Jairo, ameonja ladha zote za dhiki, thakili,
bughudha na kero. Hakuna mwanamke anayejua kumezamate
machungu kama Mke wa Jairo.”
2.Mtiifu
Anapopelekwa kwa Mwalimu kama zawadi, Mwalimua
anamshauri arudi kwake lakini anakataa. Anasema “sharti ni mtii
mume wangu. Mume ni mume hata akiwa gumegume.” Mwalimu
aliposisitiza, mke wa Jairo alimweleza kuwa hawezi kwenda
kinyume na amri ya Jairo mume wake.
3.Mwenye bidii
Waliandamana na mke wa Mwalimu kondeni kupanda, kupalilia,
kuteka maji vijitoni na kutafta kunikuni.
WANAFUNZI NA WAZAZI
1.Ni wenye shukrani
Wanaka katika sherehe ya kumuaga Mwalimu kwa wingi wakiwa
na zawadi chungu nzima.
2.Karimu
Wanamletea Mwalimu zawadi chungu nzima.Wanaendesha
magari makubwa na ni waadilifu kwa sababu walifuata ushauri wa
walimu wao. Wale ambao hawakupata elimu wameishia kuwa
maskini , walevi ambao hawana mbele wala nyuma. Pia hawana
maadili mema.
91.
3.Uzuzu/Ujinga
Hata baada ya kuhudhuria shule ya msingi, Jairo hawezi kuunga
moja na moja. Haoni umuhimu wa elimu. Anamlaumu Mwalimu Mesi
eti alimpotezea muda wake bure shuleni kwa kumwambia kila
uchao kwamba ataimarika na hakuwahi imarika. Anamlaumu
Mwalimu kwa kumshauri asinywe tembo ilhali anaamini hiyo tembo
ndio humpa raha ya kuishi. Anaamini kinyume cha nasaha za
Mwalimu ndio utamu na uhondo wa maisha. Uzuzu unamfanya
awapeleke mke na watoto wake kwa Mwalimu kama zawadi.
Anaona soni kupokea zawadi kutoka kwa Mwalimu. Haelewi
mbona akapewa zile zawadi ilhali alizihitaji zaidi.
MAUDHUI
Kuwajibika
Hii inadhihirika zaidi siku ya sherehe za kumuaga Mwalimu Mesi
pale shuleni.
Waliohudhuria sherehe hii walikua wengi mno. Mwandishi asema
“walika kwenye kiambo cha shule kama mashabiki wa mchuano
wa soka wa kuwania kombe la dunia kutokana na kazi nzuri ya
Mwalimu, wanafunzi wake waliishia kuwa madaktari, wabunge n.k.
Hotuba zilizotolewa zilisheheni sifa kwa Mwalimi Mesi.
Elimu
Mwandishi anatuonyesha umuhimu wa Elimu.watu waliomakinika
k a t i k a e l i m u h a t i m a y e w a l i k u w a ‘ w a t u ‘ , w a k a w a
mawaziri,wabunge, marubunu n.k. Wakawa pia wanaendesha
magari ya nguvu. Elimu unawafanya watu kuwa watu wa maana
,watu bora kwa hadafu. Lakini wale ambao hawakumakinika,
hutumia yao duni, maisha ya umaskini. Pia wana mitazamo hasi
kuhusu maisha.
Utabaka
Utabaka unasababishwa na kupata au kukosa elimu. Waliosoma
na kufaulu katika elimu, wanaishi kama ‘watu’. Wanapata kazi
nzuri, zinzwapa mshahara.
92.
Ukarimu
ukarimu unajitokeza wakati Mwalimu Mesi anampa Jairo zawadi
zake zote, anasema “mimi nimeamua kwa hiari yangu kukupa
wewe zawadi hizi.”
Mwalimu na mkewe (Bi Sera) ni karimu,wanawakaribisha mke na
watoto wa Jairo kwao.
MBINU ZA LUGHA
Kuorodhesha
Mwandishi anatumia mbinu ya kuorodhesha mfano;
Uk 120: Wanafunzi waje wote hao wanafunzi wake hawamsahau
kwa nasaha zake,kwa insafu yake, kwa huruma zake ,kwa hekima
zake, kwa ustaarabu wake, kwa uadilifu wake…
Uk 121:Wanafunzi wake waliokuwa bado wanasoma kwenye shule
hiyo waliimba tele, nyimmbo za jamii mvbalimbali, wakacheza
zeze,mariamba, lelemama, mdundiko, violoni.
Uk 122:…sikwambii haya madude makubwa waliokuja kututisha
nayo akina Bariki,Festo, Mshamba ,Nangeto na hali kadhalika.
Tabaini
Uk 124:Si matoroli,si vijiko vikubwa vya kuzola mchanga,si
makubadhi ,si meza na samani aina aina, si fedha
Uk 124:Si matoroli,si vijiko vikubwa vya kuzolea mchanga,si
makubadhi,si meza na samani aina aina,si fedha.
Takriri/Uradidi
Uk 126:Wanafunzi wako wote hao wanafunzi wake.
Uk 128:Jairo aliambiwa , akaambiwa na kuambiwa na wajuao.
Tashbihi
Uk 120:…mvi zimemkaa kwa haiba kama theluji kwenye mlima
Kilimanjaro.
Uk 121:…walifurika kwenye kiambo cha shule kama mashabiki
wa mchuano.
93.
Uk 122:Kichwa chake chenye upana killing’aa utosini kama sufuria
kwenye duka la Buniani.
Uk 125:…wakapokeza hotuba hio kama huizi kutoka kizazi kimoja
hadi kingine.
Uk 129:…kimenawiri kama ua linalotimbuka kudamu.
Uk 129:Aliona madodo yamesimama kifuani kama kanzi mbili za
mwanamasumbwi.
Uk 129:…kiuno kimechukua umbo mduara kama cha nyigu.
Tashhisi
Uk 120:Alijaaliwa mvi nyeupe zilizojianika kwenye kichwa chake
kidogo.
Methali
Uk 121: Anayo maneno ya kuweza kumtoa nyoka pangoni.
Uk 123: : Kuwashia pofu taa si kuharibu mafuta.
Uk 128:Alikuwa ametuma jongoo na mti wake.
Jazanda
Matumizi ya maneno yenye maana che.
Uk 121:…wenzao hao waliokuwa wamekua watu.
Uk 121:…lakini nadhani ni jambo la busara kutotia mchanga
kitumbua.
Uk 129:Walitafuta kitabu cha maisha na kuanza kuandika kurasa
mpya za maisha yao pamoja.
Uk 124:…kusubiri hadi ndio ndipo kuchuna ngozi.
Kinaya
Kinyume cha matarajio
Uk 123: Ni kinaya kwa Jairo hakuona sifa nzuri ya Mwalimu Mesi.
Yeye anamuona kama kikwazo kikubwa kwake. Kama yeye Jairo
anaishi maisha duni kwa sababu ya Mwalimu Mesi.
Uk 126:Ni kinaya Mwalimu Mesi kumpongeza Jairo kwa hotuba
yake kumhusu ambayo ilijaa kumlaumu Mwalimu kisha Mwalimu
Mesi anamueleza akifa mwanzo azungumze siku ya mazishi yake.
Uk 126:Ni kinaya Jairo anapopeleka mke wake na watoto kwa
Mwalimu Mesi kama zawadi.
Uk 127:Ni kinaya kwa mkewe Mwalimu Mesi (Bi Sera)kumkaribisha
mke na watoto wa Jairo kwao “Mwachie akae huyu binti na watoto
wake, tutawatunza.”
94.
Msemo
Uk 121:Wanafunzi wake wa zamani waliopewa kisogo na dunia
Uk 126:Hakuna mwanamke anayejua kumeza mate machungu.
Mdokezo/Kauli isiyokamilika
uk 120:kisa na maana ni huyo Mwalimu Mesi.
uk 123:kwamba kuwashia pofu taa si kuharibu mafuta.
UK 125:…umefanya makosa makubwa sana.
Uk 125:…hamna mwendawazimu wala mahaka kati yetu.
Uk 126: “Badala ya ngojera nyingi za huyo anayemwita si siri au
siri sijui.
Sadfa(matukio mawili yanayotokea kwa pamoja).
Inasadifu kuwa baada ya Mwalimu kuondoka na kile kisichana
kununua kitabu hakuonekana tena. Watu wakakiri eti Mwalimu
alikua amekioa kile kisichana. Kumbe wakati huu Mwalimu alikua
akiugua na alikua ndani(nyumbani) wakati wote huo na ndio
sababu hakuonekana.
Maswali
1.Onyesha umihimu wa wahusika wafuatao katika hadithi ya
Mwalimu Mtaafu.
i)Mwalimu Mesi
ii)Jairo
iii)Mkewe Jairo
iv)Wanakijiji
(al 20)
2.Fafanua maudhui yoyote manne katika hadithi hii. (al 20)
Ukarimu
Mwalimu Mstaafu ni mkarimu. Hii inadhihirika anapopokea zawadi
kutoka kwa wazazi na wanafunzi na kumpa Jairo zote.
Pia Mwalimu na mke wake ni wakarimu kwa mke wa Jairo na watoto
wake. Waliwapa nyumba akae na watoto wake. Waliwachukua
kama binti yao. Bintiye Jairo alipofukuzwa shuleni kwa kukosa
kitabu, Mwalimu Mstaafu alimnunulia.
95.
Utabaka
Utabaka umesababishwa na kupata au kukosa elimu. Waliopata
elimu walipata kazi nzuri kama za uwaziri ,ubunge, udaktari, urubani
n.k. kazi zilizo na mshahara mzuri. Wakawa wanaishi maisha mazuri
na kuendesha magari ya nguvu. Wale nao ambao walikosa elimu,
waliishi kuwa maskini na walevi.
Kuwajibika
Hii inadhihirika zaidi siku ya sherehe za kumuaga Mwalimu Mesi.
Kutokana na kuwajibika kwake kama Mwalimu,wanafunzi wake
wa n a f a u l u m a i s h a n i . Wa n a p a t a k a z i n z u r i k a m a z a
udaktari,ubunge,uwaziri n.k. Hii ndio sababu walikuja kwa wingi
kumshukuru Mwalimu Mesi. Hotuba zao pia zilijaa sifa tele.
Bidii
1.Mwalimu anajibidiisha katika kuwafunza na kuwashauri wanafunzi
wake.
2.Wanafunzi walifanya bidii na kufaulu mitihani yao.
3.Mkewe Mwalimu na mkewe Jairo wana bidii pale kondeni wanapo
panda mbegu,wanapalilia,wanateka maji.
12.MTIHANI WA MAISHA
Eunice Kumaliro ni mzaliwa wa Kenya. Mshauri na mtaalam wa elimu
aliyeandika vitabu kadhaa.
Muhtasari
Je,Samueli alikuwa amepita mtihani wake wa Elimu? Kuanguka
mtihani wa elimu ni kuanguka pia mtihani wa maisha?
Samueli ambaye ni mhusika mkuu katika hadithi anaenda shuleni
kuchukua matokeo yake ya mtihani. Akiwa pale foleni nafanya moyo
wake kwa kuwa alikuwa na uhakika kuwa alikuwa amepita mtihani
wake vizuri.
Kule ndani ya osi , Mwalimu Mkuu ameketi pale na anapuuza
kuwepo kwake osini humo. Hatimaye anamtupia Samueli stakabadhi
ya matokeo yake.
Samueli anapotambua alivyokuwa amefeli mtihani wake,
anamdanganya babake kuwa hakupata matokeo yake kwa dai ya
kutokamilisha kulipa karo ya shule.
Samueli haoni haja ya kuishi tena. Anakata kauli kujitosa majini afe.
Hakuwa tayari kupata aibu kutokana na matokeo yake mabaya.
96.
Mamake Samueli ana matumaini kuwa kuanguka mtihani wa elimu
si kuanguka mtihani wa maisha. Anamshika Samueli mkono na
wanaelekea nyumbani.
Anwani
Anwani ya hadithi hii, MTIHANI WA MAISHA inaoana na yale
yaliyomo. Kupitia kwa mamake Samueli, mwandishi anaonyesha
kuwa kuna maisha hata baada kuanguka mtihani wa elimu.
Kuanguka mtihani wa elimu sio kuanguka mtihani wa maisha.
Dhamira
Mwandishi alikusudia kuonyesha;
1.Kuanguka mtihani wa elimu sio mwisho wa maisha. Bado kuna
matumaini.
2.Umuhimu wa kumakinika katika masomo kwani athari za
kuanguka mtihani ni hasi.
MAUDHUI
Ukatili
Samueli analinganisha babake na hayawani ambaye anaweza
kumrarua mtu na kumla mzimamzima. Samueli alipofeli mtihani
wake, anavunjika moyo na kuona maana ya kuishi. Anakata kauli
ya kujiangamiza kwa kujitosa majini. Babake hata baada ya
kumuona mwanawe katika hali ya kuvunjika moyo, hakumhurumia,
badala yake anaamrisha watu wamuache ajitose majini afe. Pia
anampa kamba atumie kujitia kitanzi.
Ucheshi
Samueli ni mcheshi. Anachekesha anaposema udongo uliowaumba
babake na mamake ni tofauti na ndio sababu mama angeweza
kuelewa kidogo atakapojua amefeli mtihani lakini baba hawezi.
Anapomwangalia Mwalimu Mkuu, anamwona ni kama aliyezidiwa
na maumivu au anayepaswa kufanyiwa oparesheni ya ubongo na
anayehitaji maombi.
Anapoamka kuchukua hatua ya kujiangamiza ,anatazama juu
kumpasha Muumba wake ujumbe kuwa alikuwa njiani akielekea
mbinguni. “Naja huko juu mbinguni mapena kidogo Baba.
Nitengee nafasi. Nimeruka foleni…”
97.
Nafasi ya Mwanamke
Mwanamke anapuuzwa katika jamii hii. Inathibitishwa na mtazamo
wa baba kupitia elimu. Ingawa baba aliyaonea fahari mafanikio
ya binti zake, aliwaona kama wanawake tu. Fahari yake ya dhati
ilikuwa katika kumwona mwanawe wa kiume akifua dafu. Samueli
haamini vipi angeweza kushindwa katika mtihani na dada zake
ilhali ni wanawake.
Mwanamke kupitia kwa mhusika mama amechorwa kama aliye na
utu na matumaini. Anamshika Samueli mkono na kumwambia
waende nyumbani na kumweleza maneno ya kumpa tumaini. Pia
anapenda amani na ni mshauri mwema. Anamshauri mumewe
aende shuleni wasuluhishe sintofahamu kuhusu karo.
Kufa moyo/kuvunjika moyo
Samueli alipoanguka mtihani hakuona haja ya kuendelea kuishi na
anaamua kujitosa majini afe. Anasema, “Acha nijiondokee duniani
niwaachie wafanisi wafanikiwe.” Katika ujumbe wake na Muumba
anasema itabidi aende mbinguni kwa sababu stahamala
zimekwisha.
Elimu
Elimu ni muhimu maishani. Wasichana katika jamii hii wanafanya
vizuri kuliko wavulana. Wavulana wanamchezo shuleni (Mahoka)
unaochangia kuanguka kwao. Hakuna anayepewa matokeo yake
ya mtihani kabla ya kumaliza kulipa karo. Athari za kuanguka
mtihani ni kama vile aibu na hata kujiangamiza.
WAHUSIKA
SAMUELI
Ndiye mhusika mkuu
Mcheshi
1.Anaposema, “labda Mwalimu mkuu kazidiwa na maumivu. Labda
anapaswa kufanyiwa operesheni ya ubongo ama anahitaji
maombi hasa atakuwa na akili razini tena.”
2.Samueli anasema kuwa mamake na babake wameumbwa kwa
aina tofauti kabisa ya udongo.
3.Anamuarifu Muumba kuwa yumo njiani akienda mbinguni basi
atengewe nafasi kwani ameamua kuruka foleni.
98.
Mwenye Matapo
Anaposema yeye hana moyo wa bua. Kile asomacho ndicho kijacho
kwenye mtihani. Anaelewa kuwa yeye si mwerevu sana laikini
anajua kupanga mikakati na pia anaamini ana bahati ya mtende
anaamini kuwa amepita mtihani wake vyema na kuwa motokeo
yake yangemshtua Mwalimu mkuu ambaye hakuwa na imani naye.
Mwongo
(uk 137) Samueli anamdanganya babake kuwa hakupata matokeo
yake kwa sababu hakuwa amemaliza kulipa karo.
Mwoga
Uk 133: Anaogopa anapoingia katika osi ya Mwalimu mkuu.
Woga unajitokeza kutokana na anavyozungumza/anasitasita.
“Mwa…limu nimekuja kuchu…chukua matokeo…” “samaha…ni.
Waa…zazi wangu.” Samuel anatetemeka anapomwona babake
pale kwenye bwawa(uk 132)
Mwenye machoka
(uk 134)ni kutokana na tabia hiyo pale shuleni ndipo akapewa jina
‘Rasta’
Kufa moyo/kuvunjika moyo
Kuanguka mtihani kwa Samwueli si jambo alilokuwa akitarajia.
Alikuwa ana uhakika kuwa amepita mtihani wake.Jambo hili
ameliona kama la kumletea aibu mbele ya wazazi wake,
alivyopendekeza Samueli.
Anakata kauli kujitosa majini afe. Hakuna maana ya kuuendelea
kuishi. Anasema “Acha nijiondokee duniani niwaachie wafanisi
wafanikiwe anamwambia Mungu kuwa amekosa stahamala.”
MAMAKE SAMUELI
Mwenye utu
Mamake Samuel anaka kwenye bwawa la maji alipokuwa
amejitosa Samuel, anamshika Samuel mkono na kumwomba
waende nyumbani. Anamwambia Samuel maneno ya kumpa moyo,
“huwezi kushindwa na mtihani wa shule na vilevile kushindwa na
mtihani mwisho.
99.
Mwenye Matumaini
Hata kana kwamba Samuel ameanguka mtihani wa shule, mamake
Samuel anaamini kuwa kuna matumaini hata baada ya kuanguka
mtihani huo. Anaamini Samuel hajaanguka mtihani wa mwisho.
Anaamini pia kuwa Mungu hamkoseshi mja wake yote. (UK 139)
Mwenye Kuelewa Mambo
Samuel anasema kuwa kweli amemusaliti mamake kwa kuanguka
mtihani lakini mamake tofauti na babake, ataelewa.
Mpenda Amani
Samuel anapomdanganya babake kuwa hakupata matokeo ya
mtihani wake ati kwasababu hajamaliza kulipa karo, anakereka.
Mamake Samuel anaingilia kwa upole na kumshauri mume wake
amuone Mwalimu mkuu ili wasuluishe suitofahamu hiyo.
BABA SAMUEL
Katili
Samueli anamlinganisha babake na hayawani ambaye anaweza
kumrarua mtu na kumla mzimamzima.
Baada ya Samueli kuanguka mtihani alikuwa na kipindi kigumu na
anaamua kujiangamiza. Babake hakuwa na huruma naye hajali
kama atajitosa maji afe. Anasema “mnamzuia kwa nini? Mwachie
ajitose majini kama anataka. Ana faida gani huyo? Sikuzaa
mwana nilitoa tu maradhi tumboni.” Uk 139 Anampa Samueli
kamba aitumie kujiangamiza.
Mwenye moyo mgumu
Babake Samueli ana moyo usiojua kusamehe. Anaamrisha watu
wamuache ajitose majini afe. Anampa Samueli kamba ajitie
kitanzi ikiwa anaogopa kujitosa majini. Samueli anasema kuwa
mamake ataelewa atakapojua kuwa Samueli amefeli mtihani.
Lakini babake aliyeumbwa na udongo tofauti hawezi.
Amewajibika
Aliweza kulipa karo yote ya shule.
100.
MWALIMU MKUU
Mwenye madharau
Samueli alipoingia katika osi yake,anachukuwa muda mrefu sana
kuinua uso wake kumuangalia Samueli. Baada ya kuzichambua zile
stakabadhi za matokeo, anatoa moja na kumtupia Samueli.
Anamtupia kwa mtu anavyomtupia mbwa mfupa.
Amemakinika kazini
Hakuamini Samueli alipomwelezea kuwa amekamilisha kulipa
karo, alitumia “daftari la karo” kuhakikisha. Anasema mali bila ya
daftari hupotea bila ya habari. Ndio maana ameweka daftari la
kuweka kumbukumbu ya wanaodaiwa karo na waliolipa karo.
MBINU ZA UANDISHI
Tashbihi
Uk 131:waliokuwepo waliotoka wamenywea kama kuku walionoa
maji ya mvua.
Uk 132:akitoka ndani atakuwa akitembea kama fahali.
Uk 131:amamtupia kama mbwa anavyomtupia mbwa mfupa.
Uk 137:anamuona baba akilini kama hayawani.
Uk 135:imekwenda kama chendacho kwa mganga kisichokuwa na
marejeo.
Tashhisi/uhaishaji/uhuishi(personication)
Hii ni mbinu ya kupatia kitu kisicho hai sifa za kiumbe mwenye
uhai(sifa za kibinadamu).
Uk 134:Nzi wa kijani ya samawati waliokula wakashiba.
Linampokea kwa vilio nao mnuko kwa kughasi unampokea kwa
vigemo.
Uk 135: Safu sa ya D na E ilimkodolea macho bila kupesapesa.
Uk 137:Ilimuradi mawazo yana mwadhibu sasa.
Uk 138:Alitupia jicho safu ya maji akaona yanasumbuka na
kuhangaika.
101.
Msemo
Uk 132:Uso wake wenye makunyanzi ulipiga mapeto.
Uk 133:Anakitazama kidole cha Mwalimu mkuu kupiga masafa.
Uk 135:Juhudi zake zimegonga ukuta.
Uk 137:Nina kuambulia patupu.
Uk 139:…huhu kila mtu akipigwa na kibuhuti.
Kichanganya ndimi
Kutumia zaidi ya lugha moja tofauti.
Uk 132:come on
:yes
Utohozi
Kuswahilisha maneno/kutamka maneno yasiyo ya Kiswahili kama
ya Kiswahili.
Uk 133: Bodi,operesheni.
Maswali balagha
Maswali yaliyoulizwa bila ya kutarajia majibu.
Uk 131: Mtu angesemaje ati? Wanafunzi na wakati huo huo
wanasononeka?
Uk 133: Nazo fedha ulitoa wapi mtoto pale ulipo.
Uk 135: Karo yote niliolipa iwe bure? Pesa aliyolipa baba tusome
imekwenda bure?
Uk 136: Ali umefeli mtihani ? sasa nitafanya nini?
Methali
uk 132:Mdharau biu hubiuka.
uk 132:Usione wembamba wa reli kwani gari moshi hupita juu
yake.
uk 135:Imekwenda kama kiendacho kwa mganga kisichokua na
marejeo.
uk 139: Mambo ni kuganga huenda yakaja.
102.
Uzungumzi nafsia
Mhusika hujizungumzia ama kwa kuongea au kuwaza bila
kukusudia kusikika na yeyote.
Uk 132:mimi tangu hapo najijua bwana. Sina moyo wa bua. Mtihani
haunibabaishi sana.
Uk 132:hajawai kuniamini huyo hambe. Lakini mimi mwenyewe
najiamini. Lazima mtu ajiamini… au sio?
Uk 135: Hivyo ndivyo kusema lolote wala chochote . kwamba mimi
si lolote wala chochote. Kwamba mimi si chochote wala lolote
katika medani ya masomo?
Mdokezo/usemi usiokamilika
Uk 132:tena angaa sikukutana na paka mweusi njiani siku zote za
mtihani…
Uk 133:…chukua matokeo…
Uk 135:si mjinga mimi. Najua vitu vingi tu…
Uk 136: Mama ataelewa lakini baba…
Sadfa
Matukio mawili au zaidi yanayotokea kwa pamoja bila ya
kupangwa.
Uk 135:Ilisadifu kuwa siku na wakati ambapo Samueli alitaka
kujitosa majini ili afe, siku hiyo ilikua tofauti kwani wachunga
wapitia hapo wakiwapeleka mifugo malishoni hawakuwepo. Ikawa
rahisi kuweko kujitosa majini.
Uk 138: Inasadifu pia kuwa baada ya Samueli kujitosa majini na
kupiga mikupuo kadhaa ya maji, mwanamume mmoja akawa
ameachwa na basin na akaamua kutumia njia karibu ya kamwokoa
Samueli.
Taharuki
1.Kuna wanafunzi waliotoka osini mwa Mwalimu mkuu wakiwa na
furaha na huku machozi yanawatoka. Msomaji anabaki hata hamu
ya kujua ikiwa walikuwa wamepita mtihani au la.
2.Msomaji pia angetaka kujua ikiwa Nina alimuacha Samueli
kutokana na vituko vyake au la.
3.Msomaji anabaki na hamu ya kutaka kujua maisha ya Samueli
yaliendelea vipi. Je alifaulu maishani. Baba alibadilika na
kumsamehe .
4.Kuanguka mtihani wa elimu na kuanguka mtihani wa maisha?
103.
Maswali
1.Andika sifa za wahusika hawa kama zinavyojitokeza katika
hadithi ya mtihani wa maisha.
i)Samueli
ii)Babake Samueli
iii)Mamake Samueli
iv)Mwalimu Mkuu
Jadili nafasi ya mwanamke katika hadithi ya Mtihani wa Maisha.
Mwanamke amepuuzwa katika jamii. Hii inadhibitishwa na
mtazamo wa baba kupitia elimu. Ingawa baba aliyaonea fahari
mafanikio ya binti zake,aliwaona kama wanawake tu. Fahari yake
ya dhati ilikua katika kumwona mwanawe wa kiume akifua dafu.
Samueli hakuamini vipi angeweza kushindwa katika mtihani na
dada zake ilhali ni wanawake.
Mwanamke ni mpenda amani na mshauri mwema. Anamshauri
mumewe aende shuleni wasuluhishe sintofahamu kuhusu karo
Pia ni mwenye utu.Anamshika Samueli mkono na kumwambia
waende nyumbani. Anamwambia maneno ya kumpa tumaini.
13. MKUBWA
Na Ali Mwalimu Rashid
UFAAFU WA ANWANI MKUBWA
Neno mkubwa linatokana na kivumishi ‘–kubwa’ ambalo lina maana
ya kuzidi kwa umbo au kimo; -siyo ndogo. Pia neno hili lina maana ‘-
enye kwisha kukua’ au ‘kuwa juu’.
Anwani ‘Mkubwa’ inaaki kazi hii kwani yafuatayo ni mambo yaliyo
wazi zaidi;
F Msimulizi anatueleza kuhusu mhusika mkuu kazini aliyeitwa
Mkubwa. Alikuwa anajihusisha na biashara ya kuuza pweza wa
kukaanga. Hii ndiyo biashara iliyompa kipato na faraja.
F Mkubwa alipoingia uongozini alikuwa na madaraka makubwa.
Alikuwa na uwezo uliozidi. Viongozi walipapata pasipoti za
kidiplomasia ziliwawezesha kutosachiwa bandarini wala
kwenye uwanja wa ndege.
104.
F Uovu wa Mkubwa ulikuwa umezidi. Aliweza kumwingiza raki
yake Mkumbukwa kwenye biashara ya kuuza dawa za kulevya.
Mkumbukwa aliponaswa na kutiwa ndani kwa kupatikana na
mkoba uliojaa dawa hizo alijuta mno. Majuto yake yalikuwa
makubwa.
F Ushawishi wa Mkubwa ulikuwa umezidi. Aliweza kumtoa
Mkumbukwa ndani baada ya siku tatu. Pia alipewa mzigo wake
ukiwa katika hali ile ile.
F Baada ya Mkumbukwa kutolewa ndani , aliichukia sana
biashara ya kuuza dawa. Aliapa na Mola kuwa hatofanya tena
biashara hiyo tena.
F Mkubwa alipojilaza kwenye kochi na usingizi kumchukua anaota
kuwa vijana wameongezeka mjini wanaosinzia ,wengine hali
yao imedhooka sana na wizi umewazidi mitaani.
F Mshituko wa Mkubwa ulizidi alipoona kuwa watoto wake wa
kiume walikuwa miongoni mwa vijana waliokuwa wameandikwa
kwenye nyuso zao ‘mla unga’ jambo liliomfanya chizi.
DHAMIRA YA MWANDISHI
Mwandishi amelenga kupiga vita biashara haramu ya uuzaji wa
dawa za kulevya au “kuuza unga”. Kupitia kwa Mhusika Mkubwa
tunagundua kuwa viongozi ndio walanguzi wakuu wa dawa hizi.
Viongozi wawa hawa huwatafuta vijana ambao huzipeleka dawa
hizo kwa wateja. Wanaoumia zaidi ni vijana ambao wanaponaswa
hutiwa ndani huku walanguzi halisi wakiufurahia uhuru wao nje.
WAHUSIKA
1. Mkubwa – alikuwa muuzaji wa pweza wa kukaanga kabla
ya kuingia kwenye uongozi alikoingilia biashara haramu ya
kuuza dawa za kulevya. Ana sifa zifuatazo:
a) Mwenye bidii- alikuwa akishughulisha na kazi ya kuuza
pweza wa kukaanga na baadaye akauza kipande cha ardhi
ili kuingia uongozini.
b) Mwenye utani- anamtania utingo kuwa huwa haogi jambo
lililomfanya utingo kukimia kwa kuchekwa na abiria.
c) Ni mtambuzi- aliweza kuelewa maana ya unga japo
hakuwahi tu kuona vituko vyake.
105.
a) Mwenye utu- alimpigapiga kijana mbwia unga aliyekuwa
ameinama kama kwamba anarukuu na kumuuliza iwapo
anaumwa.
b) Mwenye tamaa ya mali- alipotanabahi namna viongozi
wanavyotajirika kwa kuuza unga , maneno ‘unga na utajiri’
yalimkaa moyoni kiasi chake kukosa usingizi usiku huo.
c) Ni maskini- alikuwa akifanya biashara ya kuuza pweza
iliyokuwa na kipato kidogo . vilevile kabla ya kupata uongozi,
alikuwa na suruali na shati kipande papa
d) Ni sadi- baada ya kutia na kutoa, aliamua kufanya
biashara haramu ya kuuza dawa za kulevya biashara
ambayo huonekana kama ya kishetani. Vile vile alitoa kiasi
kikubwa cha pesa ili kuwashawishi wapiga kura kumpendelea
na ndipo akaupta ushindi.
e) Mwenye msimamo dhabiti- baada ya kuyatia moyoni
maneno aliyopewa na kijana yule kuhusu utajiri na unga
aliamua kutafuta kwa udi na uvumba na ndipo akamwendea
rakiye kwa jina Mkumbukwa.
f) Ni msiri- mwanzoni hakumweleza Mkumbukwa sababu yake
kuutafuta uongozi.
g) Mwenye wasiwasi- aliogopa kuwa huenda kisomo chake
kingemzuia kupata uongozi.
2. MKUMBUKWA – ni rakiye Mkubwa aliyejitwika jukumu la
kuwarai watu ili wampigie Mkubwa kura.
a) Raki wa dhati- Mkumbwa alimwendea kwa mawaidha
baada ya kuamua kuugombea uongozi na ndipo
Mkumbukwa akamshauri Mkubwa augombee.
b) Mkakamavu – alimweleza Mkubwa bila kupepesa macho
wala kugugumizi kuwa pesa na ukaragosi wa chama ndiyo
mambo muhimu pale Mchafukoge yatayomwezesha
kuupata uongozi.
106.
c) Mwenye kutimiza ahadi- alimwambia Mkubwa kuwa
akitafuta milioni kumi kisha ampe yeye ataupata uongozi na
kuapa kuwa iwapo ataukosa amuue.
d) Ni mwenye bidii- baada ya Mkubwa kujaza fomu; alianza
kazi ya kuingia /kupita nyumba baada ya nyumba kumtafutia
kura mkubwa.
e) Mwenye busara- alifahamu ka kuwa ili kufanya kazi vyema
ni lazima angemtafuta Bi Kibwebwe (Sada) na kumhusisha
katika harakati za kumtafutia Mkubwa kura.
a) Mwenye majuto- aliponaswa na askari wa kitengo cha
kupambana na dawa za kulevya alijuta kimoyomoyo.
b) Mwenye kulalamika- alipotiwa ndani alikuwa
akilalamika kupuuzwa kwa haki za mahabusu.
Zoezi
1. Fafanua sifa za wahusika hawa.
a) Sada
b) Vijana wabwia unga
c) Askari
1) ATHARI ZA DAWA ZA KULEVYA
F Vijana wanaolangua dawa za kulevya(unga) huishi kwa
woga huishi kwa mfano yule kijana baada ya kumrushia
Mkubwa maneno aliogopa wenyewe wasije wakamwona.
F Vijana wabwia unga(wanaotumia dawa hizi) hugeuka
karakana za matusi. Km yule kijana mbwia unga alimuuliza
Mkubwa kijeuri “kwani tunakula kwa babako? Vile vile kijana
aliyekuwa kichochoroni alimwita Mkubwa juha.
MAUDHUI
Maudhui ni mengi yaliyomo katika kazi. Haya ni masuala
yanayoangaziwa na mwandishi wa kazi husika.
Mwandishi ameangazia maudhui yafuatayo;
107.
F Vijana wanaozitumia dawa hizi hugeuka na kuwa mazuzukm
kijana mwingine aliyekuwa kichochoroni alikuwa
akitokwa na denda mdomoni huku amefumba macho.
F Vijana wabwia unga huota ndoto za kiajabu – kwa mfano
kijana aliyekuwa kichochoroni alimkasirikia Mkubwa kwa
kuwa aliikatiza ndoto yake na kumkatizia stimu. Analalamika
kuwa Mkubwa aliiangusha ndege yake (katika ndoto)
alipomshtua.
F Viongozi wanaojihusisha katika biashara hii haramu hugeuka
matajiri na hatimaye kuliumiza taifa kama anavyorai kijana
aliyeandamana na Mkubwa.
F Wabwia unga husinzia mchana. Hukauka midomo. Hujidunga
mili yao ikawa kama jahazi la mtefu. Zaidi ya mno vijana
hawa hujitoboa mishipa ya damu ikashabihiana na chungio.
F Vijana wanaojihusisha na biashara hii haramu huishia kwenye
seli. Wanafungwa miaka mingi huku wakuu wao
wakiyafurahia maisha yao nje.
1) UFISADI
Usadi ni uovu ambao umejitokeza katika hadithi kama
ifuatavyo;
F Pindi tu viongozi wanapopata pasipoti ya kidiplomasia wao
hujiingiza katika biashara haramu za kuuza dawa za
kulevya. Mkubwa aliweza kupita vizuizi vyote akiwa
ameubeba mkoba wenye dawa hizo na hakusachiwa.
F Mkubwa alipungiana mkono na wale askari ndani ya gari ;
pungiano hili lilikuwa na maana yake. Baadaye Mkubwa
alifanya mikakati na kumtoa Mkumbukwa ndani alikokuwa
amefungiwa. Bila shaka aliwahonga askari wamweke
Mkumbukwa huru.
F Vijana wanaopewa kazi ya kuviuza vidonge vile
wanapokamatwa hutiwa magerezani na kuwaacha viongozi
walanguzi wakiendeleza shughuli zao.
(mwanafunzi aongezee hoja ili kuonyesha namna usadi
unavyojitokeza)
108.
1) UONGOZI MBAYA
Uongozi wa Mkubwa ulikuwa uingozi mbaya kwani;
FAlishiriki usadi- alitumia ushawishi wake kisiasa kumtoa
Mkumbukwa ndani na kuuokoa mzigo wake(dawa za
kulevya)
FAlikuwa akiuza dawa za kulevya- sababu kuu ya Mkubwa
kujiingiza mamlakani ilikuwa ni utajiri na unga(dawa za
kulevya). Alimwingiza Mkumbukwa kinaki kwenye
biashara hii.
FViongozi hawasachiwi kwenye viwanja vya ndege na hivyo
basi kuwarahishia mipango ya kubeba dawa za kulevya.
Idara yauchunguzi imefeli.
FIdara ya magereza haijukumiki kuwaweka ndani vigogo
wanaolangua dawa hizi. Wao huwaweka ndani vidagaa.
(mwanafunzi aongezee hoja)
2) DHULUMA
Vijana mahabusu walio magerezani wanadhulumiwa kama
ifuatavyo:
F Wanalazwa chini kama magunia ya viazi mbatata.
F Wakiwa mle ndani kwenye vyumba vya mahabusu
wananyimwa chakula,hawakogi,hawafui nguo zao,
F Vijana hawa huhukumiwa kabla na kufungwa pasi
kupewa nafasi ya kujitetea
F Vijana hawa huteswa sana kwani hata chakula
wanachokileta jamaa zao huliwa na walinzi wa
magereza.
F Viongozi huwauzia dawa vijana ambao huathirika si
haba. (tazama athari za dawa za kulevya)
ZOEZI
· Jadili maudhui yafuatayo kama yanavyojitokeza katika
hadithi ya Mkubwa.
a) Ajira na kazi
b) Tamaa
109.
FANI
Katika Fani tutashughulikia mbinu za uandishi pamoja na tamathali
za usemi.
1. Ndoto:
Mkubwa aliota alipojilaza kwenye kochi lake. Katika ndoto hii
mambo yafuatayo yalijitokeza;
F Vijana wanaotumia dawa wameathirika mno kwani
walikuwa wakisinzia tu.
F Baadhi ya vijana(wake kwa waume) wamekondeana
kana kwamba wanaugua ukimwi au kifua kikuu.
F Vijana hao walikuwa wac hafu na walikuwa
wakivitenda vitendo vichafu vya kihayawani.
F Watu wengi aliowaona hawakuwa na raha kwani wizi
ulikuwa umewazidi.
F Nyumba zote zilikuwa zimechanwa nyavu.
F Vijana aliowaona wote walikuwa wameandikwa
kwenye vipande vya nyuso zao “mla unga”
F Mkubwa aliwaona watoto wake wa kiume miongoni
mwa vijana hao.
2. Tashbihi
Tashbihi zimetumiwa kwa mapana na mwandishi wa hadithi hii.
Mifano michache ya tashbihi ni kama
F Yule kijana alipita kama umweso…
F Majumba makubwa yamefumuka kamau yoga…
F … akipeleka pumzi juu kama mtu aliyepanda…
F …yalimkaa kama ngoma ya kimanga…
F Yalitembea kichwani kama damu itembeavyo mwilini…
F …alilidaka begi la Mkumbukwa kama mwewe anavyodaka
kuku…
F Alipita kama umeme…
F Mkubwa alikuwa amesimama kama mlingoti wa bendera…
F Lilikwama kooni kama mtu aliyekuwa anakula vigae…
110.
3. Mbalagha
Maswali ambayo hayahitaji majibu moja kwa moja yametumiwa
mara moja moja na mwandishi kama ifuatavyo;
F Kwani ulikuwa mwavuli?
F Wapi?
. Onomatopea /tanakali
Mbinu hii imetumika kazini kama ifuatavyo.
FPopooooooo! Popooooooo! – kuashiria jinsi gari lilivyopiga
honi.
5. Utohozi
Mbinu ya kuyaswahilisha maneno ya lugha ya kigeni ili yatamkike
na kuandikika kama yale ya Kiswahili.
FPasipoti – kutokana na ‘passport’
FKidiplomasia- kutokana na ‘diplomacy’
FHusachiwi- kutokana na ‘search’
FProfesa- kutokana na ‘professor’
FBegi- kutokana na ‘bag’
FKiboksi- kutokana na ‘box’
FPresha- kutokana na ‘pressure’
6. Kuchanganya ndimi
Kuna mara kadha ambapo mwandishi amevichopeka vifungu vya
lugha ya Kiingereza katika muktadha wa mazungumzo. Kwa
mfano;
F Form four
F Birthday
F Brother
F Sober house
7. Kinaya
Kinaya ni kinyume na matarajio. Mbinu hii imejitokeza kama
ifuatavyo;
F Ni kinaya kuwa , ili kuwa kiongozi katika eneo la
Mchafukoge huhitaji kuwa umesoma kwani cha muhimu ni
pesa na kuwa mzalendo kwa chama chako(ukikatwa, damu
yako inakuwa rangi ya chama)
111.
F Ni kinaya kuwawanafunzi wa Profesa walimpa kura
Mkubwa ambaye hakuwa na masomo.
F Ni kinaya kuwa walanguzi halisi wa dawa za kulevya
huachwa huru( kama vile Mkubwa)na wanaofungwa ni vijana
wanaowafanyia walanguzi hao kazi.
(mwanafunzi aongeze hoja)
8. Takriri
Pia hujulikana ka uradidi. Lengo la kutumia mbinu hii huwa ni
kusisitiza ujumbe.
Mifano ya takriri ni kama ifuatayo;
F Halimezeki, halimezeki…uk 151
F Hapo hapo!…154
F Kifo,kifo,kifo…uk 150
F Unga!unga!…uk 142
9. Istiara
Tofauti na tashbihi, istiara huwa haitumii maneno ya ulinganisho
kama ‘kama’. Mbinu hii imetumika kama ifuatavyo.
F Magereza kuna vitawi vitupu- vijana wanofungwa
wameitwa vitawi
F …wao ni matela tu- vijana wanaowafanyia kazi vigogo
kama akina Mkumbukwa wanaitwa matela.
F …vichwa vya treni huachiwa…- viongozi (vichwa vya treni)
huachwa nje wakiendelea na biashara zao haramu.
(mwanafunzi aongezee hoja)
Zoezi
F Onyesha namna mbinu hizi zimejitokeza.
a) Nidaa
b) Chuku
112.
Maswali ya kudurusu.
1. “ Usiteketeze umati kama kuni zinavyoteketeza moto. Rudi,rudi
kwa Mola wako.”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Fafanua sifa za msemewa.
c) Tambua tamathali ya usemi iliyotumika hapo juu.
d) Ni kwa nini msemewa anatakikana kurudi kwa Mola wake?
Majibu
a) Msemaji wa maneno hay ni Mkumbukwa. Anamweleza Mkubwa.
Walikuwa kwake Mkubwa.
b) Msemewa ni Mkubwa. Ana sifa hizi.
I. Mwenye bidii- alikuwa akishughulisha na kazi ya kuuza pweza
wa kukaanga na baadaye akauza kipande cha ardhi ili kuingia
uongozini.
ii. Mwenye utani- anamtania utingo kuwa huwa haogi jambo
lililomfanya utingo kukimia kwa kuchekwa na abiria.
iii. Ni mtambuzi- aliweza kuelewa maana ya unga japo hakuwahi
tu kuona vituko vyake.
iv. Mwenye utu- alimpigapiga kijana mbwia unga aliyekuwa
ameinama kama kwamba anarukuu na kumuuliza iwapo
anaumwa.
v. Mwenye tama ya mali- alipotanabahi namna viongozi
wanavyotajirika kwa kuuza unga , maneno ‘unga na utajiri’
yalimkaa moyoni kiasi chake kukosa usingizi usiku huo.
I. Ni maskini- alikuwa akifanya biashara ya kuuza pweza
iliyokuwa na kipato kidogo . vilevile kabla ya kupata uongozi,
alikuwa na suruali na shati kipande papa
113.
ii. Ni sadi- baada ya kutia na kutoa, aliamua kufanya biashara
haramu ya kuuza dawa za kulevya biashara ambayo
huonekana kama ya kishetani. Vile vile alitoa kiasi kikubwa cha
pesa ili kuwashawishi wapiga kura kumpendelea na ndipo
akaupata ushindi.
iii. Mwenye msimamo dhabiti- baada ya kuyatia moyoni maneno
aliyopewa na kijana Yule kuhusu utajiri na unga aliamua
kutafuta kwa udi na uvumba na ndipo akamwendea rakiye
kwa jina Mkumbukwa.
iv. Ni msiri- mwanzoni hakumweleza Mkumbukwa sababu yake
kuutafuta uongozi.
v. Mwenye wasiwasi- aliogopa kuwa huenda kisomo chake
kingemzuia kupata uongozi
c) Tashbihi- Usiteketeze umati kama kuni zinavyoteketeza moto.
d) Amevitenda vitendo vingi viovu kama vile ;
F kuuza dawa za kulevya.
F Kutoa hongo ili apate uongozi.
F Kumtapeli raki yake Mkumbukwa na kumuingiza katika
uuzaji wa dawa za kulevya. Kutumia pasipoti ya
kidiplomasia vibaya. nk
114.

Leave a Comment